Skip to main content

'WANAWAKE KUSAIDIA KIUCHUMI' : WAZIRI PEMBE

 


          

Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto imeahidi kuendelea kushirikiana na Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (ZEEA) katika kuwapatia wananchi fursa zitakazoweza kuwasaidia kujikwamua kimaisha na kuwajengea uwezo ikiwa ni ya chachu ya maendeleo yaliokusudiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).

Kauli hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma wakati akiwa katika ziara ya Chuo cha Wajasirimali Wanawake (Bare foot Collage) kiliopo Kinyasini Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Amesema lengo la ziara yake ni kujifunza pamoja na kuona jitihada zinazofanywa na wanawake katika jamii, hivyo Wizara itaendelea kushirikiana na Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (ZEEA) katika kuwapatia wanawake fursa na kuondokana na ugumu wa maisha.

Amefahamisha kwamba kila mwanamke ni kiongozi katika familia hivyo Serikali  itaendelea kuwaunga mkono wanawake na kuwashauri wajasirimali Wanawake kutovujinka moyo na kuzikabili changamoto wanazokutana nazo katika shughuli zao za ujasiriamali kwani hakuna mafanikio yasiokuwa na changamoto.

Aidha Mhe.Riziki amewaomba wanaume waliyokatika ndoa kuwaruhusu wake zako kwenda kujifunza shughuli za Ujasiriamali kwani kumekuwa na malalamiko kwa baadhi ya Wanawake hawapewi ruhusa na Waume zao hali hiyo inarudisha  nyuma maendeleo katika jamii pamoja na kusababisha ugumu wa Maisha kwa wanawake.

Naye Mkurugenzi wa Kituo cha Wajasirimali Wanawake (Bare foot Collage) bi Brenda Godfrey Ndossi amesema  taasisi hiyo itaendelea kutoa elimu kwa wanawake ambao hawana ujuzi wowote ili wapate ujuzi kwa kujikimu kimaisha  pamoja na kuzisaidia familia zao.

Kwa upande wake mwezeshaji katika kituo hicho Bi Miza Juma Othman ameishukuru Serikali kwa kuwaekea mazingira mazuri ya kuwakomboa wanawake kimaisha. Pia ameiomba Serikali kuendelea kuwaunga mkono wanawake  katika shughuli walizozianzisha za kujikomboa na ugumu wa Maisha.

Akizungumza moja katik Wanafunzi waliopatiwa ujuzi, bi Fatma Haji Machano kutoka  Shehiya ya Zingwezingwe ameshukuru kupatiwa elimu hiyo pamoja na kutoa wito kwa wanawake wengine ambao hawana kazi wala ujuzi kujiunga na kituo hicho ili kuondokana na umasikini.

Kituo cha Wajasirimali Wanawake (Bare foot) kina wanafunzi 21 ikiwemo wazanzibar 12 na wasomali 9 wanaojifunza utengenezaji wa taa za kutumia umeme wa jua.  Piachuo hicho  kinatoa ujuzi wa fani tofauti ikiwemo ufugaji nyuki, ushoni na elimu ya kilimo na tayari kimeshatowa jumla ya wanafunzi 1054 katika fani tofauti.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan