Skip to main content

WAKULIMA MRADI WA VIUNGO WAKABIDHIWA VIFAA

 


NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR@@@@

 WAKULIMA wanaojishughulisha na kilimo cha  mboga mboga, matunda na viungo kupitia  MRADI wa  VIUNGO (AGRI-CONNECT)  wamekabidhiwa vifaa vitakavyowasaidia kuongeza nguvu katika uzalishaji wa bidhaa bora zitakazokidhi masoko.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vifaa hivyo iliofanyika katika jengo la Kificho Mwanakwerekwe Meneja Mkuu wa mradi huo Simon Makobe alisema  vifaa hivyo vitatumika kusaidia kuongeza uzalishaji na kufikia malengo ya utekelezaji wa mradi huo.

Alisema MRADI wa VIUNGO ulilenga mambo mbalimbali ikiwemo kufungua fursa na kuongeza mnyororo wa thamani ya mazao hapa Zanzibar pamoja na kupatiwa vifaa kwa lengo la kuwawezesha wakulima kuwa na nyenzo muhimu ili kulima kilimo bora kitakachowasaidia kujikwamua kiuchumi,”alisema.

 “Ugawaji wa vifaa hivyo ni moja ya mikakati ya utekelezaji wa mradi huo pamoja na kutumia ujuzi mulioupata juu ya matumizi ya teknolojia muliyojifunza kipindi chote cha utekelezaji wake,” alisema Makobe.

Alifahamisha kuwa lengo la mradi huo ni kuleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi kwa wakulima na taifa hivyo kupitia hatua hiyo itasaidia kufikia malengo hayo.

Sambamba na hayo aliwataka wakulima walionufaika na vifaa hivyo kufuata maelekezo ya matumizi ya vifaa hivyo ili viweze kuleta tija kwenye shughuli zao za kilimo.

Kwa upande wake Meneja tathmini na ufatiliaji wa mradi huo Ali Abdalla Mbarouk alisema kukabidhiwa kwa vifaa hivyo itasaidia kuimarisha ustawi wa shughuli zao kwa kuondosha changamoto zilizokuwa zikijitokeza baina ya viongozi wa mradi huo na wakulima.

“Tulitegemea vifaa hivi vitolewe  kipindi cha utekelezaji wa mradi kwa bahati mbaya sasa mradi umemaliza ila tulikabiliwa na changamoto ya fedha kidogo,”Mbarouk alisema.

Mratibu wa mradi huo kutoka Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar Mashavu Said Sukwa alisema mradi huo pamoja na changamoto za hapa na pale zilizojitokeza katika utekelezaji wake lakini umeweza kuleta tija kwa wakulima kwa kupata elimu ya kuongeza uzalishaji na kuzalisha bidhaa bora.

Alisema endapo wakulima hao wakishindwa kuvitumia vifaa hivyo ni vyema kuvirudisha serikali na sio kufanya wanavotaka wao kwani kufanya hivyo ni kwenda kinyume na malengo ya matumizi ya vifaa hivyo na kutawasababisha kuingia katika matatizo.

“ Wakulima tunawaomba  kuvitunza vifaa hivyo na kuvitumia kwa mujibu wa matumizi yaliopangwa na si vinginevyo, mukenda kinyume na hayo kwa mujibu wa Sheria mutafanya kosa na kuingia hatiani,” Mashavu alisema.

 Kwa upande wa Ofisa elimu kutoka Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi Zanzibar (ZAECA) Saumu Ramadhan Haji alisema watafatilia kwa karibu matumizi ya vifaa bivyo ili kuondosha ubabaifu unaofanywa na baadhi ya wakulima kwa kuvitumia kinyume na malengo ya vifaa wanavokabidhiwa.

Sheria ya ZAECA No 5, (2023), kifungu No 53 kinaeleza juu ya matumizi mabaya ya Umma, pindipo utatumia vibaya mali ya Umma utaingia hatiani na adhabu yake ni shilingi milioni 10 za Kitanzania, au utafungwa jela kifungo cha miaka 5 au vyote kwapamoja.

Kwa upande wa wakulima hao walishukuru kupatiwa vifaa hivyo na kuahidi kuvitumia kama walivyoelekezwa ili kwenda sambamba na malengo husika ya mradi.

 Walisema vifaa hivyo vitasaidia kuongeza kasi ya uzalishaji wa kilimo chao kutokana na kikwazo kikubwa kilikuwa ni kukosa nyenzo za kisasa za kuendeleza kwa shughuli zao hivyo kupitia hatua hiyo wataweza kufikia malengo yao.

Jumla ya wakulima 31 walikabidhiwa vifaa mbalimbali  vya kilimo na watatu (3) fedha taslimu ikiwemo matenki ya maji, mashine za kuvutia maji, mipira ya kusambazia maji na vifaa vingine kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao za kilimo.

Mradi wa VIUNGO ulioanza mwaka 2020-2024 ni mradi wa miaka minne (4) uliomaliza mda wake, uliwafikia wakulima wapatao elfu hamsini na saba, mia tisa na sabiini na nne hapa Zanzibar kwa Wilaya tisa (9), tano (5) Unguja na nne (4) Pemba ambao  ulitekelezwa kwa pamoja na TAMWA,  People Developmend Forum (PDF) na Community Forest in Pemba (CFP)  kwa kushirikiana na Jumuiya ya Umoja wa Ulaya.

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan