Skip to main content

WANANCHI CHAKE CHAKE WAUMISHA VICHWA AJALI ZA BODA BODA

 


NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@


WANANCHI wa kijiji cha Ole Kianga wilaya ya Chake chake, wamesema ajali nyingi za barabarani zinasababishwa na waendeshaji wa  bodaboda kutokana na utumiaji mbaya wa  barabara wanapokuwa kwenye shughuli zao.


Wameyasema hayo leo Septemba 19, 2025 walipokuwa wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya uwepo wa ajali nyingi zikisababishwa na waendeshaji wa bodaboda.

 


Wakieleza kuwa ajali hizo kwa sasa zimekuwa tishio na kuwaweka roho juu, wanaotumia usafiri wa bodaboda kupitia vyombo hivyo.

 
Mpanda bodaboda Aisha Ali Abdullah alisema ni usafiri unaorahisha kwa sasa, ingawa wamekuwa hawana amani, kutokana na waendeshaji kukosa umakini.


Alisema kuwa ndani ya barabara kumekuwa na vyombo vya usafiri kila aina, ingawa kwa upande wa pikipiki aina ya bodaboda, zimekuwa zikihatarisha usalama wao.


Alifafanua kuwa waendeshaji bodaboda hao, weingi wao wamekuwa ndio chanzo kikubwa cha kusababisha ajali barabarani, kwani wamekuwa wakitumia barabara.


"Niseme dhahiri hawa waendeshaji bodaboda, ndio chanzo kikubwa wanaosababisha ajali kw akule kuwa matumizi ya kizembe barabarani,’’aliafafanua.

 

Kwa upande wake muendesha bodaboda katika kituo cha Ole Kianga Wahid Khamis Mohamed, alisema, sio sahihi kuwa, wao ndio chanzo cha ajali, kama wingine wanavyodai.


Alisema kuwa sio waendesha bodaboda wote wanaosababisha ajali, kwani inategemea na uendeshaji wa mtu na utumiaji wa chombo chake.


"Ijapokuwa, na sisi ni wadau wakubwa wa watumiaji barabara tunao na wenzetu, lakini chakushangaaza, pakitokea ajali tunaelekezewa kidole sisi,’’alilamika.

 

Mtumiaji wa usafiri wa bodaboda Maryam Mabrouk Khamis alisema wapo wale waendesha bodaboda wanaojita, majina sio mazuri, na wakiingia barabarani huendesha vyombo watakavyo wao.

 

Kwa mujibu takwimu, kutoka Ofisi ya Taifa ya Mtakwimu na jeshi la polisi ya matukio ya usalama barabarani kwa Zanzibar ni 49 zilizosabishwa na waendesha piki piki.

 


Ikafahamika kuwa, hizo ni zile zilizoripotiwa kwa mwaka jana pekee, ambapo ni punguzo la ajali12 ikilinganishwa na ajali 61 za mwaka 2023.

 

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, kwa ajali hizo zimesababisha vifo 37, ikilinanishwa na vifo 53 vilivyotokea kwa mwaka 2023, ambapo sawa na kupungua kwa vifo 16.

 

Aidha kwa mwaka jana, kuliripotiwa majeruhiwa 43, waliotokana na ajali hizo, ambapo kwa mwaka 2023, taarifa zinaonesha kupungua kwa majeruhi 12, baada ya kubainika kuwa ni 55.

 


Upande mwingine, taarifa ikafafanua kuwa, kwa Tanzania nzima, kwa mwaka jana pekee, kuliripotiwa vifo 378 vilivyosababishwa na ajali 432 za pikipiki.

 

Aidha kati ya ajali hizo pekee kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Disemba mwaka jana, ofisi hiyo ikaeleza kuwa, kulikuwa na majeruhi 395.        

 

                    Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...