Skip to main content

ACT- WAZALENDO KULIIMARISHA ZAO LA KARAFUU IKIINGIA IKILU

 


NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT- Wazalendo, Othman Masoud Othman amesema, atahakikisha wananchi wa Pemba, wananufaika moja kwa moja na rasilimali ya zao la karafuu ambalo ni uti wa mgongo wa uchumi wa Zanzibar.

Akiwahutubia wananchi kwenye viwanja vya Mchangamdogo Kambini Jimbo la Kojani, Mkoa wa Kaskazini Pemba Othman alisema, pamoja na karafuu kuwa ni zao la kimkakati, na lenye thamani kubwa duniani, bado linahitaji kufufuliwa ili kuleta tija zaidi kwa wananchi wa Zanzibar.

Alisema kuwa, Zanzibar ina uwezo wa kuzalisha zaidi zao la karafuu, ili liendelee kuwa ni mwega wa uchumi wa nchi, hivyo atakapopewa ridhaa ya kuiongoza nchi,  atalifufua zao hilo pamoja na mazao mIngine ya viungo kwa ajili ya kuiinua Zanzibar kiuchumi.

"Nitatafuta wawekezaji watakaokuja kununua karafuu hapa, hivyo zao hilo litaongezeka thamani na wananchi wataongeza vipato vyao," alisema mgombea huyo.



Aidha alieleza kuwa, wamejipanga kuwawezesha wavuvi ili waondokane na umasikini kwa kuwatafutia Teknologia za kisasa na vyombo vyao kutosha vya kuvulia, sambamba na kuwawezesha kuongeza thamani ya kile anachokivua.

Akizungumzia suala la uzalishaji wa chumvi, mgombea huyo alifafanua kuwa, Pemba imezungukwa na bahari ambayo inaweza kuzalisha chumvi inayohitajika duniani kote, hivyo atahakikisha kila mzalishaji ananufaika na fursa hiyo ili kujipatia kipato kitakachowasaidia kimaisha.

"Naahidi kuwekeza kwenye miundombinu ya kisasa ya uzalishaji wa chumvi, ili wananchi wa Pemba wapate kipato cha uhakika kupitia bidhaa hiyo," alisema.

Wakati huo huo aliwaomba wananchi kwenda kupiga kura ifikapo Oktoba 29 kwa ajili ya kumpatia ushindi huku akiwahimiza kutunza amani kwani ndio jambo la msingi wa maendeleo.



Awali, Meneja wa Kampeni wa ACT Wazalendo, Ismail Jussa Ladhu alisema, wanahitaji soko la karafuu huria litakalomfanya mwananchi na mkulima kuuza zao hilo anapotaka, kwani itasaidia kuwa na ushindani wa masoko, jambo ambalo litakuza kipato kwa wananchi.

"Zao la karafuu linalotoka kisiwani Pemba ni lenye thamani kubwa kuliko nchi nyengine yeyote, hivyo tutawaleta wawekezaji kuja hapa kununua bidhaa hiyo," alieleza.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Zanzibar kupitia Chama hicho, Omar Ali Shehe aliwataka wananchi waende kupiga kura kwa ajili ya kuchagua kiongozi wao, kwani uchaguzi ni fursa na ni haki ya kila raia kupiga kura.

Nae Mwenyekiti wa Mkoa wa Wete kichama Juma Khamis Ali aliwahamasisha akinamama kuwashawishi waume zao waliokwenda dago, kurudi kisiwani Pemba ili itakapofika Oktoba 29 wakapige kura.

                         MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...