WAANDISHI
wa habari wa mataifa ya Afrika, wameiomba serikali ya China, kuyapa mataifa yao
miradi endelevu mikubwa ya maendeleo, ili baadae yaweze kujiendesha, badala ya
kutegemea misaada kila baada ya muda.
Wakizungumza
kwenye ziara ya kuvitembelea vituo vya Tehema, star times vilivyopo Beijing
nchini China, walisema urafiki na uhusiano wa China na mataifa ya Afrika,
unaweza kuchapuzwa na miradi mikubwa.
Mwandishi wa
habari kutoka Gambia Arret Jatta, alisema kwa muda mrefu mataifa hayo, yamekuwa
yakipokea misaada kutoka kwa serikali ya China, ingawa baada ya miradi
kumazilika, hurejea kwenye utegemezi.
Alieleza
kuwa, China imekuwa ikitumia mamiliobi ya dola, kuyaunga mkono mataifa ya
Afrika, ingawa huwa ni kwa kiasai kidogo, kwa mujibu wa mahitaji ya wakati
uliopo.
‘’Wakati
umefika sasa kwa taifa la China, kulielekea taifa moja moja la Afrika, na
kulipa msaada mkubwa wa maendeleo, katika nyanja ama ya elimu, afya,
miundombinu ili changamoto hiyo imalizike,’’alipendekeza.
Nae
mwandishi Agren Mutambo kutoka Kenya, alisema ipo miradi mikubwa kama ya ujenzi
wa miundombini, afya, maji safi na salama, kama China ikiyafanya kwa ukubwa
wake katika mataifa yanayoendelea, inaweza kusaidia.
‘’Ijapokuwa
China imekuwa ikitoa misaada mikubwa kwa mataifa ya Afrika, lakini napendekeza
iongeze nguvu, maana bado baadhi ya mataifa shida ipo,’’alisema.
Kwa upande
wake mwandishi Yakali Tariku kutoka Ethiopia, alisema changamoto kubwa ndani ya
baadhi ya mataifa ya Afrika, ni kukosekana miradi mikubwa na endelevu, hivyo ni
wakati umefika kwa China, kuongeza juhudi.
‘’Tunajua Rais wa sasa wa China Xi Jinping , amekuwa na uhusiano na urafiki kwa dhati kwa
mataifa ya Afrika, likiwemo la Ethiopia, lakini sio vibaya kuongeza nguvu
katika eneo la miradi mikubwa,’’alifafanua.
Waandishi wa
habari Josphine Mabere wa Kenya na mwenzake Zuhura Juma wa Zanzibar,
waliipongeza serikali ya China kwa misaada yao ya kibinaadamu, wakati wa janga
la Covid19.
Mtaalamu wa
sayansi ya jamii kutoka taasisi ya Magharibi mwa bara la Asia na Afrika,
anayefania kazi zake nchini China Professa: He Wenping, alisema China imekuwa
ikihakikisha kila muda, kupeleka misaada mikubwa kwa Afrika.
Akiwasilisha
mada ya sera na utendaji kazi kwa China, juu ya maendeleo ya Afrika Dk. Yao
Shuai, alisema misaada yenye thamani ya dola bilion 615.8 imeshapeleka mataifa
ya Afrika, kati ya mwaka 1950 na mwaka 2018.
Aidha
alisema, wapo madaktari zaidi ya 1,069 wamesambaazwa katika mataifa, na maeneo
76, barani Afrika wakitoa huduma za matibabu ya kibinaadamu.
‘’Na kuanzia mwaka 2000 hadi mwaka 2020, China imeshajenga vituo vya michezo 45 na skuli 170 katika maeneo mbali mbali ya mataifa ya Afrika, ikiwa ni sehemu ya kuongeza uhusiano wake,’’alifafanua Dk. Yao.
Awali
akifungua mafunzo ya siku 20 kwa waandishi wa habari wa mataifa ya Afrika,
yanayozungumza lugha ya kiengereza, Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la
Mawasiliano (CICG) Han Likiang, alisema mafunzo hayo, ni sehemu ya kuziwezesha
nchi ukuaji uchumi wao.
Waandishi wa
habari wa redio, tv, mitandao ya kijamii na magazeti wapo nchini China,
wakiendelea na mafunzo na ziara, ni kutoka nchi za Gambia, Zambia, Kenya,
Ethiopia, Tanzania Zanzibar na wenyeji China.
Mwisho
Comments
Post a Comment