Skip to main content

ZNCC: YAWAKUMBUSHA WAJASIRIAMALI KUZISAJILI BIDHAA ZAO

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAJASIRIAMALI kisiwani Pemba, ambao bado hawajazisajili biashara zao, wamekumbwa kufanya hivyo haraka, ili wawe na sifa wakati wanapoomba misaada ama kuingia, katika mashindani mbali mbali.

Ushauri huo umetolewa leo Septemba 18, 2025 na Mkurugenzi mtendaji wa Jumuiya ya kitaifa ya wafanyabishara Zanzibar ‘ZNCC’ Hamad Hamad, alipokuwa akizungumza na wajasiriamali hao, wakati akiyafungua mafunzo, ya umuhimu wa usajili wa majina ya biashara na bidhaa zao, yaliyofanyika ukumbi wa Manispaa Chake chake.

Alisema, njia moja kwa wajasiriamali hao kufikia ndoto zao, suala la kusajili bidhaa zao na majina ya biashara, haliepukiki, ikiwa wana malengo ya kufika mbali.


Alisema, unapoisajili biashara na jina la biashara, huwa ni kuilinda na kujihakikishia kuipandisha hadhi, kama zilivyo kwa biashara nyingine za makampuni.

‘’Niwatake haraka sana, ambao hawajajisajili ‘BPRA’ kufanya hivyo, maana kinyume chake, jina la bidhaa zako ambazo zimeshakuwa maarufu kama hujazisajili, huna hakika ya kubakia nazo,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo mtendaji wa ZNCC, Hamad Hamad, aliwataka wajasiriamali hao, kujiunga na jumuiya hiyo, ili wawe na sauti moja, wanapokuwa na changamaoto zao.


Alieleza kuwa, ZNCC ndio mkombozi kwa wajasiriamali wote wa Zanzibar, na hasa ikiwa wataamua kujiunga, ili kuwa na suati ambayo, itasaidizi kuzipatia ufumbuzi changamoto zao.

Wakati huo huo, Mkurugenzi huyo Mtendaji, aliwahimiza wajasiriamali hao, kuendelea kutengenza bidhaa zitokanazo na zao la mwani, kwani bado soko lake liko juu.

‘’Na bahati nzuri kwa sasa baada ya suati zetu, serikali imesikia kilio chetu, na wameamua kujenga kiwanda cha kuusarifu mwani, na kuachana na kuzalisha na kuuza kama ulivyo, jambo ambalo faida ilikuwa ndogo,’’alifafanua.

Mapema mtendaji kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Mali Zanziba ‘BPRA’ Pemba Yussuf Juma Ali, alisema suala la kusajili jina la biashara ni lazima, kwa mujibu wa sheria, ili kuepusha mvutano na wafanyabishara mwingine.

Akiwasilisha mfumo wa kielektroniki unaobeba taarifa za bidhaa husika ‘barcode’ mtendaji kutoka Jumuiya ya kitaifa ya wafanyabiashara Zanzibar ‘ZNCC’ Tumai Soud, alisema mfumo huo ni muhimu, katika kuipa thamani bidhaa husika.

Alisema, mfumo huo ndio chanzo kwa mteja kuinunua bidhaa husika, kutokana na kumpa taarifa zote, aina ya bidhaa, malighafi iliyotumika na muda wa mwisho wa matumizi.




‘’Suala la msimbomlia ‘barcode’ ni vyema nyinyi wajasiriamali mkaweka, ili kuhakikisha bidhaa zenu, zinakuwa zinawavutia wateja,’’alifafanua.

Aidha mtendaji huyo, aliwafahamisha kuwa, namba za biashara ‘barcode’ kwa Tanzania huanzia nambari 620 na kufuatiliwa na namba nyingine, wakati kwa Kenya inaanzia nambari 616.

Mjasriamali Fatma Abdalla Nassor, alisema wakati umefika kwa BRA, ZBS, ZNCC kuwangalia kwa jicho la huruma, ili kuwapunguzia gharama za usajili.

Kwa upande wake mjasiriamali kutoka Kifumbikai Wete, Fatma Nassor, alisema bado ZBS, wamekuwa wazito kuwahudumia, jambo linalowarejesha nyuma.


Mafunzo hayo ya siku moja, yaliowashirikisha wajasiriamali 53 kutoka wilaya nne za Pemba, yameandaliwa na ZNCC ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mpango kazi wa 2020/2025.

                    Mwisho  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...