Skip to main content

TAMWA YAWAPA MAFUNZO YA UWAJIBIKAJIN MADIWANI NA WARATIBU WANAWAKE




NA MOZA SHAABAN, PEMBA

MADIWANI wakuchaguliwa na waratibu wanawake na watoto kutoka wilaya nne za Pemba  wametakiwa kuwajibika ipasavyo katika utekelezaji majukumu yao ya msingi ya kiuongozi, ili kujenga imani kwa jamii juu ya uwezo alionao mwanamke katika kuongoza na kuleta maendeleo.

Wito huo umetolewa na Afisa Progamu wa mradi wa kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika masuala ya uongozi (SWIL) unaotekelezwa na TAMWA-Zanzibar Sabrina Ali Mwatanga wakati wa mafunzo  kwa madiwani na waratibu wanawake na watoto kutoka wilaya nne za Pemba, yaliolenga kuwajengea uwezo juu ya namna ya kuwajibika ipasavyo katika uongozi wao, yaliofanyika katika ukumbi wa mikutano TAMWA Mkanjuni Chake chake Pemba.

Alieleza mafunzo hayo ni mwendelezo wa hamasa na kuwajengea uwezo madiwani na waratibu hao juu namna bora ya kutekeleza majukumu yao ya kiongozi, ili jamii ione ufanyaji kazi wao kivitendo.

Afisa huyo alisema  TAMWA imekua ikifanya juhudi kubwa katika kuwajengea uwezo wanawake mbali mbali katika kushiriki kwenye vyombo vya maamuzi kupitia uongozi na demokrasia, ila bado jamii haina imani kubwa na viongozi hao hivyo kuwajibika kwao kutaionyesha jamii nguvu walionayo wanawake katika kuleta maendeleo.

"TAMWA imekua ikifanya juhudi kubwa katika kuwajengea uwezo wanawake katika kushiriki kwenye vyombo vya maamuzi kupitia uongozi na demokrasia, ila bado jamii haina imani kubwa na viongozi wanawake, basi kuwajibika kwenu kutaionyesha jamii nguvu ya wanawake katika kuleta maendeleo", alisema.

Aliongeza kua uwajibikaji mzuri ni msingi wa uaminifu kwa wanawake katika kugombea nafasi mbali mbali za uongozi, ambapo kitakua kipimo muhimu kwa jamii katika kufanya maamuzi ifikapo uchaguzi mkuu 2030, hivyo TAMWA-ZANZIBAR ikaamua kuwapatia mafunzo hayo ili kuwandaa kwa uchaguzi mkuu ujao.




" Jamii pia huangalia uwajibikaji wa mtu anapopata nafasi, ambapo huchukua hilo kama ni kigezo cha kufanya maamuzi katika uchaguzi, ndio TAMWA tukaamua kuwapa mafunzo haya mukayatumie kama ni maandalizi ya uchaguzi wa 2030", alisema.

Nae Kaimu Mratibu wa TAMWA Ofisi ya Pemba Amina Ahmed Mohammed alisema, mafunzo hayo yanalenga kutoa hamasa kwa madiwani na waratibu wanawake na watoto ili kuongeza ushiriki wao katika ngazi za maamuzi, ili sauti za wanawake ziweze kusikika na kua tumaini kwa wanawake na watoto, ambapo zinaweza kusaidia kuleta mabadiliko ya upatikanaji wa haki mbali mbali kwa jamii.

Alisema wanawake wanamchango mkubwa katika maendeleo, siasa utawala na utamaduni iwapo watawajibika ipasavyo katika kuzitumikia jamii zao kwa kuzipatia maendeleo.

Akiwasilisha mada kuhusu ushiriki wa wanawake  katika kugombea nafasi mbali mbali za uongozi mkufunzi wa mafunzo hayo Fat-hia Mussa Said, aliwataka wanawake kua na uthubutu katika kugombea nafasi hizo.

Alisema katika miongo ya hivi karibuni dunia imepiga hatua kubwa kuongeza ushiriki wa wanawake katika uongozi na siasa, ambapo nchi nyingi zimeanzisha sera, sheria na mikakati ya kuhakikisha wanawake wanapata fursa sawa na  wanawake kushiriki katika nafasi za uongozi.

Alisisitiza pamoja na mafanikio hayo wanawake bado wapo chini ya uwakilishi wa wanaume katika mabunge, serikali za mitaa vyama vya siasa na taasisi mbali mbali za maamuzi ikilinganishwa na wanaume, hivyo alisisitiza wanawake kuchukua juhudi za makusudi kuongeza ushiriki wao.



Nao washiriki wa mafunzo hayo waliipongeza TAMWA-Zanzibar kwa  kuwapatia mafunzo hayo na kuona umuhimu wa kuwaongezea maarifa ya uwajibikaji wanawake viongozi    jambo litakalo saidia kutimiza majukumu yao ipasavyo pamoja na kwashajihisha wanawake wengine katika kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali za uongozi katika uchaguzi wa 2030.

Hata hivyo walieleza bado wanawake viongozi wanakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo mfumo dume, kutojiamini na kutokukubalika kwa jamii, hivyo wameomba wadau mbali mbali kuendeleza mapambano dhidi ya changamoto hizo, ili kuinua ushiriki wao katika kugombea nafasi za uongozi.

TAMWA- ZNZ  kupitia mradi wa SWIL  imekua ikishajihisha wanawake kushiriki katika kugombea nafasi mbali mbali za uongozi, ili kupata uwakilishi wao katika ngazi za maamuzi kwa lengo la kupaza sauti zao juu ya uvunjaji wa haki zao za msingi na kukuza usawa wa kijinsia,  ambapo huonekana kuvunjwa mara kwa mara.                                                                    

                                                                     MWISHO.

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...