Skip to main content

WATU WENYE ULEMAVU WA UZIWI, WATAKA WAKALIMANI TAASISI ZA UMMA

 



NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

Watu wenye ulemavu wa Uziwi wameziomba taasisi Serikali na binafsi  zinazotoa huduma mbali mbali za kijamii, kuweka wa kalimani wa alama katika taasisi hizo ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora kwa watu wote.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti  watu wenye ulemavu wa uziwi walisema, wamekua wakichelewa  kupata huduma bora na stahili katika baadhi ya taasisi  kutokana na kutokuwepo mawasiliano mazuri kati yao na watoa huduma, hali inayosababishwa na upungufu wa wakalimani wa  lugha za alama katika taasisi hizo.

Mmoja kati ya watu wenye ulemavu wa uziwi Zuhura  Kombo Omar kutoka Mjimbini Mkoani Pemba alisema, katika taasisi nyingi za utoaji huduma za kijamii  kumekua na uhaba wa wakalimani wa lugha ya alama hali inayosababisha kutopata huduma bora na kwamuda sahihi.

Alisema kukosekana kwa wataalamu hao unasababisha kutokuwepo kwa mawasiliano mazuri jambo linalosababisha  kukosekana na kwa huduma bora pamoja na haki zao msingi ambazo ni lazima kuzipata.

" Tunapokwenda katika taasisi za utoaji huduma zikiwemo za serikali na zisizo za kiserikali tumekua tukichelewa au kutopata huduma stahili, kutokana na kukosamawasiliano sahihi hali inayosababishwa na  kutokuwepo kwa wakalimani wa lugha ya alama pamoja na watoa huduma wenye ujuzi wa lugha hio ,"  alisema.



Nae Mbarouk Ali Saleh kutoka Mtambile Mkoani Pemba alisema, changamoto za  kutokuwepo kwa wakalimani wa lugha za alama katika sehemu za kutoa huduma za jamii, kunasababisha baadhi ya watu wenye ulemavu wa uziwi  kushindwa kupata huduma stahili  kutokana na kutokuwepo watu wenyeuwezo wa kufahamu mahitaji yao.

Alieleza kuwa iwapo kila taasisi itaweka watoa huduma wenye taaluma ya lugha  za alama itasaidia kurahisisha mawasiliano pamoja na upatikanaji wa huduma bora kwa kila mmoja, jambo litakalosaidia ustawi wa jamii kwa ujumla.

Nae Fatma Kombo Omar wa Mjimbini Pemba alisema, mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu katika taasisi za utoaji huduma muhimu,  ni moja kati ya hatua muhimu katika kuhakikisha usawa na upatikanaji wa haki zao za msingi.

Aidha  aliiomba serikali kuhakikisha uwepo wa wataalamu wa lugha za alama katika taasisi hizo  ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora kwa watu wenyeulemavu wa uziwi.

" Mazingira rafiki kwetu ikiwemo wakalimani wa  lugha za alama ni hatua muhimu katika kuhakikisha usawa na upatikanaji wa haki na huduma bora, hivyo ni vyema kwa serikali kulizingatia hili ili kuhakikisha tunapata mawasiliano sahihi tunapofuata huduma, " alieleza.



Kwaupande wake  Mratibu Baraza la Taifa la watu wenyeulemavu Pemba Mashavu Juma Mabrouk alisema, nivyema kwa Serikali na taasisi zote za binafsi zinazotoa huduma kwa jamii kuweka wataalamu wa lugha za alama ili kurahisisha mawasiliano wakati wa utoaji huduma kwa kila mtu.

Aliongeza kua, baraza limekua likichukua jitihada kadhaa ikiwemo kuzishauri baadhi ya taasisi hizo ikiwemo wizara ya Afya  kuweka wakalimani wa lugha za alama katika taasisi hizo, lengo ni kujumuisha watu wote katika upatikanaji wa huduma mbali mbali nchi.

Kwa mujibu wa kifungu cha 32 (1) (d) cha Sheria ya watu wenye ulemavu ya Zanzibar ya mwaka 2022 kinaeleza kua taasisi yeyote ya Serikali au binafsi itahakikisha taratibu za utoaji na upatikanaji wa huduma zinazingatia mahitaji maalum ya watu wenye Ulemavu.

                                                      MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...