Skip to main content

ADC YAAHIDI KUWALIPA MISHAHARA WAALIMU WA MADRASSA ZANZIBAR

 


NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@


MGOMBEA urais wa Zanzibar wa tiketi ya chama cha Alliance for Democtratic Change ‘ADC’ Hamad Rashid Mohamed, amsesema moja ya kipaumbele chake, kama atapata ridhaa ya kuwa Rais wa Zanzibar, atahakikisha walimu wa madrsa kuwalipa mishahara kama, walivyo wafanyakazi wingine.


Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni za chama hicho, zilzofanyika uwanja wa Gombani kongwe Chake Chake Pemba.



Alisema kuwa atahakikisha walimu wote wa madrassa, atawalipa mishahara kama wafanyakazi wingine, pamoja kuwapatia vifaa vya TEHAM.



"Mukinipa ridhaa ya kuwa Rais wa Zanzibar, nitahakikisha walimu wote wa madrassa, nitawalipa mishahara kama wafanyakazi wengine wa utumishi wa umm," alisema.


Aidha Mgombea huyo, alisema kama atapata ridhaa hiyo, ataimarisha kilimo cha mpunga, ili kuhakikisha hakuna mwananchi anayenunua mchele.

 

Alieleza, kwa ardhi ya Zanzibar ilivyo kubwa, na kwa uzoefu wake wakati alipokuwa Waziri wa Kilimo, ana hamu kupata ridhaa, jambo hilo linawezekana mno.

 


‘’Nikiwa Rais wa Zanzibar, suala la kuimarisha kilimo hasa cha mpunga, ni jambo ambalo, nitalingalia kwa nguvu, kwani ni aibu kuona tunaagiza kila kitu kutoka nje ya Zanzibar,’’alifafanua.

 

Katika hatua nyingine, Mgombea huyo urais wa Zanzibar kwa tiketi ya ADC Hamad Rashid Mohamed, aliwataka wanachama wake, kutunza amani na utulivu kuelekea uchaguzi mkuu.

 



Mapema Mgombea urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa tiketi ya ‘ADC’ Wilson Elias Mulumbe na Mgombea mwenza wake, Shoka Khamis Juma, walisema kuwa, endapo watapata ridhaa, watahakikisha wanabadilisha katiba.


Alisema kuwa ndani ya siku100 mchakato huo utaanza  kubadilishwa kwa sheria hizo na kuanza kutumika, ili ziwe na mwalekeo mpya wa taifa.


"Tutabadilisha katiba mpya, ambayo mchakato wake tayari ulishaanza, hivyo itakuwa ni rahisi kwetu sisi ADC, maana ulishaanza zamani,’’alisema.

 

Nae Mwenyekiti wa wanawake taifa kutoka ADC Nadhira Ali Haji, aliwataka wanawake kuhakikisha, hawachokozeki na kuwa sehemu ya uchafuzi wa amani.

 



Alisema kuwa Tanzania ni nchi ya amani na utulivu na amewataka kuendeleza amani iliyotawala,  na kuiacha Tume  ya Uchaguzi kufanyakazi zake kwa uhuru.


"Niwatake wanawake wenzangu kudumisha amani na utulivu uliotawala nchini mwetu, na tuiache Tume ya Uchaguzi ifanye kazi yake,’’alifafanua.


Katibu Mkuu wa Chama cha ADC Taifa Mwalimu Hamad Azizi alisema, aliwahakikishia wazanzibari, kuwa endapo watamchagua mgombea Hamad Rashid Mohamed, atahakikisha amani na maendeleo ya nchi yatapatikana.





Nae Makamo Mwenyekiti wa ADC Tanzania Bara Hassan Shaaban Mvungi, alisema kuwa kiongozi pekee anaestahiki kushinda nafasi ya uraisi ni Hamad Rashid Mohamed, juu ya utekelezaji wa sera wa michezo, uchumi wa buluu, kuwezesha wavuvi kwa kuzalisha vitoweo kupitia biashara hizo.

 

     MWISHO. 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...