Skip to main content

ZAFELA YAJA NA JAMBO JEMA KWA WATOTO WA KIKE

 



NA FATMA HAMAD, PEMBA

MKURUGENZI wa Jumuiya ya Wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA,  Jamila Mahamoud Juma, amezitaka asasi za kiraia, kushirikiana kwa pamoja na kuwajengea uwezo watoto wa kike, waliyokatisha masomo, ili  waweze kurudi na kupata haki yao ya msingi.

Mkurugenzi huyo, aliyasema hayo katika mkutano wa kuutambulisha mradi wa Malala, utakaoendeshwa na ZAFELA, Zanzibar kwa muda wa mwaka mmoja, kikao kilichowajumuisha asasi mbali mbali za kirai kisiwani Pemba.

Alisema katika utafiti wao walioufanya, waligundu kuwa, kuna wimbi kubwa la watoto wa kike wamekuwa wakikatisha masomo yao, kutokana na sababu mbali mbali, ikiwemo kuolewa, kupata mimba za utotoni pamoja na kufanyishwa kazi za nyumbani.

Alisema, wamekuwa wakipokea kesi nyingi za watoto wa kike, kudai haki zao, aidha waliolewa au waliojihusisha na mahusiano, ambao ukiwangalia umri wao unapaswa   wawe wako masomoni.

‘’Tumeamua kuleta mradi huu wa ‘Malala’  kwa ajili ya kumuezesha na kumsaidia mtoto wa kike, ili aweze kurudi masomoni, na kumaliza masomo yake, angalau elimu ya lazima,’’alisema Mkurugenzi huyo.



Alifahamisha kuwa, mrahidi huo umelenga kuwafikia watoto 3,000 kwa Unguja na Pemba, hivyo amezitaka asasi za kiraia, kuzidisha ushirikiano wao na ZAFELA, ili kufikia lengo la mradi huo.

Aidha kwa upande mwengine Mkurugenzi huyo wa ZAFELA, aliwataka wanajamii kukaa karibu na watoto wao, na kuwasikiliza matatizo yao, ili wawe na uthubutu wa kueleza changamoto zinazowatokezea katika harakati zao za kimasomo.



‘’Inawezekana mtoto anaacha masomo kutokana na vikwazo tu vinavyo mkwaza aidha njiani au skuli, hivyo tujenge urafiki nao, ili tuwanusuru na kadhia kama hizo,’’ alifafanua.

Mapema Msimamizi wa mradi huo Hairun Abass Rajab kutoka ZAFELA, alieleza kuwa hadi sasa, bado zipo familia ambazo hazimpi fursa mtoto wa kike, kupata haki yake ya elimu kuanzia ya msingi hadi vyuo vikuu.

 


 Alifahamisha kuwa, lengo la mradi huo ni kuwasaidia watoto walioacha masomo, na walio katika mazingira magumu, ili kuhakikisha wanapata elimu na kufikia ndoto zao.

Akichangia katika mkutano huo, mwanaharakati wa kulinda na kutetea  haki za wanawake na watoto kutoka wilaya ya Mkoani,  Saada Mohamed Othman, alisema ni vyema kuweko na mkakati madhubuti ya kuwaekea usimamizi wa hali ya juu  wanafunzi hao.

‘’Kuna watoto waliokaa nje kwa muda mrefu, na tayari walishaathirika na ulevi, ulawiti, ubakaji, hivyo ni vyema tuwe makini nao, wakati tunapowarejesha masomoni,’’alifahamisha.



Nao washiriki Ali Mohamed Ali na Salim Said, walisema ili kumaliza vitendo viovu katika jamii, ni lazima kila mmoja kwa nafasi yake, kuchukua jitihada za makusudi, jambo ambalo litasaidia kupata kizazi chenye madili mema.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch