Skip to main content

UNESCO: ''MKIWA WABUNIFU MAAFISA HABARI WANANCHI WATAJUA KINACHOENDELEA SERIKALINI''

 



NA SHAIB KIFAYA, PEMBA@@@@

                    

MAAFISA habari Kisiwani Pemba, wametakiwa kuwa wabunifu zaidi kutokana na  kukuwa kwa teknologia ya habari, ili kuifikishia jamii taarifa sahihi, kwa maendeleo ya taifa .

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Hassan Khatib Hassan, alipokuwa akifungua mafunzo ya siku mbili, kwa maafisa habari, uhusino wa Wizara na tasisi za serikali na waandishi wa habari, uliofanyika Gombani Chake chake.

Alisema licha ya kuwa na ukosefu mdogo wa utendaji na vitendea kazi, bado kuna umuhimu wa kupambana na kuisaidia jamii, juu ya kupata taarifa bora na za uhakika.

Alifahamisha, kwa sasa taarifa nyingi zisizokuwa sahihi zitawa katika mitando ya kijamii, hivyo ni vyema kwa maafisa hao na vyombo vya vijana wengi wasiokuwa na taaluma  kuwa wepesi na haraka kuilezea jamii juu ya usahihi na taarifa husika.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mtendaji Idara ya Program, Tume ya Taifa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ‘UNESCO’Aboud Iddi Khamis, alisema lengo ya mafunzo hayo, ni kuwajengea uwezo maafisa habari wa taasisi za Serikali kufahamu majukumu yao.

Aidha alifahamisha kuwa, maafisa hao ni wasaidizi wa wananchi, kwa kuwasemea kero zao ambazo zinazopaswa kufanyiwa kazi, na taa sisi husika kutokna na jambo linalolalamikiwa.

Nae Mkufunzi wa mafunzo hayo Imane Duwe alisema, mwandishi ni mtu muhimu wa tasisi, hivyo ni lazima kuhakikisha kuwa karibu na vyomba vya habari.

Alieleza kuwa, hilo ni kuhakikisha kazi zake zinafanyika kwa wakati na haraka kwa kuu habarisha umma kwa jambo lilofanyika.

Sambamba na hayo, alisema ni lazima mwandishi kuangalia mipaka ya utaji taarifa, ambazo zitaweza kuhatarisha usalama wa nchi, ili kuepusha taharuki inayoweza kutokea  katika nchi.

Mkuu wa Mawasiliano na habari kutoka Tume ya Taifa UNESCO Christina Musaroche alisema, ipo haja  ya kuwandaa mpango maalum kwa maafisa habari wa Wizara, kuwapatia mafunzo ya kuwakumbusha wajibu wao.

Alifahamisha kuwa, kwani bado wako nyuma kiutendaji ili kufikia mbele na kuwaboresha kazi zao, ambazo pia wananchi wanazisubiri kwa ajili ya kujua yanayofanywa na serikali.

‘’Tume ta taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itaendelea kukutana na maafisa habari na wale wa uhusiano, ili kuwambusha wajibu katika taasisi zao,’’alieleza.

Hata hivyo alieleza kuwa, ipo haja sasa kwa mafunzo mengine, kuwakutanisha wakuu wa taasisi za serikali na maafisa hao, ili kujua changamoto na namna ya kuzitatua.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, walisema bado baadhi ya wakuu wa taasisi hawajui umuhimu wa kuwepo kwa maafisa wa habari katika taasisi zao.

                      Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch