Skip to main content

OTHMAN ATAJA MAMBO MANNE YA KUIFUNGUA PEMBA KIUCHUMI

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya ACT- Wazalendo Othman Massoud Othman, amesema kama akipata ridhaa ya kuingoza Zanzibar, atasimamisha utawala wa sheria na haki, ikiwa ni njia moja wapo ya kukuza uchumi.

Alisema, haiwezekani wananchi kupata maendeleo endelevu, kama hakuna utawala wa sheria, ambao utawahakikishia wananchi kubaki na mali zao ikiwemo ardhi.

Mgombea huyo wa urais wa aliyasema hayo jana Septemba 18, 2025, uwanja wa mpira wa Mpika tango Mkoani, wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho, wa kampeni.

Alisema, utawala huo wa sheria, utakuwa na mambo kadhaa, ikiwemo kila mmoja kupata heshima ya kufanya shughuli zake, kwa mujibu wa sheria.



Alieleza kuwa, kufanya hivyo ni kuifungua Zanzibar kiuchumi, kutokana na watu kuheshimiana na kutunza amani na utulivu miongoni mwao.

‘’Kama nikiingia mdarakani, nitahakikisha, kwanza tunakuwa na utawala wa kuheshimiana, ambao ndani yake utamuhakikishia kila mmoja mali yake ikiwemo ardhi kutoporwa,’’alieleza.

Aidha Mgombea huyo wa urais, alisema katika kufikia uchumi wa kweli, suala la ujenzi wa bandari za kisasa katika miji ya Mkoani na Wete ni lazima.

Alisema, ili kisiwa cha Pemba, kifunguke kiuchumi, ujenzi wa bandari ya kisasa itakuwa ndio kipaumbele chake, ili mzungumko wa watu uwe mkubwa.

‘’Nafahamu kuwa, ili maendeleo yapatikane, mzunguruko wa watu ni jambo lazima, na watakuja kama miundombinu ya milango ya kiuchumi iko vizuri,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, alisema njia nyingine ya kuifungua Pemba, ni kuanzisha mpango maalum ‘Cluster program’ ambao utasaidia kuwa na maeneo ya ujenzi, wa nyumba za kisasa kwa gharama nafuu.



‘’Ili kukifungua kisiwa cha Pemba, suala la uwepo wa nyumba za kisasa tena za gharama nafuu kila eneo, haliepukiki, na hili ni kwa ajili ya watakaokuja kibiashara,’’alifafanua.

Mgombea huyo wa urasi wa Zanzibar kwa tiketi ya ACT-Wazalendo Othman Massoud Othman, alisema njia nyingine ya kuifungua Zanzibar, ni kurahisisha mawasiliano ya kimtandao.

Alisema, lazima katika kufikia hilo, kuwepo kwa eneo la kupata huduma ya intanet bure litazingatiwa, ili mawasiliano yasiwe changamoto kuelekea kukua uchumi wa kati.

Alisema, kwa sasa wananchi wanapoingiza bando la shilingi 1000, linachukuliwa kwa haraka, jambo ambalo ni changamoto kwa wananchi.

Aidha, alisema katika kufikia hayo, ni vyema wananchama wa chama hicho, kuwapa kura wagombea wote wa ACT-Wazalendo, kuanzia madiwani, wawakilishi, wabunge na rais wa Zanzibar.   



 


Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Zanzibar Ismail Jussa Ladu, amesema kwenye amani na utulivu wao wanaweza kuwa wa mwanzo.

Alisema, suala la kutunza amani, mamlaka zisiwe na wasi wasi, kwa wanachama wa chama hicho wataunga mkono, na hawatokubali kuchokozeka.

‘’Wanachama wa ACT-Wazalendo, suala ka kutunza amani ni jambo la kawaida kwetu, na na kuomba haki itatendeka katika mchakato wa uchaguzi mkuu,’’alifafanua.

Nae Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Omar Ali Shehe, alisema ili chama hicho kishinde, suala la kujitokeza kupiga kura, ni lazima kwa kila mmoja.





Alieleza kuwa, ACT-Wazalendo haina wasiwasi na ushindi, kutokana na mtaji wake mkubwa wa kuwa na wanachama wingi, ambao wataingia kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu.

‘’ACT-Wazalendo, kulekea uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, suala la ushindi kwetu halina shaka, ninachowaomba mwende mkapige kura,’’alifafanua.





Wakati huo huo Mwenyekiti wa chama mkoa wa Mkoani Mohamed Ali, amesema suala la kuendesha uchaguzi kwa njia ya kistaarubu, iwe ni lazima kwa kila mmoja kutunza amani.

                  Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...