Wizara ya Maendeleo ya
Jamii Jinsia Wazee na Watoto imeahidi kuendelea kushirikiana na Wakala wa
Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (ZEEA) katika kuwapatia wananchi fursa
zitakazoweza kuwasaidia kujikwamua kimaisha na kuwajengea uwezo ikiwa ni ya
chachu ya maendeleo yaliokusudiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).
Kauli hiyo imetolewa mwishoni
mwa wiki iliyopita na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Mhe. Riziki Pembe Juma wakati akiwa katika ziara ya Chuo cha Wajasirimali
Wanawake (Bare foot Collage) kiliopo Kinyasini Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Amesema lengo la ziara
yake ni kujifunza pamoja na kuona jitihada zinazofanywa na wanawake katika
jamii, hivyo Wizara itaendelea kushirikiana na Wakala wa Uwezeshaji Wananchi
Kiuchumi (ZEEA) katika kuwapatia wanawake fursa na kuondokana na ugumu wa
maisha.
Amefahamisha kwamba kila
mwanamke ni kiongozi katika familia hivyo Serikali itaendelea kuwaunga mkono wanawake na
kuwashauri wajasirimali Wanawake kutovujinka moyo na kuzikabili changamoto
wanazokutana nazo katika shughuli zao za ujasiriamali kwani hakuna mafanikio
yasiokuwa na changamoto.
Aidha Mhe.Riziki
amewaomba wanaume waliyokatika ndoa kuwaruhusu wake zako kwenda kujifunza
shughuli za Ujasiriamali kwani kumekuwa na malalamiko kwa baadhi ya Wanawake hawapewi
ruhusa na Waume zao hali hiyo inarudisha nyuma maendeleo katika jamii pamoja na
kusababisha ugumu wa Maisha kwa wanawake.
Naye Mkurugenzi wa Kituo
cha Wajasirimali Wanawake (Bare foot Collage) bi Brenda Godfrey Ndossi
amesema taasisi hiyo itaendelea kutoa
elimu kwa wanawake ambao hawana ujuzi wowote ili wapate ujuzi kwa kujikimu
kimaisha pamoja na kuzisaidia familia
zao.
Kwa upande wake
mwezeshaji katika kituo hicho Bi Miza Juma Othman ameishukuru Serikali kwa
kuwaekea mazingira mazuri ya kuwakomboa wanawake kimaisha. Pia ameiomba
Serikali kuendelea kuwaunga mkono wanawake katika shughuli walizozianzisha za kujikomboa
na ugumu wa Maisha.
Akizungumza moja katik Wanafunzi
waliopatiwa ujuzi, bi Fatma Haji Machano kutoka
Shehiya ya Zingwezingwe ameshukuru kupatiwa elimu hiyo pamoja na kutoa
wito kwa wanawake wengine ambao hawana kazi wala ujuzi kujiunga na kituo hicho
ili kuondokana na umasikini.
Kituo cha Wajasirimali
Wanawake (Bare foot) kina wanafunzi 21 ikiwemo wazanzibar 12 na wasomali 9
wanaojifunza utengenezaji wa taa za kutumia umeme wa jua. Piachuo hicho kinatoa ujuzi wa fani tofauti ikiwemo ufugaji
nyuki, ushoni na elimu ya kilimo na tayari kimeshatowa jumla ya wanafunzi 1054
katika fani tofauti.
Mwisho
Comments
Post a Comment