Skip to main content

TAMWA ZANZIBAR YATANGAAZA AWAMU YA PILI TUZO KWA WANDISHI WA HABARI

 


 

CHAMA cha Waandishi wa habari TAMWA-ZNZ kimesema jitihada zaidi zinahitajika  ili kuleta mabadiliko  ya baadhi ya sheria ,sera, na mifumo iliyopo  ambayo inaonekana  bado  inamnyima fursa  mwanamke za kushika nafasi za  uongozi  ili kuhakikisha usawa wa jinsia unazingatiwa kwa kuteuliwa au kuchaguliwa  kwa upande wanafasi za kiutawala na kisiasa. 

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Chama hicho wakati alipokua akizungumza na waandishi wa habari mjini Unguja katika mkutano maalumu ulilenga kuzinduliwa kwa awamu ya pili ya tunzo za waandishi wa habari kuhusu wanawake na uongozi pamoja natakwimu.

Alisema pamoja na  jitihada na hatua mbalimbali zinazochukuliwa na  Serikali  kuridhia mikataba ya kitaifa na kimataifa Pamoja na  malengo endelevu ya milenia na ASASI za kiraia zinazojihusisha na utetezi wa  haki za wanawake katika kuwajengea uwezo na kuwahamasisha kugombea nafasi mbalimbali.

Alisema bado takwimu  zinaonesha kuwa ipo namba ndogo  ya viongozi  wanawake katika ngazi mbali mbali ukilinganisha na wanaume katika nafasi za kiutawala  lakini Zaidi kwenye nafasi za kisiasa ambako bado kunaonekana mwanamke anakosa  fursa hasa katika nafasi za juu  zakushika uongozi katika miundo  ya vyama vya siasa vyenyewe  Pamoja na kuwa na  jumuiya za wanawake katika  vyama hivyo

Alieleza kuwa hadi sasa takwimu zinaonesha ni mawiziri 6 tu wanamwake  kwenye idadi ya mawaziri 18 ambapo ni  sawa 33.3 % vile vile katika nafasi za ma naibu mawaziri ambapo   hadi sasa ni 1 kwenye idadi ya manaibu Waziri 7 ambapo ni sawa na    14.3 %, hali   hii pia inaonekana katika nafasi za makatibu  wakuu wakuu 5 tu kati 12 ambao  ni wanaume sawa na  29.4 % samba na wakuu wa mikoa  ni 1 tu ndio mwana mke kati ya 5 hali hii pia  imejitokeza pia katika ngazi za halmashauri na serikali za mitaa wawilaya  kwenye  viongozi wa shehia 



 

Sambamba na hayo Mkurugenzi huyo alisema Chama cha waandishi wahabari waanawake Tanzania ofisi ya Zanzibar (TAMWA), ikishirikana na  Jumuiya wanasheria wanawake  (ZAFELA) na jumiya ya Utetezi wa jinsia na mazingira Pemba (PEGAO) kupitia  udhamini wa Ubalozi wa  Norwey nchini Tanzania inatekeleza mradi wa kuwainua  wanawake katika Uongozi (SWIL).

 

Aidha alisema kupitia   mradi huu wa kuwawezesha wanawake katika uongozi kwa  kiasi kikubwa  imeweza kulipa umakini wa karibu Zaidi , fursa uwezo, mapungufu juu ya jitihada kufikia kutambua usawa wa kijinsia  na uwewezashaji wa wanawake  hususan katika nafasi za uongozi .

 

Hata hivyo  kwa upande wa vyama vya siasa , baadhi ya vyama vimekuwa vikibana fursa kwa wanawake kuwapa nafasi za juu kuongoza kutokana na mifumo waliyonayo au kutokuwa na mikakati ya makusudi kwa kulizingatia suala la usawa wa jinsia katika nafasi za uongozi

 

Hivyo basi Pamoja na kuendesha shughuli mbalimbali   kupitia mradi huu TAMWA-ZNZ mwaka  2021  iliandaa mashindano ya uandishi mahiri  juu ya kuripoti  tawimu zinazohusiana na ushirikishwaji wa wanawake katika nafasi za uongozi   Zanzibar.

 

Lengo kuu La mashindano haya  ni kushajiisha  waandishi wa Habari kuandika Habari za umahiri ili kuhakikisha  tauluma ya umahiri Pamoja na mwamko katika fani ya Habari kwa kuzingatia  utambuzi wa vyombo vya Habari wenyewe juu ya dhamira ya TAMWA  katika kutetea haki za wanawake na Watoto  kwa kufanya  shughuli za kuengeza uwelewa  ikiwemo matumizi ya vyombo vya Habari kupitia  magazeti, televisheni, redio na mitandao ya kijamii.

 

Akifafanua Zaidi alisema katika zoezi hilo  lilifanikiwa  kuibua  na kuwapata washindi ambao ni waandishi  katika vyombo mbali mbali walioshinda  kutokana na kazi zao  zilizoshindanishwa  zilizozingatia matumizi sahihi ya takwimu, pamoja na vigezo vyengine vya habari za umahiri Zanzibar kupitia uanzishwaji wa tunzo ya uandishi wa habari ya “Sauti Yangu, Haki Yangu”  sambamba na kuwashajiisha wanahabari kuona umuhimu wa kuzingatia dhana hii katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku  ikiwa ni sehemu ya uwajibikaji wao  katika jamii na kuwafikia makundi yaliyo pembezoni  kuweza kupaza sauti zao kupitia vyombo vya Habari kwa  kuzingatia haki na usawa kijinsia.

 

Katika muendelezo wa shuguli za mradi  kwa mwaka huu   TAMWA ZANZIBAR imekusudia kuendesha  mashindano ya  Habari  zinazohusiana zinazohusiana na ushirikishwaji wa wanawake katika nafasi za uongozi   Zanzibar  na changamoto zinazokabili jamii katika kujenga jamii  ambayo inaheshimu  haki , heshima  katika usawa wa jinsia kwa kuzingatia makundi mengine yanayoishi na  mazingira magumu  na wanaotaka kusaidiwa kupaza sauti zao.

 

Katika mashindano  ya mwaka  2021 jumla ya   kazi 452  zilipokelewa, ambapo kazi 73 zilikuwa makala za magazeti, kazi 3 zilikuwa makala (documentaries) za televisheni, makala 116 zilikuwa za redio na makala 260  zilikuwa za mitandao ya kijamii kutoka vyombo mbali mbali  vya Unguja, na Pemba,  na kutolewa tuzo  kwa kila mshindi

 

Hata hivyo TAMWA Zanzibar  kwa kushirikiana na Jumuiya wanasheria wanawake  (ZAFELA) na jumiya ya Utetezi wa jinsia na mazingira Pemba (PEGAO) kupitia  udhamini wa Ubalozi wa  Norwey nchini Tanzania kupitia mradi wa SWIL inapenda kuwaalika na kuwataka ushiriki wao Waandishi wote kitaaluma na  wa kujitolea ambao huandikia magazeti  kutoka Unguja and Pemba  ambao Habari zao  wanachapisha  katika magazeti na Habari za kieletroniki kwa kuzisambaza  katika  maeneo mbali  mbali kwa kuwalenga   wahusika.

 

Vile vile TAMWA inawasisitiza  washiriki  wote walioshiriki katika shindano lilopita   ambao  alama zao hazikutosha kutumia fursa hii kuandika tena habari za umahiri zenye  dhumuni  linalohusiana  na  wanawake  na   uongozi kipindi cha mwaka  cha mashindano ya  2022 kwa kuzingatia vigezo vifuatavyo.

 

Akieleza kuhusu vigenzo vitakavyotumika katika kuhakiki kazi za waandishi na watayarishaji wa vipindi hadi kupata washindi, mbali ya kuzingatia vigezo vya kitaaluma na uandishi wa habari zenye umahiri, vigezo kadhaa kama vifutavyo,Ubora wa kazi  utakaowasilishwa  utaangaliwa uweledi, umahiri wa uandishi,Upekee wa mada ,Umuhimu wa kuzingatia uwiano wa usawa wa jinsia,vyanzo vingi vya habari vilivyojitawanya pamoja na ushirikishaji wa wananchi na  wadau(different sources)Ubunifu wa mada husika.

 

Mpangilio wa mada,Ufasaha na mtiririko wa lugha,Kuzingatia maadili ya uandishi wa habari,Uweledi wa matumizi ya takwimu,matokeo baada ya kutoka habari au kipindi hicho (impact) Kipindi cha Redio na Televisheni kisichozidi dakika 30 na kuzingatia ubora wa sauti na ubora wa picha.

 

Katika mashindano  ya mwaka  2021 jumla ya   Habari 452 zilikusanywa  kutoka vyombo mbali mbali  vya Unguja, na Pemba, Habari hizi ni kutoka magazeti ,radio,  televisheni  na mitandao ya kijamii  na kutolewa tuzo  kwa kila mshindi

 

Mradi wa kushajiisha ushiriki wa wanawake katika uongozi na demokrasia  ni mradi wa miaka minne (2020 – 2023), wenye lengo la kukuza ushiriki wa wanawake katika uongozi ambao unatekelezwa  na Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) jumiya ya Utetezi wa jinsia na mazingira Pemba (PEGAO) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kwa kushirikiana na Ubalozi wa Norway chini Tanzania.

  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch