Skip to main content

HEDHI SALAMA KWA WANAFUNZI BADO KITENDAWILI, WAPO WANAOAZIMANA VITAMBAA

 

   

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

HEDHI ni damu maalum, anayotoka mwanamke pekee, mwenye umri maalum na kwa siku maalum.

Tena mwenye umri wa kubeba ujauzito, ambapo mabadiliko hayo, hata uwe fukara, fakiri, maskini na tajiri hujitokeza.

Naam….damu hii haitoki eneo jingine la mwanamke, bali ni kwenye sehemu yake ya uke tu, tena ni yenye rangi, harufu na uzito kama damu ya kawaida.

Tulishazoea kila atokae damu, huwa ni kwa ugonjwa, ajali, kuumia, ingawa kwa ii, ndio uzima na umadhubuti wa mwanamke kiafya.

KWA NINI DAMU HII ITOKEA?

Kwamba, kiyai kilichokomaa na kutoka nje ya kifuko kisipopata mbegu ya mwanamme ‘sperm’ baada ya siku moja, kinaharibika haraka haraka.


Hapo ngozi nyembamba ya tumbo au mji wa uzazi, iliyotanuka kwa damu, ili kupokea na kulisha mimba, inachanika chanika na kutoa damu.


Kumbe mbegu ikikifikia kijiyai, mimba inapatikana na kujishikiza kwenye kuta ‘wall’ za tumbo la uzazi, ili iendelee kukua.


Ingawa, kama mimba ikishika rasmi, hapo huwa vigumu mno damu kutoka, na ujauzito hujitokeza.


Mizunguko mingi ya hedhi, huwa na siku kadhaa za mwanzo, ambapo mimba haiwezi kupatikana muda wa kutoshika, kabla ya kudondosha kijiyai.


Siku ya kwanza ya kuvuja damu, inahesabiwa kuwa siku ya kwanza ya mzunguko wa hedhi.





Mbinu mbalimbali za kufahamu uwezo wa kushika mimba, huhesabu kwa njia tofauti kidogo kipindi ambapo kuna uwezekano wa kupata mimba, yaani hutumia ishara za msingi, za uwezekano huo.

 

JE UNAYAJUA MAUDHI YA HEIDH?

Yapo aina mbali mbali, kwa kila mwanamke, ingawa lazima yatafautiane kati ya mmoja na mwengine.

 

Kwa mfano, yapo maumivu ya heidhi aina ya kwanza ambayo ni ya kawaida ‘Primary Dysmenorrhea’ haya kwa wanawake, wanapopitia kipindi hiki, ambacho hujirudia kila mwezi.

 

Ambapo kwa kawaida, huanza kati ya siku moja ama mbili, tena kabla ya hedhi kuanza kutoka, mwanamke hujiskia mamumivu haya kwenye tumbo la chini, nyonga, na kiuno.

 

Maumivu haya yanaweza kuwa madogo au makali, na huishia ndani ya saa 12 mpaka 72 huku yanaweza kuambatana na kujitokeza kizunguzungu.



 

 Yapili ni yale maumivu yasio ya kawaida ‘Secondary Dysmenorrhea’ ambapo haya, hutokana na tatizo la kiafya, kwenye via vya uzazi, kama vile uvimbe ambao sio wa saratani ndani ya mfuko wa mimba ‘uterine fibroids’.

 

Maumivu haya, yanaweza pia kusababishwa kwa athari za bakteria na virusi katika via vya uzazi, ambapo kwa kawaida, maumivu haya huanza mapema zaidi wakati wa hedhi.

 

JE HEIDH INA MUDA MAALUM?

Mtaalamu wa afya ya uzazi kutoka hospitali ya Chake chake Pemba, Rahila Salim Omar, anasema kwa kwaida, hedhi haina muda maalum.

 

Miongoni mwa wanawake kuna anayeingia hedhini, kwa muda wa siku tatu, nne, ingawa muda wake sana huwa ni kati ya siku sita au saba.

 

Aligusia kuwa, suala la lishe bora, mazoezi, kupata muda wa mapunziko, kupunguza mawazo na uchangamshi, ni vichecheo vya kupata mzungumko bora na imara wa hedhi.

 

HEDHI SALAMA KWA WANAFUNZI NI IPI?

Hedhi kwa wanafunzi, ni jambo lisilozungumzwa hadharani, katika jamii nyingi Tanzania, kutokana na imani za kidini na kitamaduni.

 

Aisha Haji Omar miaka (71) wa Machomane anasema, achia mbali kwa wanafunzi, hata kwa wanawake wengine, inaonekana kama vile ni aibu.

 

‘’Usiri huu ndio unaochangia, wanawake wengine kupata madhara kwenye via vya uzazi, kwani inaonekana kama vile ni matusi, kuzungumza hedhi salama hadhari,’’anasema.

 

Mayasa Haji Vuai (45) wa Mwambe, anasema kwa umri wake, alipata elimu mara moja tu alipohudhuria kliniki, juu ya hedhi salama.

 

Mtaalamu wa afya ya uzazi hospitali ya Chake chake Dk. Rahila Salim Omar, anasema usiri uliopo wa kuizungumzia hedhi salama, huzaa matatizo kadhaa, ikiwemo hata kuharibika kwa njia za uzazi.

 

‘’Via vya uzazi vinahitajika kuhifadhiwa kwa vitambaa ama vifungashio vilivyo salama na hata sehemu ya kuanikia, ambapo haya hayatojulikana, ikiwa kuna usiri wa elimu ya hedhi salama,’’anasema.

 

Mwanafunzi wa skuli ya Madungu Aisha Hassans, anasema hedhi salama bado ni changamoto kwake, kuanzia matumizi ya vitambaa na namna ya kujihifadhi.

 

‘’Mimi na wenzangu hadi leo ikitokezea hedhi, huwa vigumu kuhudhuria masomoni, na furaha yetu ni kubakia nyumbani,’’anaeleza.

 

Radhia Issa Maliki wa skuli ya Kiuyu, anasema usiri ulioanzia ngazi familia na skuli, unawafanya wakose furaha, kipindi cha hedhi.

 

Maua Mkubwa Haji na mwenzake Hanifa Juma Hamad wa skuli ya Mwambe wanasema, hedhi salama wanavyojua wao, ni kutokuumwa na tumbo pekee.

 

‘’Wakati mwengine hata vitambaa sisi tunaazimana, kama ikitokezea mwenztu amepata hedhi, tuko safarini, na hadi leo sijapata maumivu,’’anasema Maua.

 


Akizungumzia kuhusu hedhi salama, Balozi wa Flowless Sanitary Pads, Dk. Romana Malik anasema, kama mwanamke anaandaliwa kubeba mimba hapo baadae, jamii izingatie misingi ya hedhi salama.

 

“Hedhi salama hufanyika pale ambapo binti au mwanamke yuko katika mazingira rafiki ya kupata taulo salama, zenye ubora kwa afya yake hasa kwenye via vya uzazi.

 


Akasema jambo la kuzingatia pamoja na taula ama vitambaa maalum, lakini maji safi na salama pamoja na sabuni, viwepo kwa ajali ya kukoshea vitambaa anavyotaka kuvirudia.

 

Pamoja na Umoja wa Mataifa ‘UN’ na Jumuiya za Kimataifa ikiwemo taasisi isiyo ya kiserikali WASH United ya Ujerumani, ziliamua kuitangaaza Mei 28 ya kila mwaka, iwe siku ya hedhi salama, bado changamoto kwa wanafunzi ipo.

 

 DHANA POTOFU KWA WENYE HEDHI

Kampeni hizi zinaibua hisia tofauti, miongoni mwa jamii, wapo ambao wanachukizwa wakiamini kuwa si jambo sahihi kuzungumzia suala la hedhi salama.

 

Wapo wanawake na wasichana, hukanywa na jamii zao juu ya kutofuata mambo kadhaa kwa sababu ya kuwa na hedhi, ikiwemo kutohudhiria misiba na harusi hasa nyakati za usiku.

 

WIZARA INAFANYA NINI KWA WANAFUNZI?
 Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Mohamed Nassor Salim, anasema, wizara inachukuwa juhudi ya kupambana na hedhi salama kwa wanafunzi, kwakuwapa elimu ya stadi za maisha .

 

Anaeleza kuwa stadi za maisha hizo ni pamoja na kujitambuwa na udhalilishaji, kuwa salama na hedhi na kuimarisha miundombinu hususani yvoo.

 



Wizara pia imewawezesha waalimu wa kutosha wa ushauri nasaha wa madarasa ya msingi na sekondari, na kwamba kila skuli, lazima wawepo waalimu wa aina hiyo.


Anasema wamekuwa wakishirikiana na hata wadau wa maendeleo, ili kupata taula za kike, kama ambavyo mwaka jana, walikabidhiwa pedi 3,000  na kuzigawa kwa wanafunzi 314.


Wamekuwa wakipata wahisani mbali mbali wanaotoa elimu ya kujihifadhi kwa wanafunzi hao kama vile Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania ‘TAMWA’, UNICEF na Serikali kuu.

Taasisi kama ni KFHI kupitia ‘mradi wa kuwajengea uwezo waalimu katika mazingira rafiki ya moto wa kike’ unaofadhiliwa na Korea ambao kwa Zanzibar umeshatoa mafunzo kwa skuli tano, ikiwemo ya sekondari Shumba Vyamboni na Chwaka Tumbe.

Ambapo Mkurugenzi wa mradi  huo Esther Mwakarobo, anaeleza Lengo la mradi huo, ni kutaka kutengeneza mazingira rafiki kwa wanafunzi hasa wa kike, kwenye hedhi salama.

 

Anaona usafi usipozingatiwa katika kipindi cha hedhi kunaweza kusababisha maambukizi, katika mfumo wa uzazi na kwenye njia ya mkojo.

Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Sekondari Shumba Vyamboni Khatib Rashid Mwinyi, anasema anona utoro wa wanafunzi na kuumwa, hasa kipindi cha hedhi, ikisababishwa na kutokuwa na elimu ya hedhi salama.

 

TAMWA INAFANYA NINI?

Afisa Mradi wa afya ya uzazi Zaina Abdalla Mzee, anasema wameibua mradi wa mwaka mmoja, kwa ajili ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari.

 

Kwani utafiti waliofanya kabla ya kutekeleza mradi huo wa majaribio, waligundua kuwa uelimishaji juu ya afya uzazi, kupitia vyombo vya habari uko chini.

 

‘’Tumeshakutana na waandishi wa habari wa Unguja na Pemba, kuwajengea uwezo kupitia wataalamu wa afya ya uzazi, sasa tunategemea mno kuona inaeleweka maana ya afya uzazi,’’anasema.

 

Kwake anaona mafanikio makubwa iwe, kwanza wanawake na wasichana wa mjini na vijijini wanauwelewa haki ya afya ya uzazi.

 

Jingine ni kwa vyombo vya habari, kukuza na kuenedeleza uwelewa kwa jamii, ili sasa suala la afya ya uzazi lisionekane kama vile ni kwa kundi maalum.

 

 MIKATABA YA KIMATAIFA

Mwaka 2001, nchi za Afrika zilikutana Abuja na kutangaaza ili ziweke angalau asilimia 15 ya bajeti zao, kuimarisha sekta ya afya, ikiwemo afya ya uzazi.

 

Imebainika kuwa, sasa nchi za Afrika zinatumia dola 8 hadi 129 kwa kila mtu kwa afya, ikilinganishwa na nchi zenye kipato cha juu, zinzotumia zaidi ya dola 4,000.

 

Mkataba wa kutokomeza aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake ‘CEDAW’ wa mwaka 1979, unazitaka nchi wanachama, kuchukua hatua kuhakikisha zinaheshimu utu wa bindamu na kuondoa ubaguzi.

 

Lengo la tatu kati ya 17 ya Maendeleo Endelevu ‘SDGs’, inazitaka nchi wanachama kuhakikisha maisha bora yenye afya na kukuza ustawi kwa watu wote.
                        MWISHO

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch