Skip to main content

 

TAMWA - ZANZIBAR YAWAPA SOMO WAANDISHI WA HABARI HABARI ZA UDHALILISHAJI MAENEO YASIOPEWA KIPAOMBELE


 

NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

MRATIBU wa Program ya Mradi wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji wa "Tunaweza kwa pamoja  kutokomeza vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia" kwa wanawake na wasichana unaotekelezwa na  chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA -ZANZIBAR  kwa kushirikiana na UN - WOMEN, Asia Hakim Makame amewataka waandishi wa habari kutumia taaluma zao kuielimisha jamii juu ya masuali mbali mbali ya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na wasichana.

Alisema waandishi wa habari wanamchango mkubwa katika kutoa elumu ya kupinga vitendo vya udalilishaji wa kijinsia  kwa wanawake na watoto hususan katika sekta zisizo rasmini ikiwemo ya uchumi,elimu, afya na usafirishaji.

Aliyasema hayo wakati  akifungua mafunzo ya uandishi wa habari hizo yaliojumuisha waandishi kutoka vyombo mbali mbali vya habari watakao tekeleza mradi huo  yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa TAMWA Mkanjuni Chake chake Pemba.

Alisema kuna maeneo yenye vikwazo mbali mbali vya  udhalilishaji kwa wanawake na wasichana hivyo ni vyema kwa waandishi wa  habari kuiambia jamii  juu ya vitendo na  viashiria vitakavyopeleka udhalilishaji huo.

Aidha aliwataka waandishi hao kuyafikia maeneo ya umma  yanayotolewa huduma mbalimbali ikiwa pamoja na masoko, vituo vya afya, skuli na madrasa na katika maeneo ya usafiri wa umma,  kutokana na maeneo hayo kua na matukio mbali mbali ya udhalilishaji,  ambayo hayajapewa kipaumbele.

"Nguvu za kukemea jambo hili zielekezeni zaidi kwenye maeneo yasiopewa kipaumbele ikiwa ni pamoja na yenye mikusanyiko ya watu, huko kuna viashiria na matukio mengi ya vitendo vya udhalilishaji wa wanawake na wasichana ingawa wengi hawafahamu hilo,"alifafanua.

Alieleza kuwa  mradi huo unalenga kupunguza athari zitokanazo na  vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia  hususan katika Mikoa miwili ambayo ni KaskaziniPembana Kaskazini Unguja ambako kunaonekana kuwepo kwa tatizo hilo kwa kiwango kikubwa.

Akiwasilisha mada  kuhusu hali ya udhalilishaji kwa wanawake na wasichana katika mafunzo hayo Mkurugenzi Haji Nassor Mohammed alisema  takwimu zilizotolewa na Ofisi ya mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zinaonyesha kua wanawake na watoto ndio waathirika wakuu wa matendo ya udhalilishaji.

 Akitoa takwimu za matukio hayo kwa mwenzi Machi 2026 alisema jumla ya matukio 103 ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia yameripotiwa , huku  zikionyesha waathirika wengi ni watoto ambao walikuwa 84 sawa na asilimia 81.6 wakifuatiwa na wanawake 17 sawa na asilimia 16.5.

Alisema kuwa udhalilishaji hutokea katika namna tofauti tofauti ikiwa ni pamoja na matumizi ya lugha chafu, kupewa majina mabaya na hata matusi mambo ambayo huonekana ni ya kawaida katika jamii.

"Tukizungumzia udhalilishaji takwimu zinazoonyesha waathirika wengi ni wanawake watoto na wasichana,  ambao hupatwa na udhalilishaji wa namna mbali mbali ikijumuisha matumizi ya lugha chafu,  majina mabaya na hata matusi, ingawa jamii huyachukulia haya kama mambo ya kawaida,  alieleza.

Nao washiriki wa mafunzo hayo Mwamize Khadija Ali Yussuf na Salim Hamad Faki walisema mafunzo hayo yatawawezesha  kuibua , kufuatilia na kuielimisha  jamii  juu athari na namna ya kuchukua tahadhari na kujikinga na vitendo hivyo kwa wanawake na wasichana.

Aidha waliahidi kuyafanyia kazi mafunzo waliopewa ili kuikinga jamii yao na matendo hayo maovu,  ambayo kwa kiasi kikubwa huathiri uchumi na ustawi wa wanawake na wasichana.



                                                                            MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...