Skip to main content

Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa Ataka Wadau Kuongeza Weledi Katika Kutokomeza Ukatili

 


Na Muandishi Wetu Zanzibar

Mwenyekiti wa Kamati yaMapngo wa  Kitaifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto, ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman, amewataka wadau wanaojihusisha na masuala ya ukatili na udhalilishaji kufanya kazi kwa weledi na ushirikiano ili kutokomeza vitendo hivyo katika jamii.

Mhe. Haroun alitoa wito huo jana wakati wa uzinduzi wa Kamati ya Kitaifa ya ngazi ya Mawaziri uliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Airport, Zanzibar.

Alisema kuwa lengo la kuundwa kwa kamati hiyo ni kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi mbalimbali katika kupambana na vitendo vya ukatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto, kwa lengo la kupunguza na hatimaye kuvimaliza kabisa.

Aidha, aliitaka kamati hiyo kutekeleza majukumu yake kwa bidii, kuweka mikakati madhubuti na kuhakikisha sheria pamoja na sera zilizopo zinatekelezwa ipasavyo ili kulinda haki za wanawake na watoto.



Kwa upande wake, Mwenyekiti Mwenza wa Kamati hiyo ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Anna Athanas Paul, alisema Wizara yake itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo katika kuimarisha mifumo ya ulinzi wa jamii.

Alisema Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto itaendelea kutoa elimu kuhusu haki za wanawake, watoto na wananchi kwa ujumla ili kujenga jamii yenye kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji.



Naye Afisa Programu za Jinsia kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA), Ali Haji Hamadi, alisema shirika hilo litaendelea kushirikiana na Serikali katika kusaidia utekelezaji wa programu zinazolenga kulinda haki, afya na ustawi wa wanawake, watoto na vijana.

Katika uzinduzi huo, Mkuu wa Divisheni ya Watoto, Mohammed, aliwasilisha muhtasari wa Mpango wa Kitaifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto wa miaka mitano (2025–2030), akieleza mpangilio wa utekelezaji wake, ushirikiano wa sekta mbalimbali na wadau wa maendeleo, pamoja na mfumo wa uratibu, ufuatiliaji na tathmini ya mpango huo.

Kwa upande wa Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii, ndugu Omar Haji, aliwasilisha muundo na majukumu ya Kamati hiyo. Alieleza kuwa Kamati itaongozwa na Waziri anayeshughulikia masuala ya sheria, ndie mwenyekiti huku Waziri anayesimamia masuala ya jinsia akiwa Mwenyekiti Mwenza, kamati hiyo inawajumuisha Wizara,na taasisi za Kiserikali na binafsi na washirika wa maendeleo.




Alisema miongoni mwa majukumu makuu ya Kamati hiyo ni kutoa mwongozo wa kisera, kuhakikisha afua zinaendana na mikakati ya kitaifa, kushawishi ugawaji wa bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa mpango kazi, kusimamia usimamizi wa kesi za ukatili na kuhakikisha mashitaka yanawasilishwa na kuendeshwa kwa wakati.

Uzinduzi wa Kamati ya Kitaifa ya Kutokomeza Ukatili na Udhalilishaji dhidi ya Wanawake na Watoto ulihudhuriwa na viongozi na wadau mbalimbali, wakiwemo mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya, Jeshi la Polisi, Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), pamoja na washirika wa maendeleo wakiwemo UNICEF, UNFPA na UN Women.

Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...