Skip to main content

'KIST' CHAFUNGUA TAWI PEMBA, VIJANA WAITA KUJIUNGA



NA ZUHURA JUMA, PEMBA @@@@

MAKAMU wa Pili wa Rais wa  Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla  amesema, kufunguliwa kwa Tawi la Taasisis ya Sayansi na Teknolojia ya  Karume Pemba kutasogeza kwa karibu huduma za masomo ya sayansi na teknolojia kwa wananchi na kutoa fursa kwa vijana kujiendeleza kielimu wakiwa kisiwani Pemba badala ya kufuata masomo nje ya kisiwa hicho.


Ameyasema hayo leo Septemba 16, 2025 wakati akifungua Tawi la  chuo cha Sayansi na Teknolojia ya Karume Pemba katika viwanja vya Mnazimmoja Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba. 

 


Amesema, Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume inatoa mchango mkubwa katika kukuza taaluma ya Sayansi na Teknolojia ndani na nje ya nchi sambamba na kupata mafanikio mengi ikiwemo kuongezeka kwa wataalamu wa fani ya Sayansi na Teknolojia nchini na Barani Afrika kwa ujumla.

 


Alieleza kuwa, uwepo wa Tawi hilo kutafungua milango ya kuitangaza Pemba kielimu katika nyanja za sayansi na Teknolojia na kuwavutia watu wengi sambamba na kutoa fursa za kiuchumi kwa wananchi kutokana na wanafunzi watakaosoma chuo hicho watahitaji mambo mbali mbali ambayo yatachangia kuleta maendeleo ya kibiashara yatakayowaongezea kuongezeka kipato.

 

Makamu huyo alifahamisha kuwa, katika kuipa kipaombele sekta ya elimu Serikali kupitia Wizara ya elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, imekuwa ikiboresha sekta ya elimu ikiwemo kuimarisha miundombinu, ubora wa elimu na maslahi ya walimu ambayo yamechangia kupata mafanikio mazuri ya ufaulu kwa wanafunzi wazanzibar.

 


Aidha, alisema Serikali imeongeza bajeti ya Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu Zanzibar hadi kufikia shilingi bilioni 37.5 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 ambayo itawanufaisha zaidi ya wanafunzi elf 14 wakiwo wanafunzi wapya na wanaendelea kupatiwa mikopo na wanafunzi wa ngazi ya diploma pia watanufaika na mikopo hio.

 

"Sambamba na hayo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleo kuimarisha sekta ya elimu kwa kuiongeza bajeti ya Wizara ya elimu hadi kufikia shilingi bilioni 864 kwa mwkaa wa fedha 2025/2026 kwa lengo la kuendeleza mapinduzi ya kielimu nchini, ili kuendana na mabadiliko ya kielimu na soko la ajira duniani," alieleza.

 

Waziri wa elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Lela Mohamed Mussa amewatoa hofu wakufunzi pamoja na  wanafunzi wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Pemba kuwa Tawi kubwa na la kisasa litajengwa kisiwani humo, ili kutoa fursa kwa wananfunzi kujisomea vizuri na kwa ufanisi wa hali ya juu.

 


Waziri Lela alisema, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar itahakikisha chuo cha KIST kinaendela kutoa taaluma yenye ubora na viwango vinavyokubalika vitakavyowawezesha wahitumu wa chuo hicho kuweza kufanya kazi mahala popote duniani.

 

Aidha Waziri Lela amewataka wazazi na wananchi kwa ujumla kuitumia fursa ya uwepo wa tawi la KIST kisiwani Pemba kwa kuwasajili vijana wao kujiunga na chuo hicho na kuamini kuwa elimu inayotolewa hapo ni sawa sawa na elimu inayotolewa katika vyuo vinavyotoa taaluma kama hio nje ya kisiwa cha Pemba.

 

Kwa upande wake Mkuu wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST) Dk. Mahmoud Abdulwahab Alawi alisema KIST imejikita katika kutoa mafunzo mbali mbali yanayohusu sayansi na teknolojia yakiwemo pia mafunzo ta muda mfupi, ili vijana waweze kujifunza na kufanya kazi zao kwa kujiamini kitaaluma.

 

Dk. Mahmoud alieleza kuwa, katika kuunga mkono juhudi za Serikali za kuifungua Pemba kiuchumi na kielimu KIST imeamua kufungua Tawi lake kisiwani hapa, ili kuhakikisha wanatoa fani mbali mbali za sayansi na Teknolojia ambapo kwa sasa wanafunzi 90 wameshajiunga na chuo hicho.

 

Alisema, Tawi la KIST Pemba limenza kutoa mafunzo ya cheti ambapo uongozi wa Taasisi hiyo upo katika mchakato wa kuanzisha mafunzo ya ngazi ya Diploma, ili kuwawezesha wanafunzi wanaoishi kisiwani Pemba kujiunga, ili kuwapunguzia gharama za masomo.

 


Nae Mwenyekiti wa bodi ya Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST) Dk. Afwa Khalfan Mohamed alifafanua kuwa, kuanzishwa kwa Tawi la KIST Pemba kumeondoa kilio cha muda mrefu cha wananchi wa Pemba ambao walihitaji kufunguliwa kwa Tawi la chuo hicho, ili kuwapunguzia  gharama za ada ya masomo pamoja fedha za kujikimu wanapokuwa vyuoni.

 

Alisema, kwa sasa Taasisi hiyo inafanya kazi zake katika jengo la kukodi ambalo halitoshelezi kutoa mafunzo ya ngazi ya cheti hadi diploma kama ilivyo malengo ya chuo hicho, hivyo ameiomba Serikali kusaidiwa upatikanaji kwa jengo la kudumu ambapo tayari eneo la kutosha kwa ajili ya ujenzi limeshapatikana.

 

                        MWISHO.


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...