Skip to main content

WATAALAMU ‘ECD’ WATAJA MBINU UJENZI WA UBONGO WA MTOTO MCHANGA

 



NA HAJI NASSOR, DODOMA

WAZAZI na walezi, wametakiwa kuzungumza na watoto wao wachanga kwa lugha rasmi, zinazozungumzwa na jamii yao, kwani kufaya hivyo, ni sehemu ya kuongeza makuzi, ufahamu na utanuzi wa ubongo wao.

Kwani, tafiti zimegundua kuwa, watoto hata wanapokuwa tumboni, wanauwezo mkubwa wa kusikia mazungumzo ya lugha yoyote, hivyo mara wanapozaliwa wazazi wawe nao karibu.

Muwezeshaji kwenye mafunzo ya Kitaifa ya Sayansi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto ‘SECD’ kutoka Mombasa Kenya Everlyne Okeyo, aliyaeleza hayo mjini Dodoma.

Alisema, watoto wanakosa ukuaji mzuri wa kutengeneza ubongo wao, kwa kule wazazi kutowashughulika kuzungumza nao, wakidhani hawana uwezo wa kufahama lugha zao.

Alieleza kuwa, makuzi mazuri ya awali ya mtoto, ni baina ya siku moja baada ya kuzaliwa hadi miaka minane, ambapo hapo huwa rahisi kwa wazazi na walezi, kuweke mwelekeo wa maisha ya mtoto.

‘’Wazazi waliowengi wamekua wanaanza kuweka nguvu zaidi za watoto wao, mara wanapokuwa na umri wa kuanza elimu ya awali, jambo ambalo sio sahihi,’’alifafanua.

Mwezeshaji huyo na mtaalamu wa malezi ya sayansi ya awali ya watoto ‘SECD’ alisema, tafiti zinaonesha kuwa, mtoto anauwezo wa kuzungumza zaidi ya lugha 600 mara anapozaliwa, ambapo hapo ni jukumu la jamii yake, kumuelekeza wanapotaka.

Katika hatua nyingine, Everlyne alisema, ubongo wa binadamu una nyuroni bilioni 100, na ndio maana mtoto mara anapozaliwa, huwa na asilimi 25 ya ubongo wake ni mtu mzima.

‘’Mtoto anapofikia mwaka mmoja, hufikia asilimia 60, wakati miaka miwili huwa na asilimia 75 na kuanzia miaka minne hadi sita, hubeba asilimia 90 ya uwelewa,’’alieleza.



Kuhusu mazingira, kama ya mtoto kucheza, kujumuika na wenzake na kujifunza, huchangia kwa haraka ukuwaji wa ubongo wake.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dk. Dorothy Gwajima, aliwataka waandishi wa habari, kuifikisha kwa jamii, dhana ya malezi ya kisayansi ‘SECD.



Alisema nguvu ya vyombo vya habari, vinaweza kuwa chachu kwa wazazi na walezi kufikiria sasa, namna ya kuwalea na kuwaandaa watoto kukabiliana na changamoto mapema.

Aidha waziri Gwajima, alisema bado ukatili wa watoto umekuwa mkubwa Tanzania, na ndio maana mwaka 2021 pekee walipokea matukio 11,499.

Kwa upande wake, mchechemuzi kinara wa ‘ECD’ kutoka Umoja wa vilabu vya waandishi wa Habari Tanzania ‘UTPC’ Victor Maleko, alisema tokea kuzinduliwa kwa mradi huo, habari 1,000 zimeshaandikwa.

Alieleza kuwa, kwa awamu ya pili baada ya kuwepo kwa mafanikio, umehusisha waandishi wa habari wa nchi nzima kupitia vilabu vyao 28 ikiwemo, kutoka Zanzibar.

Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Children in Crossfire, Craig Ferla, alisema mradi wa mtoto kwanza, umeleta mafanikio makubwa kwa wanafunzi wa elimu ya awali.



Alisema ushirikiano uliopo baina ya shirika lake na serikali, umepelekea kuwa na hamu ya kuendelea kuutekeleza, katika skuli mbali mbali nchini mradi huo.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo mkaazi, amempongeza waziri Gwajima, kwa kuendelea kushirikiana kwa karibu, juu ya kuwapatia malezi ya kisayansi watoto nchini Tanzania.

Meneja Mradi wa ‘ECD’ kutoka tasisi ya maendeleo ya binadamu kupitia Chuo cha Aga Khan, Joyce Marangu, amesema wameona sasa kuupanua mradi huo wa malezi ya kisayansi ‘SECD’ baada ya awamu ya kwanza, kufanikiwa.


Alisema ingawa bado baadhi ya mikoa haijafikiwa kikamilifu, lakini kutokana na ushirikiano uliopo, hana hofu na jambo hilo.

‘’Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa karibu mno na Chuo cha Aga Khan, na hili linatupa hamasa kuona mradi huu wa sayansi ya malezi na makuzi utafanikiwa,’’anasema.

Mafunzo hayo ya siku sita, yanayojumuisha washiriki 79 wakitoka mikoa kadhaa, yamehusisha waandishi wa habari, maafisa uastawi, maafisa maendeleo na watendaji wa asasi za kiraia.

                            Mwisho       

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch