Skip to main content

Dk. SAMIA AAHIDI MAKUBWA BANDARI YA WETE, UWANJA WA NDEGE PEMBA UMO

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’ Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema kama atapata ridhaa ya kutetea nafasi hiyo, ataijenga bandari ya Wete ili, iwe ya kisasa.

Mgombea huyo wa Urais, aliyasema hayo jana, uwanja wa Gomabani ya kale, wilaya ya Chake chake Pemba, kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni, kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Oktoba, mwaka huu.

Alisema, ili kuifungua Pemba hakuna budi suala la miundombinu ya bandari, ni lazim kupanuliwa, ili kurahisisha usafirishaji wa wananchi na mizigo yao.

Alisema, tayari fedha zake zipo, ambazo ni mkopo kutoka Korea, na anachosubiri ni kupata tena ridhaa ya wananchi ifikapo Oktoba 29, mwaka huu, aanze kazi.

‘’Niwahakikishie kuwa, mini na Dk. Mwinyi kama mtatupa ridhaa, basi moja ya eneo ambalo kwa Pemba, tutaliangalia, ni ujenzi wa bandari ya kisasa ya Wete,’’alisema.

Ahadi nyingine, ambayo Mgombea huyo wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema atakeleza ni ujenzi wa barabara ya Chake chake – Mkoani, pamoja na kuzimaliza zile nyingie saba, ambazo ujenzi wake unaendelea kisiwani humo.

‘’Hatuwezi kuzungumzia maendeleo ya Pemba, bila ya kuangalia miundombinu ya usafiri wa nchi kavu, na ndio manaa tunakusudia kuziharakisha, kumalizia barabara hizo,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Dk. Samia, alisema kama akipata ridhaa, anakusudia kuondoa matumizi ya mkaa, kuni, matumizi ya mafuta ya petroli, diseli na mafuta ya taa katika harakati za maisha ya kila siku.

Alifafanua kuwa, anakusudia hadi ikifika mwaka 2034, asilimia 80 ya watanzania, wawe wanatumia nishati safi, iwe kwa kupikia, kuonea na kwenye shughuli nyingine za kimaendeleo.

‘’Tunakusudia nisahti hizo, ziwe chanzo chake ni jua, upepo mabwawa ya maji kama la Mwalimu Nyerere, ambalo, litaunganishwa na gridi ya taifa, ili kuzalisha nishati safi,’’aliahidi.

Katika hatua hatua nyingine, Mgombea huyo wa urais, aliwahakikisha wananchi kuwa, vikosi vya ulinzi na usalama vitalinda amani na utulivu, kuelekea uchaguzi mkuu mkuu mwaka huu.

‘’Kila mmoja awe mlinzi wa mwenzake, juu ya kulinda amani, na baada ya kupiga kura rudini nyumbani, msubiri taratibu nyingine zifanyike,’’alifafanua. 

    


Aidha Dk. Samia alisema, CCM imekuwa ikitekeleza miradi zaidi kwa wananchi na sio, maneno kama baadhi ya vyama vinavyodai.

‘’CCM sio chama cha blaablaa, ni vitendo kwani inawatumikia wananchi wote bila ya ubaguzi wa aina yoyote,’’alifafanua.

Alisema, kwa sasa Pemba, inazo skuli za ghorofa pamoja na nyumba za waalimu, ikiwemo eneo la kisiwa cha Kojani wilaya ya Wete.

‘’Leo hadi kisiwa cha Kojani na maendeo mingine kama Konde, Kiwani, Michakaini zipo skuli ambazo ni za kisasa, na ni haya ni ushirkiano kati yangu na Dk. Mwinyi haoa Zanzibar,’’alisema.

Kuhusu yaliotekelezwa kwa miaka mkitano iliyopita na serikali zote mbili, alisema zimefanikiwa, kuweka mazingira ya uwekezaji, na kuwepo kwa viwanda kama vya maji, majani ya mkarafuu na kunuwafaisha wananchi.

Alieleza kuwa, kwa baada ya mazungumzo ya kideplomasia, sasa makontena ya bidhaa yanashushwa moja kwa moja katika bandari ya Mkoani Pemba, na kusababisha ahuweni ya bei ya bidhaa.

‘’Sasa meli kubwa hazishushi tena Unguja kwa bidhaa ambazo zinakuja Pemba, bali ni moja kwa moja, na hii ni mwanzo, lakini kwa miaka mitano ijayo, tutaimarisha zaidi,’’alifafanua.

Awali Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Asha Rose Migiro, alisema CCM ikiendelea kukaa madarakani, mafanikio makubwa yataendelea kupatikana.

Alisema, hayo yanaweza kufikiwa, ikiwa watanzania watampa kura Dk. Samia Saluhu Hassan na kwa upande wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi.

‘’Sio hayo tu, tunao wabunge, wawakilishi na madiwani wote kutoka CCM, ni vyema nao wakapewa kura ili kuwa safu imara ya kuliendelea taifa mbele,’’alifafanua.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM taifa, Hemed Suleiman Abdulla, alisema Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025, imetekelezwa zaidi ya ilivyopangwa, kwa Tanzania nzima.

Alisema, ipo miradi kama ya barabara, maji safi na salama, afya, elimu, uwezeshaji kiuchumi, jambo ambalo limenawirisha maisha ya wananchi.

