Skip to main content

SERIKALI YAAHIDI KUZISIMAMIA HAKI, FURSA ZA WATU WENYE ULEMAVU



NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@


Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, amesema serikali itaendelea kulijali kundi la  watu wenye ulemavu, ili kuhakikisha wanapatiwa haki zao msingi, ikiwemo za uongozi na uchumi.

 
Hayo aliyasema leo Septemba 16, 2025 kwenye hutuba yake, iliyosomwa kwa niaba yake na Katib tawala wilaya ya Micheweni Sheha Mpemba Faki, alipokuwa akifungua kongamano la wadau wa maendeleo jumuishi katika jamii, lililofanyika skuli ya Utaani Pemba.

Mkuu huyo mkoa alisema, serikali imewapa haki na fursa na kuwathamini pamoja na kuwaunga mkono, watu wenye ulemavu kama walivyo watu wingine.

 


Alieleza kuwa, watu wenye ulemavu wamepewa fursa kubwa ya kushiriki katika kupiga kura na kuchagua viongozi, wawatakao, kama msingi wa sheria mama katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, ilivyoekeleza kifungu cha 7 na ch 12.

 

"Niwatoe hofu nyinyi watu wenye ulemavu, mnayo fursa kubwa ya kushiriki kikamilifu katika harakati mbali mbali zikiwemo za kisiasa na uongozi,’’alifafanua.

Akizungumzia suala la amani, kuelekea uchaguzi mkuu, Mkuu huyo wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, alieleza kuwa serikali imejipanga kikamilifu, kusimamia amani na utulivu wa nchi, na kuondosha changamoto zote hatarishi dhidi yao.

 


Hata hivyo, alilipongeza shirikisho la jumjuiza za watu wenye ulemavu Zanzibar ‘SHIJUWAZA’ kwa kuzaa fikra ya kulileta kongamano hilo, wakati taifa likielekea uchaguzi mkuu wa vyama vingi.

 


Mapama Mkurugenzi Mtendaji kutoka shirikisho la jumuiya za watu wenye ulemavu,  Ali Machano alisema kuwa, juhudi kubwa zinachukuliwa na shirikisho hilo, ili kuhakikisha haki na fursa za watu wenye ulemavu, zinapatikna.



Alisema kuwa, wamekuwa mstari wa mbele kutetea na kupaza sauti zao, kupitia makongamano na mikusanyiko mbali mbali, ili kuhakikisha watunga sera na waandaji mipango, ujumbe unawafikia.

 

"Tumekuwa tukitetea haki na fursa za watu wenye ulemavu, kupitia makongamano, vyombo vya habari na hata mitandao ya kijamii, ili kuhakikisha changamoto hazijitokezi, katika maisha yao,"alifafanua.


Meneja Program kutoka shirikisho la jumuiya za watu wenye ulemavu, Sophia Azidihery Leghela alisema, lengo la kongamano hilo ni kujadili, namna bora ya watu wenye ulemavu wanashiriki kikamilifu katika maisha muhimu ya kiuchumi, kijamii na kimaendeleo.


Alisema kuwa jukwaa hilo la maendeleo jumuishi, linalenga kuwaweka pamoja viongozi wa serikali, asasi za kiraia, watu wenye ulemavu, mabaraza na jumuiya za watu wenye ulemavu.

"Jukwaa hili litasaidia kuibua changamoto zinazowakumba watu wenye ulemavu, na vipi tutaziimarisha haki na fursa zitakazowafikia, kusudi waishi maisha mazuri kama wingine,’’alifafanua.


Mratibu wa Baraza la taifa la watu wenye ulemavu Ofisi Pemba, Mashavu Juma Mabrouk alisema, serikali imekuwa ikiwajali mno, watu wenye ulemavu kwa kuwawekea chombo kinachosimamia haki na fursa zao.





"Mimi mjumbe la baraza la watu wenye ulemavu, kwanza niipongeze serikali, kwa kutuwekea chombo chetu kinachosimamia haki na fursa zetu, maana awali tulikuwa hatuna jukwaa la kupazia sauti zetu kwa pamoja,’’alifafanua.


Awali Afisa ufuatiliaji na tathmini Ofisi ya Mrajis wa NGO's Pemba Aziza Yussuf Saleh, alisema watu wenye ulemavu wanauhitaji mkubwa wa kupatiwa elimu, na haki zote za harakati za kisiasa.



Akilifunga kongamano hilo, Mwakilishi wa Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Pemba, Shaaban Mohamed Abdalla, alisema baraza, shirikisho na jumuiya za watu wenye ulemavu, zimekuwa na mchango mkubwa wa kusaidia, kutambulika kwa haki mbali mbali za watu wenye ulemavu.

 
Kauli mbiu la kongamano hilo ni "haki za watu wenye ulemavu ni haki za bnaadamu" hakikisha ushiriki wa watu wenye ulemavu kwenye siasa na uongozi.


   MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...