Skip to main content

WAZAZI WAANZA KUTOA USHAHIDI KESI YA DAKTARI PEMBA

 



IMEANDIKWA NA HAJI NASSOR, PEMBA

MAHAKAMA ya Mkoa Wete imeanza kusikiliza ushahidi wa kesi ya daktari Is-hak Hadid Rashid anaedaiwa kumbaka mtoto wa miaka 16.

Shahidi namba moja ambae ni baba mzazi wa mtoto huyo alidai mahakamani hapo kuwa, Aprili 21 mwaka 2022 majira ya saa 10:00 jioni wakati anarudi kwenye pirika zake za kazi aliambiwa na mke wake kuwa, mtoto wao hajarudi skuli mpaka muda huo.

Alidai kuwa, hakufanya wasiwasi sana kwani aliamini kuwa itakuwa yuko kwa shoga zake baadae alikwenda bondeni na aliporudi saa 11 jioni aliambiwa bado mtoto huyo hajarudi.

“Nilikwenda kwa shoga zake kumuulizia, lakini hawakuwa na taarifa zozote, ndipo nikarudi nyumbani kushauriana na mke wangu na tukaamua kwenda kutoa taarifa kituo cha Polisi Madungu’, alidai baba huyo.

Mama wa mtoto huyo alidai mwanawe ni mwanafunzi wa kidato cha nne, ambapo alikwenda skuli majira ya saa 4:00 asubuhi kwa vile ilikuwa ni mwezi wa Ramadhani, ingawa ilifika muda wa kurudi skuli hajafika nyumbani, ndipo walipoanza kumtafuta na baada ya kutofanikiwa kumpata walikwenda kituo cha Polisi kutoa taarifa.

“Kwa kipindi chote alichoondoka mtoto wake alikuwa hapatikani kwenye simu yake mpaka pale alitaka mwenyewe kunipigia simu Aprili 25 mwaka huu na kuniambia kuwa yupo Kangagani  ambapo nyumbani aliondoka tangu Aprili 21 mwaka huu”, alidai mama huyo.

Alidai kuwa, baada ya kupigiwa simu na mwanawe huyo alimtaka arudi nyumbani kwao ingawa alifikia kwa mjomba wake na ndipo alipokenda kumchukua na kumpeleka Polisi.

Mara baada ya mtuhumiwa kupanda kizimbani akisubiri taratibu za mahakama, wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa mashitaka Juma Mussa Omar alipodai kuwa, shauri hilo lipo kwa ajili ya kusikilizwa mashahidi.

“Tunao mashahidi watatu ambae ni baba wa mtoto, mama, na mtoto mwenyewe, hivyo muhehismiwa hakimu tuko tayari kusikiliza mashahidi wetu”, alidai wakili huyo.

Baada ya kusikilizwa ushahidi wa baba na mama, mtoto anaedaiwa kufanyiwa kitendo hicho, katika ushahidi wake alikana kubakwa na daktari huyo na ndipo wakili huyo alipoiomba mahakama iliahirishe shauri hilo hadi tarehe nyengine.

“Muheshimiwa hakimu, ushahidi anaoutoa mtoto huyu hapa mahakamani ni wa uongo kwa sababu kituo cha Polisi alitoa maelezo na leo anayakana haya na kutoa mengine”, alidai DPP huyo.

Hakimu wa mahakama hiyo Ali Abdul-rahman Ali alikubaliana na ombi la upande wa mashitaka na kusema kuwa kesi hiyo itarudi tena Juni 22 mwaka huu kwa ajili ya kusikilizwa mashahidi.

Ilidaiwa kuwa, baina ya Aprili 21, mwaka huu mtuhumiwa huyo alimtorosha mtoto huyo kutoka nyumbani kwao Gombani wilaya ya Chake Chake na kumpeleka nyumbani kwake anakoishi Kangagani wilaya ya Wete, ambapo usiku wake alianza kumbaka na kuendelea kumfanyia kitendo hicho kwa siku tatu tofauti.

Kufanya hivyo ni kosa, kinyume na kifungu cha 113 (1) (a) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

Kosa la pili kwa mtuhumiwa huyo, baada ya kumtorosha mtoto huyo, siku hiyo hiyo majira ya saa 3:00 usiku alimbaka, ambapo ni kinyume na kifungu cha 108 (1), (2), (e) na 109 (1) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018.

Kosa la tatu, ambalo lilitokea Aprili 22 mwaka huu na la nne ambalo lilitokea Aprili 23, mwaka huu pia, alilitenda kwa nyakati tofauti za usiku, ambapo alidaiwa kumbaka mtoto huyo.

Kufanya hivyo, ni kinyume na kifungu cha 108 (1), (2), (e) na 109 (1) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

                                          MWISHO.

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch