Skip to main content

IDARA YA KATIBA KUWASAKA WASIOJISAJILI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

MKURUGENZI wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar Hanifa Ramadhan Said, amesema msako mkali unakuja kuwabaini watu na taasisi, zinazofanyakazi za kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria, pasi na kujisajili kama sheria inavyotaka.

Alisema, Sheria ya namba 13 ya mwaka 2018 ya Msaada wa Kisheria  Zanzibar, inamtaka mtu yeyote au taasisi inayotaka kujishughulisha na kazi hiyo, kwanza kujisajili, ili kuwa halali kufanya kazi hiyo.

Alieleza kuwa, Idara imebaini wapo watu na hata taasisi zinaendelea kutoa ushauri, msaada na elimu ya kisheria, bila ya kujisajili, jambo ambalo ni kosa kwa mujibu wa sheria hiyo.

Mkurugenzi Hanifa, aliyasema hayo Septamba 16, 2023 ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makoyo Wawi Chake chake Pemba, wakati akijibu hoja za baadhi wa wahusika wa msaada wa kisheria, kwenye mkutano wa nusu mwaka, ambao umeandaliwa na Idara hiyo, kwa kushirikiana na UNDP.

Alieleza kuwa, msako utanzia katika wilaya za Wete, Micheweni, Chake chake na kumaliza wilaya ya Mkoani kwa Pemba, kisha kuhamia kisiwani Unguja.

Alieleza kuwa msako huo, hauna nia mbaya bali ni kuitekeleza kwa vitendo sheria ya Msaada wa kisheria ya Zanzibar, ambayo imelekeza mambo kadhaa, likiwemo la kujisaliji.



Aidha Mkurugenzi Hanifa, alisema jingine ambalo wameligundua ni kuwepo kwa Mawakili nao kijisajili kama wasaidizi wa sheria, jambo ambalo ni kosa kubwa zaidi.

‘’Ni kweli kati ya wasaidizi wasaidizi wa sheria 250 kwa Unguja na Pemba ambao hadi sasa walioshajisajili hawafiki hata nusu yake, na kwa upande wa wa Mawakili nao wapo waliojisajili kama wadaidizi wa sheria, wakae tayari tunakuja,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo wa Idara ya Katiba na Sheria Zanzibar kutoka Wizara ya Nchi, Ofisi ya rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar, alilipongeza shirika la UNDP kwa kuendelea kuwaunga mkono, katika shughuli zao mbali mbali.

‘’Hata mkutano huu wa nusu mwaka kwa wahusika wa msaada wa kisheria Zanzibar, wametusaidia kwa asilimia kubwa, na ndio maana hata washiriki kutoka kisiwa cha Unguja leo tunao,’’alieleza.

Aidha aliwakumbusha wasaidizi wa sheria, kuendelea kuifikia jamii, kuwaelimisha athari za udhalilishaji, migogoro ya ardhi, utelekezaji na rushwa, kwani ndio msingi mkuu wa kazi zao.



Hata hivyo amewakumbusha wasaidizi hao wa sheria kuwa, bado nia ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi wa ununuzi wa bajaji kwa taasisi 11 za wasaidizi wa sheria Zanzibar, bado ipo pale pale.

Akifungua mkutano huo, Afisa Mdhamini wa wizara hiyo Halima Khamis Ali, alisema kazi inayofanywa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, ni kubwa kwa jamii na taifa.




Alieleza kuwa, Mkurugenzi wake amekuwa akizaa mbinu na juhudi binafsi, kuhakikisha wasaidizi wa sheria na taasisi zao zinafikia malengo yao waliojipangia.

Aidha aliwasisitiza wasaidizi hao wa sheria, kuendelea kufanyakazi zao kwa ushirikiano, na taasisi nyingine, ili kuhakikisha wanafikia malengo yao.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema wakati umefika sasa kwa taasisi nyingine, kuongeza ushirikiano na wasaidizi wa sheria wanapokuwa na shughuli zao.

‘’Kwa mfano mabaraza ya miji, halmshauri na Manispaa, wanakuwa na shughuli kadhaa, kama za kuandaa sheria ndogo ndogo, msisite kutushirikisha,’’alifafanua.



Afisa sheria kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar Ali Haji Hassan, alisema kazi zinazofanywa na wasaidi wa sheria zitakuwa na uhai, ikiwa wenyewe watajiendeleza kielimu.

Baadhi ya washirika wa mkutano huo, akiwemo Fatma Khamis kutoka ZAPAO, alishauri kuwa, kunapokuwa na mikutano yao mikubwa ni vyema kuwepo na vipeperushi maalum.

Mkutano wa nusu mwaka ulijadili mambo kadhaa, ikiwemo tathimini na mwelekeo wa maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria mwaka 2023, maandalizi ya jukwaa la tatu la mwaka la maaada wa kisheria pamoja usajili wa watoa msaada wa kisheria.

                       Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch