NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
SERIKALI ya Canada, imesema itaendelea kushirikiana na serikali za
Tanzania, katika maeneo mbalimbali, ikiwemo kwenye uchumi wa buluu, ili
walengwa wakuze pato lao na taifa.
Hayo yameleezwa leo Juni 23, 2026
na Balozi wa taifa hilo, nchini Tanzania Emily Burns, kwenye hafla ya ugawaji
wa vitendea kazi kwa vikundi vya wajasiriamali, waliokeza kwenye bahari, na
ufunguzi wa kituo cha mafunzo eneo la Chamanangwe wilaya ya Wete Pemba.
Alisema,
ushirikiano huo, anaamini utawasaidia wajasriamali waliokeza kwenye eneo hilo,
hasa wanawake na vijana, ambao kwa muda mrefu walikuwa hawakuhusishwa moja kwa
moja.
Alieleza kuwa,
kwa eneo la Zanzibar na baadhi ya mikoa ya Tanzania bara, ilivyozungurukwa na
bahari, wakati umefika manufaa yake, yawanufaishe makundi yote.
‘’Serikali
ya Canada, inaziahidi serikali zote mbili kwamba, ushirikiano huu kwenye sekta ya
uchumi wa buluu, utakuwa endelevu pamoja na maeneo mingine,’’alifafanua.
Katika hatua
nyingine, Balozi huyo wa Canada nchini Tanzania, aliwataka wajasiriamali hao,
kuhakikisha vifaa hivyo ikiwemo boti maalum, wanavitumia, kwa lengo la kukuza
pato lao.
Alisisitiza
kuwa, serikali ya Canada imetumia gharama kubwa, ili kununa vifaa hivyo, kama
sehemu ya kuziunga mkono seriali za Tanzania, hivyo lazima waelekeze nguvu zao
huko.
‘’Vifaa
hivi tulivyovikabidhi kwenu, ni heshima kubwa kwa viongozi wa Tanzania, ambao
wamekuja na sera ya uchumi wa buluu, sasa mwelekeo uwenu uwe wa maana sana,’’alisisitiza.
Hata hivyo,
alipongeza hatua za marais wa Tanzania, kwa kuzingatia kwa vitendo sera ya uchumi
wa buluu, kwa wananchi wake.
Mapema Mkurugenzi wa Mradi wa Resea Andreanne Martel- Mi, alisema ni jambo la faraja, kuona serikali ya Canada imetekeleza kwa vitendo ahadi yake.
Alisema,
amefarajika sana kuona kuwa, wameingia kwenye siku nyingine, yenye mwalekeo wa
kuwasaidia vifaa vya kutendea kazi, wajasiriamali hao wingi, wakiwa wanawake.
‘’Kama inavyoeleweka
kuwa, wanawake ndio kundi ambalo liliachwa nyuma kwenye sekta kadhaa, ikiwemo
ya bahari, lakini kwa hili lililofanywa na wenzetu wa Canada, matunda yanakuja
kwa haraka,’’alifafanua.
Aliongeza kuwa,
mradi huo ambao unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya IUCN, WFTT na Ocean hub, ni
kuona taasisi hizo zinatia nguvu, ili mradi utekelezeke.
Alieleza kuwa,
mfano wa utoaji wa vifaa hivyo, wala sio shughuli ndogo, bali pia ni kutambua
uwepo wa kundi hilo na umuhimu wake, katika kukuza pato lao na taifa.
‘’Kushirikiana
kwetu na taasisi hizo, sio tu kwamba tuwe pamoja, bali ni kuleta mageuzi ya
kiuchumi na kuimarisha mnyororo kwa wanawake na vijana, kwenye eneo la uchumi
wa buluu,’’alifafanua.
Katika hatua
nyingine, alisema vikundi hivyo kwa sasa vimekuwa kiuchumi, na kama vile
kukabidhiwa kwa vifaa hivyo, vinakwenda kujitegemea.
Mkuu wa wilaya ya Wete Abdalla Rashid Ali kwa
niaba ya Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, amewataka wajasiriamali waliokabidhiwa
vifaa hivyo, kwanza kuvithamini na kisha kuhakikisha vinazaa matunda.
Alieleza kuwa,
fedha nyingi zimetumika kununulia vifaa, hivyo sasa ni wajibu wao, kuona
vitawasaidia wao na wingine hapo baadae.
‘’Kwa
hakika wenzetu wa jumuiya ya Inclusion wamefanya jambo jema, kuwapata wafadhili
wa serikali ya Canada na sasa kuwagawia vifaa hivi,’’alifafanua.
Kwa upande
wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Ruzuku wa Wanawake Tanzania ‘WFTT’ Rose Marandu,
aliiongeza serikali ya Canada, kwa kukubali ununuzi wa vifaa hivyo.
Alieleza kuwa,
serikali ya Canada, imekuwa mdau mkuu wa maendeleo katika sekta mbalimbali,
ikiwemo ya uchumi wa buluu.
Nae Ofisa
Mdhamini wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Pemba Dk. Salim Hamza, alisema kwa
miaka 10 iliyopita, Zanzibar hakukua na sera na uchumi wa buluu, jambo
lililowatenganisha wanawake.
Alisema,
sasa serikali imeshatekeleza kwa vitendo hilo na ndio maana, rasimali za bahari
zinawanufaisha wanawake na wanaume.
‘’Niwapongeze
sana Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania na yule wa Zanzibar, kwa kuzitafsiri
kwa vitendo ahadi zao, kwa walioekeza kwenye sekta ya baharini,’’alisema.
Wakisoma risala
yao, iliyosomwa na Saada Juma Haji kutoka kikundi cha Tusijisahau cha Madenjani,
alisema, sasa wanakwenda kuuwaga umaskini.
Alieleza kuwa,
hilo linakuja baada ya vifaa ambavyo waliviomba, vimekujana kama walivyotaka,
na kupata ari na mori ya kuendelea na kazi zao.
Alisema,
wamekuwa wakijishughulisha na ukulima wa majongoo bahari, mwani, usarifu wa
dagaa na uhifadhi wa mazingira ya bahari.
Vifaa
vilivyokabidhiwa kwa vikundi hivyo 12 ni boti maalum na mashine zake, viatu,
meza za ofisi, mabero, viatu maalum, lapo top, mezani.
Vyingine
ni makoti maalum ya kuokolea maisha, waya za kuanikia dagaa na mwani, vioo vya
kuzamia, majembe pamoja na uzinduzi wa kituo cha mafunzo cha wajasiriamali, kwa
mujibu wa kazi zao hizo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 270.
Vikundi
vilivyokabidhiwa vifaa hivyo ni pamoja na Jiongezee, Jitihada, Mtu ni yupi, Tusijisahau,
Mwendaji si mkaaji, Tushikamane, Hapa kazi tu kwa upande wa Pemba na Mafanikio
group, Tageti group, Magarawani na Marikacha kwa upande wa mkoa wa Tanga.
Mradi wa
Resea ambao ulikuwani wa miaka mitatu, kutoka mwaka 2023 hadi 2025, ingawa
umeongewa muda hadi mwishoni mwa mwaka huu, unafadhiliwa na serikali ya Canada.
Mradi huo
unatekelezwa na mashirika matatu, likiwemo la Mission inclusion, IUCN na WFTT,
unafanyika mataifa ya Kenya, Moazambique, Madascar, Comoros na Tanzania, ambapo
mradi huo unao maeneo kadhaa, ikiwemo la uchumi wa buluu.
Mwisho
Comments
Post a Comment