Skip to main content

SHEIKH SAID, AWAONESHA NJIA WAZAZI CHUMBAGENI KUWA NA KIZAZI CHEMA

  


NA SALIM HAMAD, PEMBA@@@@

WAZAZI na walezi katika shehia ya Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, wamehimizwa kuwasomomesha watoto wao kitabu kitukufu cha Qu-ran, ili kupatikana kwa kizazi chenye misingi ya maadili mema leo na baadae.

Shekh Said Abdalla Nasor, ametoa kauli hiyo leo Septemba 8, 2024, wakati akizungumza na wazazi, walimu na wanafunzi wa Amladrasatul Imanniya ya Chumbageni Wambaa wilayani humo, katika mahafali ya kuwatunuku vyeti wanafunzi waliomaliza juzuu 30, na tathmini ya mwaka uliopita kwa madrssa hiyo.



Alisema ili kupatikana kwa viongozi bora wa nchi, maimamu, masheikhe na hata watumishi wa umma wa baadae, hakuna budi kwa wazazi katika kuwabidiisha watoto wao, kukisoma kitabu hicho.

Alieleza kuwa, taifa linahitajia madaktari, wakuu wa wilaya, waalimu wa madrassa na masheikhe wenye misingi ya dhati ya dini ya kiislamu, ambapo hilo litafanikiwa, ikiwa watakisoma kwa dhati kitabu hicho.

‘’Nichukuwe nafasi hii, kuwataka wazazi na walezi wetu, kuhakikisha tunawabidiisha watoto wetu na kitabu kitakatifi cha qur-an, ili kupata raia wenye Imani na misingi ya dini yao,’’alieleza.


Katika hatua nyingine, sheikh Said Abdalla Nassor, ameutaka uongozi wa madrssa hiyo, kuandaa mpango maalum, kwa ajili ya mashindani ya qur-an, katika mwezi mtukufu wa ramadhani mwaka huu.

Mapema Mkurugenzi Uratibu wa Shirika la Magazeti ya serikali Zanzibar ofisi ya Pemba, Haji Naasor Mohamed, amewataka wazazi na walezi, kuwalipia ada za watoto wao kwa wakati, ikiwa ni sehemu ya kuungamkono juhudi za maendeleo ya elimu.




‘’Wapo wazazi na walezi wamekuwa walipaji wazuri wa ada kwa watoto wao kwa masomo ya skuli, lakini kwenye madrassa shilingi 200 kwa wiki hailipwi kwa wakati,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo Uratibu wa Shirika la Magazeti ya serikali ofisi ya Pemba, ameahidi kusaidia gharama zote za ujenzi wa shimo la choo katika madrassa hiyo.

Alisema, kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi katika madrssa hiyo, amelazimika kuungano juhudi za ujenzi wa huo wa choo, ili kuwakinga wanafunzi na magonjwa ya mripuko.



 ‘’Hali inatisha kwa idadi ya matundu ya vyoo ilivyo na idadi ya wanafunzi zaidi 200, nami nimeguswa na hili na naahidi kuchangia gharama za ujenzi wa shimo la choo,’’alieleza.

Hata hivyo, amewakumbusha wazazi na walezi, kuongeza bidii katika kufuatilia nyenendo za watoto wao, ili kuwasaidia waalimu katika kufanikisha ndoto za watoto.


Akisoma risala katika mahafali hayo, mwalimu Saleh Abdalla Mohamed, amesema pamoja na mafanikio yanayopatikana katika madrassa hiyo, bado kuna changamoto kadhaa zinazorejesha nyuma, ikiwemo uhaba wa vifaa vya kusomeshea kama vile vitabu.








Alieleza kuwa, jambo jingine ni uhaba wa makaazi, ulipaji mdogo wa ada kwa wazazi na utoro wa wazazi kwenye vikao vya kutathamini maendeleo.

Katika mahafali hayo, yaliambana na mambo mbali mbali ikiwemo mashindano ya kuhifadhi qur-an, sira, fikih na qur-an tafsiri, ambapo wanafunzi17 wakiwa wote wanawake waliomaza juzuu 30 walikabidhiwa vyeti.

                                  Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan