Skip to main content

MABADILIKO TABIA NCHI, YAWAUMIZA KICHWA WAKULIMA ZAO LA KARAFUU PEMBA

 


NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

WAKULIMA wa zao la karafuu kisiwani Pemba wamesema, kilimo cha zao hilo kwa sasa kimekabiliwa na changamoto kadhaa, ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, jambo linalosababisha kupungua kwa uzalishaji.

Waliyasema hayo wakati wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, kuhusu changamoto mbali mbali za uzalishaji wa zao hilo.

Walisema kwa sasa, wanakabiliwa na changamoto ya uzalishaji mdogo wa zao hilo, unaotokana na  kutostawi vizuri kwa mikarafuu wanayoendelea kuotesha, hali inayosababishwa na kuongezeka kwa jua na  joto kali.

Mmoja kati ya wakulima hao Said Mattar Mohamed alisema, kwa mwaka wa saba sasa, uzalishaji wa zao hilo umepungua, kwani mikarafuu iliokwishastawi vizuri na kutegemewa kuanza uzalishaji yamekua yakinyauka na kukauka.

" Sasa hivi sisi wakulima wa kilimo cha zao la karafuu, tunaathiriwa sana na mabadiliko ya tabia ya nchi, kwani mikarafuu iliokwishastawi vizuri na kutegemewa, kuanza uzalishaji yamekua yakinyauka na kukauka, kutokana na jua kali,"alisema.

Akieleza namna uzalishaji wa zao hilo, unavyopungua alisema, kuna baadhi ya mikarafuu mikubwa  waliokua wakivuna kiasi cha pishi 40 hadi 60 za karafuu mbichi, kabla ya miaka saba  iliopita, ambapo kwa sasa hawanavuni zaidi ya pishi 20.



Kwa upande wake mkulima Shaaban Haji alisema, mbali na uzalishaji mdogo wa zao hilo, kumekua na changamoto ya ustawi wake pamoja na kuingiliana kwa misimu miwili, hali inayosababishwa na mvua nyingi zinazonyesha bila ya mpangilio.

" Uzalishaji wa karafuu ni mdogo, kwa miaka hii ya karibuni, lakini pia ustawi wake sio mzuri, kama ilivyokua zamani, kutokana na kuathiriwa na mvua nyingi, mfano mzao huu tulionao karafuu nyingi zilianguka,’’ alisema.

Hivyo ameiomba serikali, kupitia wizara ya kilimo kuongeza jitihada kwa kuwapatia wakulima wa zao hilo mafunzo ya kitaalamu, ili kuwapa njia sahihi za kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Kwa upande wake mkulima Habib Khatib Faki wa Kangani alisema mbali na kututumia nguvu kubwa, kuekeza katika kilimo hicho ambacho ndio tegemeo, bado uzalishaji wake umepungua kwa kiasi kikubwa.

Alieleza kua lengo la kuwekeza kwao, ni kuongeza uzalishaji ili waweze kunufaika ipasavyo, kama lilivyo lengo la serikali la kuhakikisha wakulima wananufaika na kilimo hicho.

Afisa Maendeleo ya Kilimo wilaya ya Mkoani, Said Ali Hassan alikiri kuwa, mabadiliko ya tabia ya nchi, ni miongoni mwa changamoto inayowakabili wakulima wa zao hilo.





Alifafanuwa kuwa, baada ya kujitokeza kwa changamoto hiyo, wamekuwa wakichukua jitihada mbali mbali, ikiwemo kuwashauri wakulima kutoipalilia mikarafuu yao mara kwa maram ili kuzuia athari za joto.

Waziri wa Biashara na Viwanda Omar Said Shaaban, alisema Shirika la Biashara la Biashara la Taifa ‘ZSTC’ kwa mwaka 2023/2024 lilipanga kununua tani 4,940 za karafuu kavu, ingawa hadi mwezi Machi mwaka 2023, lilinunua tani 3,917.28.

Waziri alisema, sababu kubwa ya kushuka kwa ununuzi wa zao hilo kulitokana na mambo kadhaa, ikiwemo mabadiliko tabianchi, ambayo yamepelekea karafuu nyingi kununuliwa katika robo ya kwanza.

Aidha ZSTC kwa mwaka huo, lilipanga kununua makonyo tani 988, ingawa hivyo, hadi kufikia Machi 2023, halikufikia lengo na kununua tani 771.3, kulikosababisha na kushuka kwa uzalishaji wa zao la karafuu.                                                                    MWISHO

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...