Skip to main content

RC MATTAR: AAHIDI KUWATIMUA KAZI MASHEHA IKIWA.......

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

MKUU wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, amewahakikishia masheha mkoani humo, kuwa watakosa kazi na kisha kusughulikiwa kisheria, ikiwa watasimama kama mashahidi kuzifanyia sulhu kesi za udhalilishaji.

Alisema kwa sasa imekuwa ni mchezo endelevu mkoani humo, kwa baadhi ya masheha kujihusisha na sulhu kwa kesi za ukatili na udhalilishaji, jambo ambalo amesema sasa imetosha.

Mkuu huyo mkoa aliyaeleza hayo, wakati akilighairisha kongamano la kujadili changamoto za matendo ya ukatili na udhalilishaji, lililofanyika hivi karibuni mjiji Chake chake, lililoandaliwa na Jumuiya ya Tumaini Jipya Pemba TUJIPE.

Alisema kama kuna sheha ameshachoka kuhudumu kwenye nafasi hiyo, ajaribu kuzitia mkono kesi hizo, ambazo kwa sasa zimekuwa zikijotokeza siku hadi na kuvizisha juhudi za serikali na wadau wake.

Alieleza kuwa, sasa kila sheha lazima ajitenge mbali na kushiriki kwenye jamvi au vikao vya sulhu, baina ya wazazi wa pande mbili, na akigundulika hatua za kinidhamu dhidi yake zitachukuliwa.

Hata hivyo aliwataka masheha hao, wanapobaini uwepo wa matukio kwenye shehia yake kuwasiliana na yeye moja kwa moja, kabla ya kutoa taarifa kwenye mamlaka yoyote.

‘’Kama mpaka leo hii kuna sheha anajifanya ni sehemu ya mahakama kwa kuzikalisha pande mbili chini, ili sulhu ipatikane baada ya mtoto kudhalilishaji, kwanza hana tena kazi pili taratibu nyingine zitafuata,’’alieleza.

Katika eneo jengine Mkuu huyo wa mkoa, amelitaka Jeshi la Polisi mkoani humo, kuwasweka lupango, wazazi na walezi watakaobainika kuwatorosha vijana wao, wanaotuhumiwa kufanya makosa ya udhalilishaji.



Alisema wapo baadhi ya wazazi wamekuwa, wakitengeneza mazingira na kisha kuwatorosha vijana, wao wakijua kuwa wanatafutwa na Jeshi la Polisi kwa tuhma zinazowabili.

Alilitaka Jeshi la Polisi mara wabainipo mtuhumiwa kutoroka waanzishe uchunguzi na wakibaini kuwa wazazi wamehusika, waanze na wao kwa kuwaweka ndani hadi kijana wao atakaporudi.

‘’Jeshi la Polisi naliagiza rasmi, ikiwa kuna wazazi na walezi wamekuwa wakibuni mbinu na kuandaa mikakati ya kuwakimbiza watuhumiwa, msipate shida kamata mama, baba au mlezi weka ndani hadi mtuhumiwa arudi,’’alieleza.

Katika hatua nyengine Mkuu huyo wa Mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahoro Massoud ameitaka jamii, kuacha rushwa muhali na kwenda mahakamani kutoa ushahidi, ili watuhumiwa wapatiwe adhabu.

‘’Hakuna kesi itakayopatiwa hatia pasi na mashuhuda wa tukio kufika mahakamani kutoa ushahidi, lakini ikiwa mmezidiwa na rushwa muhali matendo hayo hayatokoma,’’alifafanua.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali, alisema kama hakuna njia ya kumaliza matendo, kama sio kuyaripoti kwa wakati.



Akizungumza kwenye kongamano hilo, Mratibu wa TUJIPE Pemba Tatu Abdalla Msellem, alisema moja ya jambo linalowaumiza kichwa ni wazazi na walezi kukubali sulhu kwa kesi za udhalilishaji.

‘’Wazazi wamekua wakali mara tukio linapotokezea, lakini linapoanza kufika mahakamani huanza dharura za hapa na pale na wakati mwengine hadi kumkana mtuhumiwa,’’alieleza.

Kamanda wa Polisi mkoa wa kusini Pemba Richard Tadei Mchomvu, aliwataka wazazi kuwa karibu na watoto wao, ili wanapopata shida kama ya udhalilishaji kupata taarifa mapema.

 

                     Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch