Skip to main content

‘AAFP’ CHAWATAKA WANANCHI KUDUMISHA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

 


NA MARYAM SALUM, PEMBA @@@@ 

MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Wakulima, ‘AAFP’ Said Soud Said amewataka wananchi, kutokubali kushawishiwa na mtu au chama, kuchafua amani, na badala yake kuilinda na kuitunza kwa maslahi ya umma.

 

Alitoa wito huo wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara, wa kampeni kwa chama hicho, uliofanyika Kiuyu wilaya ya Wete Pemba.

 

Alisema kuwa, suala la uwepo wa uchaguzi wa vyama vingi, hakuna uhusiano wowote na uvunjifu wa amani, hivyo ni vyema kila mmoja kuliheshimu hilo.

 


Alieleza kuwa, siasa, mikutano ya kampeni na hatimae uchaguzi wa kuwachagua viongozi mbali mbali, ni jambo la kupita, ingawa kuichafua amani na kuirejesha ni jambio zito.

 

Mgombea huyo wa urais, aliwaasa wananchi hao na hasa vijana, kujitenga mbali na chama ama kundi la watu, lenye dhamira ya kutaka kuchafua amani ya nchi.

‘’Mimi nikiwa mgombea urais wa Zanzibar, niwaeleze kuwa, kwanza tuichaguweni amani na kisha ndio tuwapigie kura wagombea wetu,’’alifafanua.

 

Katika hatua nyingine, Mgombe huyo aliwaahidi wananchi wa Zanzibar, kama endapo atapata ridhaa, atahakikisha wale ambao walipata ajali ya kuzama kwa meli ya Mv.spice Island kutafuta familia zao na kuzilipa fidia.

 


Alisema, familia hizo ni sehemu ya wazanzibari, hivyo bado tokea zilipokumbwa na kadhia hiyo, hazipewa fidia, jambo ambalio analikusudia kulifanya.

 

‘’Naelewa kuwa, zipo familia ambazo zilipoteza wapendwa wao, lakini hadi leo hakuna fidia ambayo walipewa na serikali, lakini kama nitapata ridhaa, nitawasaidia,’’alifafanua.

 

Aidha sera yake nyingine ambayo aliinai Mgombea huyo, ni kuhakikisha anapandisha bei zao la karafuu na kunua kwa shilingi 40,000, ili kuwabufaisha wakulima.

 

Alieleza kuwa, ameona wakulima waliowengi wa zao la karafuu, wamekuwa hawanufaiki vilivyo na jasho, hivyo anaamini kama akiingia Ikulu, suala la kupandisha bei ni lazima.

 




Wakati huo huo Mgombea huyo wa urais wa kwa tiketi ya AAFP Said Soud Said, aliwahakikisha wananchi hao na wanachama wake kuwa, ataweka taa kwenye maeneo makubwa ya kuzikia.

 

Hata hivyo, aliwataka wananchi siku ya kupiga kura itakapofika kwenda kwenye vituo kupiga kura na kurudi nyumbani, na kuiacha Tume za uchaguzi kufanya kazi zake.

 


Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar, Omar Juma Said alieleza kuwa chama, kina dhamira ya kuwakomboa wananchi wote kiuchumi.

 

"Mgombea wetu kwanza ni mkulima, na kilimo ndio kila kitu, sasa tunahitaji ridhaa yenu ili aingie ikulu na kuhakikisha tunastawisha wananchi kiuchumi,’’alieleza.

 

 Aidha aliwataka wananchi wa Kiuyu kufikiria kwanza kabla ya kufanya maamuzi, ili waweze kuchagua kiongozi atakae waletea maendeleo na siyo kuangalia chama au mtu.

 

Nao viongozi wa Chama hicho kutoka katika Mkoa wa kaskazini na wilaya ya Chake pamoja na mgombea ubunge wa jimbo la Wawi, Khamis Mohamed Haji, walieleza kuwa si vyema, wananchi kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani.

Viongozi hao waliwataka wananchi wa Kiuyu na maeneo mingine, kuunga mkono chama cha AAFP, kwa kumchagua mgombea huyo, ili waweze kupata maendeleo zaidi.

 

        MWISHO. 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...