Kuhusu Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, alisema amefanikiwa kusimamia umoja, mshikamano na kurahisisha maendeleo kwa wote.



Alieleza kuwa, Dk. Samia asiwe na cha kupoteza kwa wananchi wa Pemba, kama sehemu ya kumtunza, ili aiongoze tena Tanzania kwa miaka mitano ijayo.

‘’Miradi kadhaa iliyopo Pemba, Dk. Samia amehusika kwa njia moja ama nyingine, hivyo hakuna haja ya kumpa kura mgombea mwingine,’’alisema.

Alifafanua kua, ujio wa miradi hiyo ni kuimarisha ustawi wa wananchi kwa makundi, ama mmoja moja, ili kuhakikisha kila mmoja anaishi kwa furaha.

Hata hivyo, Mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya halmashauri kuu ya CCM taifa, aliwataka wananchi kutokochokozeka na kuendelea, kuilinda amani iliyopo.

‘’Niwasihi wananchi wenzangu, jambo moja na la muhimu kwetu, ni kuilinda amani na utulivu, ili kila kitu kifanyike kwa nafasi pana,’’alifafanua.

 Mapema Waziri ya Uchukuzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambea ni Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mkoani Prf: Makame Mbarawa Mnyaa, alisema, ujenzi wa uwanja ndege wa Pemba, ambao unatarajiwa kuanza wakati wowote, mwaka huu.

Alisema, utakuwa na urefu wa kilomita 2.5 ambao utajumuisha pia jengo kubwa la abiria, litakalo kuwa na uwezo wa kuhudumia abiria 300,000 (laki tatu) kwa mwaka.

Akizungumzia ujenzi wa barabara ya Chake chake- Mkoani, alisema ndani ya mwezi huu, Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, atazindua ujenzi wa barabara hiyo, kwa kumkabidhi mkandarasi kazi

‘’Barabara hii yenye urefu wa kilomita,43.5 itakuwa na njia nne, mbili za kwendea na mbili za kurudia, ambayo, itaunganishwa na ile ya Chanjaani- Uwanja wa ndege, itakayokuwa na taa maalum na za kisasa,’’alifafanua.

Aidha aliwaomba wananchi, kumpa kura za ndio Dk. Samia ili awe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Dk. Hussein Ali Mwinyi awe kwa upande wa Zanzibar.

Nae Mbunge mteule wa CCM kwa Mkoa wa kaskazini Pemba, Asya Sharif Omar, amesema kwa sasa hadi mama mtilie, wanaendelea kufaidika na matunda ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuwezeshwa kuichumi.

Kwa upande wake Maryam Azan Mwinyi kwa nafasi kama hiyo kwa mkoa wa kusini Pemba, alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuwapeleka TASAF, na kuwanufaisha wanawake na watu wenye uleamvu, na sasa wapo wanaojitegemea kupitia mpango huo.

Alisema, kwa sasa wapo wanawake, ambao wamekua na kipato cha hali ya juu, kutokana na kuingizwa kwenye mpango wa kunusura kaya maskini, na wakiendelea kujitegemea kibiashara.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kojani Pemba, Hamad Chande, alisema yapo mingi aliyofanya Dk. Samia, ikiwemo ahadi ya ujenzi ya uwanja wa ndege wa Pemba na barabara Chake chake Mkoani, na zaidi ya shilingi bilioni 886 zikitarajiwa kutumika.

Alisema, fedha nyingine ni shilingi bilioni 327, ambazo zinaendelea kutumika, kwa ujenzi wa bandari ya Shumba Micheweni, na kuifanya fedha yote ilioyoingia Pemba, kwa miradi hiyo, kuwa ni shilingi trilioni 1.26.

‘’Kwa haya ambayo Dk. Samia ameyafanya, nna hakika wananchi watamchangua ifikapo Oktoba 29, mwaka huu, nakurejea ili kuendeleza mema kwa watanzania,’’alisema.

Nae Mgombea Uwakilishi Jimbo la Konde Zawadi Amour Nassor, alisema kwenye sekta ya afya, sasa huduma zinatapatikana saa 24, ikiwemo chakula cha uhakika kwa wagonjwa.

‘’Huduma za afya zimeimarika, na moja wapo ni kuwepo kipimo cha kisayansi cha magonjwa ya ndani ya mwili na mishipa midogo ‘MRI’ ambapo hapo kabla, hakikuwepo,’’alisema.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa kusini Pemba, Yussufu Ali Juma, alisema hana wasiwasi wa Dk. Samia kurejea tena madarakani, kutokana na kutekeleza miradi ya kibinaadamu mkoani humo.

‘’Tumejengewa hospitali ya Mkoa ya kisasa yenye huduma muhimu, pamoja na ujenzi wa matenki mtatu ya kuhifadhia maji safi na salama, na kila moja likiwa na ujazo wa lita milioni 1,’’alifafanua.

Mjumbe wa kamati kuu ya CCM taifa, Mohamed Aboud Mohamed, alisema sasa watanzania wana heshima kubwa kimataifa, kutokana na maono na juhudi za Dk. Samia kwa kuwaunganisha na mataifa mingine.

‘’Kwa mfano filamu ya kiutalii ‘royal tour’ sasa imeifungua Zanzibar kiutalii, na kila mmoja anaendelea kunufaika na matunda ya utalii, hivyo ikifika Oktoba 29, mwaka huu kura ni kwako,’’alifafanua.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...