Skip to main content

UZINDUZI KAMPENI ZA CCM PEMBA, RANGI NJANO, KIJANI ZAANZA KUWACHANGANYA WAPINZANI, NDEGE YANOGESHA UTAMU

 



          

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ 

SHANGWE, nderemo na vifijo vimetawala katika kiwanja cha Gombani ya Kale, wilaya ya Chake Chake Pemba, baada ya maelfu ya wanachama na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi ‘CCM’ wakiwa na kijano na njano kujitokeza kwa wingi kushuhudia uzinduzi wa kampeni za chama chao.

 

Umati huo uliofurika leo Septemba 15, 2025 unaashiria mshikamano na imani kubwa ya wananchi walioionesha kwa CCM kupitia mgombea wake Dk. Hussein Ali Mwinyi kuelekea uchaguzi mkuu mwaka huu.

 

 Kiwanja hicho kilipambwa na rangi za kijani na njano huku vijana, wanawake, wazee wenye mahitaji maalu, waliovalia rangi hizo walionekana barabarani wakitembea kwa furaha.

 

Mbali na dufu uwanjani, kulipambwa na vikundi vya ngoma, muziki wa hamasa huku bendera za chama hicho, zilizokuwa zikipepea kila kona.

 

Kwenye uwanja huo, usipokuwa makini kutokana na kushimari na kuenea kwa burudani, huwezi kujua ucheze na uitikie kikundi kipi cha ngoma uwanja hapo.

 


Lakini wingine, waliovalia vazi maalum, ambalo liliunga na sare za CCM, walionekana wakiimba na kucheza nyimbo za kampeni zinazomsifu mgombea urais wa Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi.

 

Shangwe la wana CCM lilionekana kama kutaka kuzima kidogo, ingawa bila ya kujali kijua kikali uwanjani, yalipoingia majira ya saa 7:30 mchana, nderemo zilidia, baada ya kupita ndege ya mgombea urais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi.




Ndege hiyo, ilipita kwa madaha, ikiwa imepambwa na picha za mgombea huyo, huku ikipeperusha bendera maalum, na kuzungumka eneo la uwanja wa kampeni na mitaa ya kisiwani Pemba.

 

Wakizungumza jana na Zanzibar Leo, uwanja hapo walisema, wanananchi kisiwani Pemba sasa wameamka, na kamwe hawatakubali kupelekeshwa tena kutokana na maendeleo yanayofanywa.

 

Walisema Pemba ya leo si ile ya miaka iliyopita, kwani chini ya uongozi wa Rais Dk. Hussein Ali Mwinyi, kumekuwa na mabadiliko makubwa ya kimaendeleo, katika kila sekta.

Mkaazi wa Chake Chake Mohamed Salim, alisema miradi ya barabara, afya, elimu na upatikanaji wa maji safi na salama, ni ishara nyingine ya ushahidi tosha kwa CCM na wagombea wake wote.

Nae Maryam Haji Makame wa Wawi, alisema  barabara zilizojengwa na kufanyiwa ukarabati, zimeongeza urahisi wa usafirishaji wa bidhaa na abiria kati ya vijiji na miji mikuu ya Pemba.

"Hawa wapinzani kila siku wanatupelekesha tu, wao wanachojali ni matumbo yao wala hawatufikirii sisi wananchi, lakini ndani ya miaka mitano ya Dk.Mwinyi,  maendeleo tunayaona,’’alisema.

 

Alisema, wanachokijua Chama cha ‘ACT-Wazalendo’ ni kuhamasisha vurugu na sio kuwaletea maendeleo, kwa sababu kiongozi mkuu anaposimama jukwaani ni lawama na kukebehi yaliofanywa.

 

Naye Asha Abdalla wa Mkoani alisema, sekta ya afya imeimarika kupitia ujenzi wa vituo vipya na upatikanaji wa dawa kwa urahisi huku wagonjwa wanaolazwa wakipatiwa huduma za matibabu na chakula bila ya malipo.

Naye Ali Khamis mkaazi wa Wete, alisema sekta ya elimu, imepiga hatua kubwa kutokana na ujenzi wa skuli mpya za ghorfa na kuimarika kwa mazingira ya kujifunzia.

Aidha, Fatma Omar wa Micheweni alisema, kuwa huduma za maji safi, zimefikia maeneo mengi, hivyo kupunguza adha ya kutembea umbali mrefu kutafuta huduma hiyo.

Alisema wana kila sababu ya kumuunga mkono Dk. Mwinyi, kutokana na jitihada zake za kuiletea Pemba maendeleo endelevu, na fursa za kiuchumi kwa wananchi.

Alawi Makame Alawi alisema yeye siyo mwanachama wa CCM, lakini ifikapo Oktoba 29, atampigia kura Dk. Mwinyi, ili aendelee kuwaletea maendeleo wananchi kwa ujumla.

 

Naye Faki Hamad Ahmada alisema, Pemba inajivunia mema mengi, yaliyoletwa na Dk. Mwinyi na kubwa zaidi ni amefanikiwa kuwaunganisha wananchi na kuwa wamoja, na kuondoa misuguano ya kisiasa.

 

Kisha mgombea huyo wa urais aliwasilia uwanjani hapo, na kupokelewa kwa shangwe kubwa, huku wajumbe halmshauri kuu ya CCM taifa, wenye viti wa mikoa, wilaya, watia nia ya nafasi kadhaa wakiungana pamoja.

                                MWISHO

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...