Skip to main content

UZINDUZI KAMPENI CCM PEMBA, WAANZA KWA NEEMA YA USHINDI, 453 KUTOKA ACT WAMFUATA DK. MWINYI

 

 
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

 MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema akipata ridhaa ya kuongoza nchi, miaka mitano ijayo, anakusudia kuwapa hatimiliki wakulima wa zao la karafuu, wanaomiliki mashaba ya eka.

 

 Dk. Mwinyi aliyasema hayo jana Septemba 15, 2025 katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CCM katika kiwanja cha Gombani ya Kale, wilaya ya Chake chake kisiwani Pemba.

 

Alisema hatua hiyo itawezesha wamiliki hao kuzalisha kwa wingi na hata pale watakapofariki basi, warithi wao wanaweza kuyarithi, kisheria kwa ajili ya kuyaendeleza.

 

Mgombea huyo alisema CCM ikiendelea kushika dola basi hayo yote yatatimia kwa asilimia 100, kama ilivyofanya kwa awamu iliyopita.

 


Alifahamisha kuwa, wamiliki wa mashamba hayo ya eka, wamekuwa wakipata changamoto kwa kule kuyatunza, kisha kukosa hata kukodishwa wao.


 

‘’Naomba mnipe ridhaa ya kuiongoza tena Zanzibar, na pamoja na mambo mingi, lakini nitahakikisha wanaoyashughulikia mashamba ya mikarafuu ya eka, wanapewa hati ya umiliki,’’alifafanua.

 

Aidha Mgombe huyo ambae pia ni Rais wa Zanzibar, alisema serikali, mwishoni mwa mwezi huu, inatarajia kumkabidhi mkandarasi kazi ya ujenzi wa uwanja wa ndege Pemba, pamoja na ujenzi wa barabara Chake chake- Mkoani.

 


Alisema hatua hiyo ni dhamira za serikali kuifungua Pemba kiuchumi, na kukiwezesha kiwanja hicho kupokea ndege kubwa za kimataifa pale kitakapokamilika.

 

Alisema mpango huo, utakwenda sambamba na kuendeleza ujenzi wa barabara ya Chake Chake Mkoani, hatua ambayo itaunganisha mikoa mbalimbali kisiwani humo, na kurahisisha shughuli za usafiri.

 

‘’Niwahakikishe wananchi wa Pemba, kuwa mwishoni mwa mwezi huu, natarajia kumkabidhi mkandarasi kazi ya ujenzi wa barabara ya Chakechake- Mkoani, pamoja na ule ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa Pemba,’’alisisitiza.

 


Aidha Mgombea huyo, alisisitiza dhamira yake ya kuendeleza amani, umoja na mshikamano na kuondoa aina zote za ubaguzi, ukabila au uasili kwa wananchi.

 

Alisema wakati anaingia madarakani, aliahidi jambo hilo kuondoa ukabila baina ya Unguja na Pemba, ukaskazini na ukusini na uasili, jambo ambalo amefanikiwa kwa asilimia kubwa.

 

Alisema nchi ili ipate maendeleo, ni lazima kuwa na amani na umoja mshikamano, na hakuna mbadala katika jambo hilo.

 

"Sisi tutaendeleza umoja wa wananchi wote, hili ndio jambo muhimu kwetu, ili nchi yetu iendelee kupiga hatua za kimaendeleo,"alisema.

 


Mgombea huyo alisema wananchi wa Zanzibar hawataki chuki, fitna na ubaguzi, bali wanataka amani na maelewano, na sio jambo jingine lolote  na wanaoweza kufanya hivyo ni CCM pekee.

 

Katika hatua nyingine, amewahidi wananchi hao, kama Oktoba 29, watampa kura za kumuwezesha kuwa Rais wa Zanzibar, ataendeleza ujenzi wa barabara, bandari, kuendeleza makundi yote ikiwemo, wakulima wa mwani, ili kuwawezesha kwa zana za kisasa na mikopo.

 

Aliahidi kuwa CCM itaendeleza kazi ya ujenzi wa skuli, ili kufikia lengo lake la wanafunzi wote kuingia mkondo mmoja pekee, na sio miwili, kama ilivyo hadi sasa kwa baadhi skuli za Zanzibar.

 

"Tutaendeleza kujenga skuli za sekondari na msingi, ili dhamira yetu ya watoto kuingia mikondo miwili sasa iwe basi,"alisisitiza.

 

Kuhusu huduma za afya, alisema serikali itaendelea kuweka vifaa tiba, katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani, hasa kuiwezesha kutoa huduma ya  upasuaji wa uti wa mgongo.

 

Kwa upande wa maakazi bora ya gharama nafuu, alisema ana lengo la kujenga nyumba 10,000 Unguja na Pemba, ili kuhakikisha watu wanapata makaazi mazuri, na tayari kumeshatengwa fungu maalum la bajeti.

 

Alitumia nafasi kujiombea kura na kuwaombea kura viongozi wengine wa CCM akiwemo mgombea uris wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, wabunge, wawakilishi na madiwani ili kwa pamoja, waweze kushirikiana katika kuleta maendeleo.

 


Nae Katibu Mkuu wa CCM taifa Balozi, Asha Rose Migiro, aliwaomba wazanzibari, kuchukua maoni ya viongozi wao, ili kuhakikisha Oktoba wanawapigia kura wagombea wote wa CCM, ili iendelee kuwatumikia.

 

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM taifa, Mohamed Aboud Mohamed, amempongeza mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi upitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, kwa kuendeleza maendeleo.

 

 Alisema Dk. Mwinyi ameonesha ubingwa wa kutekeleza Ilani ya CCM ya uchaguzi yam waka 2020/2025 kwa unyenyekevu, subira na kwa kuzingatia mahitaji ya wananchi wake.

 

Aboud amebainisha kuwa, kiongozi huyo amejikita katika kujenga mshikamano na umoja wa wazanzibari, jambo lililogusa nyoyo za wananchi wengi. 

 

Aidha, amewaomba wananchi kuwa Oktoba 29, 2025 wananchi watajitokeza kwa wingi kumpa kura Dk. Mwinyi pamoja na wagombea wengine wa CCM kutokana na kazi kubwa aliyoifanya. 


Alisema sasa ni wajibu wa wananchi kulipa ihsani kwa kutumia fursa ya kura, kuendeleza neema hiyo, kwani Dk. Mwinyi ameweka mikakati thabiti ya kuimarisha maisha ya wananchi, na kubaki nguzo muhimu ya kulinda misingi ya taifa. 

 

 ‘’Niwaombe wananchi kukataa watu wanaochochea chuki na mifarakano na shari unaoashiria umwagaji damu, maana hayo sio maendeleo yanayotafutwa,’’alifafanua.

 

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Mohamed Said Mohamed ‘Dimwa’ alisema mgombea urais wa Zanzibar kupitia CCM, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ndie kinara wa siasa za maendeleo ya Zanzibar, kutokana na dira na maono yake.

 

Alisema ilani ya uchaguzi ya CCM, imetoa mwelekeo mahsusi wa kuijenga Zanzibar mpya, yenye ushindani wa kiuchumi na ustawi wa kijamii, jambo linaloendana moja kwa moja na falsafa ya uongozi ya Dk. Mwinyi.

 

Alisisitiza kuwa, Ilani hiyo imejikita katika maeneo muhimu ikiwemo mapinduzi ya uchumi, kuongeza fursa za ajira, kuimarisha sekta ya habari na mawasiliano.

 

‘’Ustawi wa watu na jamii kwa ujumla pamoja na kuimarisha miundombinu ya usafiri ni nguzo kuu, zitakazohakikisha Zanzibar, inafikia hatua kubwa ya maendeleo chini ya uongozi wa Dk. Mwinyi na hasa akipata tena ridhaa,’’alifafanua.

 

Aidha alibainisha kuwa, ilani imeweka sehemu kuu ya kuchochea mapinduzi ya kiuchumi na kisiasa, kuongeza ajira na kupunguza umasikini, ambayo ni kipaumbele kikubwa.

 


Akizungumzia kuhusu amani, alisema kwa sasa ipo na maridhiano, mshikamano na demokrasia ya kweli na kuahidi CCM, itaendelea kufanya kampeni za kistaarabu kwa kuthamini umoja na utu.

 

Akizungumzia maendeleo yaliyofanyika kisiwani Pemba kwa miaka mitano iliyopita, alisema serikali ya awamu ya nane, imejenga skuli za ghorofa13 na kuajiri walimu 2,406 sawa na asilimia 40 ya walimu wote waliopo Pemba.

 

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdullah, alisema wazanzibari wamedhihirisha mapenzi waliyoyanyo kwa Dk. Hussein Ali Mwinyi, kutokana na maendeleo yaliofikiwa.

 

Alisema changamoto kubwa, ilikuwa ikiwakabili wananchi wa kisiwa hicho, wagonjwa wenye matatizo ya figo, ingawa kwa sasa, huduma za ugonjwa huo zinapatikana katika hospitali ya Abdallah Mzee, bila ya gharama.

 

 Hivyo, aliwaomba wananchi kisiwani humo, kuwachagua viongozi wote wa CCM na kutokubali kudanganywa na watu, ambao hawana muelekeo mzuri kwa wazanzibari, wakihubiri chuki na dharau kwa waanchi.

 

Mapema Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana, Mohamed Kawaida, alisema visiwa vya Zanzibar, kabla ya kufanyika kwa mapinduzi mwaka 1964, vilitawaliwa na mkoloni, ingawa baada ya chama cha ASP na kisha CCM kushika hatamu, maendeleo yalipatikana.

 


Alisema Rais Mwinyi ameimarisha sekta mbali mbali ikiwemo elimu, kwa kiwango kikubwa kwa ujenzi wa skuli za ghorofa, ambayo hayo ni mageuzi makubwa.

 

Wakati huo huo, mgombea huyo wa urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, aliwapokea wanachama 453 kutoka chama cha ACT-Wazalendo, baada ya kukihama chama hicho.

 

Aidha kabla ya hutuba yake, kulitanguliwa na shamra shamra kadhaa, ikiwemo tumbuizo za wasanii, nyimbo za hamasa na matembezi maalum ya vyombo vya moto.

 

                      mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...