Skip to main content

MAKAMU WA PILI AKIWA PEMBA AWAPA TANBIH WAKANDARASI

 


NA ZUHURA JUMA SAID, PEMBA

MAKAMU wa Pili wa rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla, amewataka wakandarasi wa ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba, kuwa wazalendo na nchi yao, kwa kujenga jengo hilo la kisasa na lenye viwango vinavyokubalika kimataifa.

Alisema, moja ya jitihada za serikali ya awamu ya nane inakusudia kuimarisha kwa vitendo, huduma za afya na ndio maana imeamua kujenga hospitali za kisasa, hivyo ni wajibu kwa wakandarasi hao, kuheshimu hilo.

Makamu huyo wa Pili, aliyasema hato wakati akiwa katika ziara yake ya siku mbili kisiwani Pemba, alipofika wilaya ya Micheweni kuangalia maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya kisasa wilayani humo.

Alisema, ni lazima kwa wakandarasi kuweka uzalendo wao mbele, na hasa baada ya serikali kwa maksudi kuamua kuwatumia wakandarasi wazalendo.

“Kazi kwanza, iwe imara na muhakikishe mnajenga hospitali hii kwa kiwango kinachokubalika, na hilo litafanyika ikiwa mtaweka uzalendo wa nchi yenu mbele,’’alieleza.

Aidha Makamu huyo wa Pili, alifafanua kuwa hata rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, mara zote amekuwa akisisitiza haja ya kuwatumia wakandarasi wa ndani.



Aliwakumbusha wakandarasi hao, kumaliza kazi kwa wakati kama walivyoahidi na kusaini mikataba ya ujenzi, ili wananchi wapate kuyatumia kwa wakati.

“Nataka nione kwanza jengo hili la hospitali ya Micheweni na Maziwani kwa wilaya ya Wete na skuli za wilaya zilizopo  Makangale na Kinyasini nazo zinamalizika kwa wakati uliopangwa,’’alieleza.

Mapema akizungumza na wananchi wa Makangale, Makamu huyo wa Pili wa rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla, aliwataka, kulinda miundombinu ya majengo ya skuli, ili kutimiza azma ya kuondoa msongamano madarasani.

Alisema, moja ya wajibu wa wananchi ni kushirikiana na serikali yao, pale inapoanzisha miradi ya maendeleo, ikiwemo barabara, hospitali au ujenzi wa madarasa.

“Serikali ya awamu ya nane, sasa imo katika harakati za kutekeleza ahadi zake, sasa ni wajibu wa wananchi ni kuonesha ushirikiano wa karibu, ili kazi zifanyike kwa ufanisi,’’alisema.

Hata hivyo, amewakumbusha wakandarasi wanaobahatika kazi za ujenzi, kuwatumia wananchi na vijana waliokaribu na miradi hiyo, ili kujipatia ajira za muda.

Katika hatua nyengine, Makamu huyo wa Pili aliwasisitiza wajenzi wa vyumba saba vya madarasa eneo la Makangale wilaya ya Micheweni na Kiyasini kuharakisha ujenzi huo, ili mvua zitakapoanza wawe wameshakabidhi serikali.

Akiwasalimia wananchi wa shehia ya Kiyasini wakati akigagua ujenzi wa hospital ya wilaya, Makamu huyo wa Pili aliwataka kuhakikisha wanailinda miundombinu hiyo, ili endelevu.

“Hospitali hii ikimalizika itakuwa na vifaa vya kisasa, na kila aina ya mashine za uchuunguzi zinatarajiwa kuingizwa, lengo ni kuona wananchi wanapata huduma za uhakikia za afya,’’alieleza.

Nae Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba na kaimu wa Mkoa wa kaskazini Pemba Mattar Zahor Massoud, alisema fedha zinazotumika kwenye miradi hiyo ni za ahuweni ya COVID 19.

Alisema matumaini yake, miradi hiyo itakapomalizika iwasaidie wananchi kwa asilimia 100, ili waondokane na usumbufu walionao sasa.

Kwa upande wake waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui, alimshukuru Makamu huyo wa Pili, kwa juhudi za kipekee, katika miradi hiyo.

Alisema utamaduni wake wa kuyakagua miradi hiyo kuanzia hatua za awali, inaonesha dhahiri umakini wake katika kusimamia ujenzi wa miradi hiyo, ikiwemo hospitali ya Micheweni na Kinyasini.

“Sisi wizara tunafarajika kuona tokea ujenzi wa hatua za awali za hospitali za Micheweni na Kinyasini unautembelea, ili kuona uimarika wake,’’alieleza Mazrui.

Nae Mkadiriaji majengo kutoka Kampuni ya Group six ya China, Omar Asumani Mzirai, wanaojenga hospitali y wilaya ya Wete iliyopo Kinyasini, alisema sasa wana wiki ya saba tokea waanze ujenzi na umeshafikia asilimi 12 ya kazi yote.

“Mheshimiwa Makamu wa Pili, awali tulikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa huduma ya maji, lakini kwa sasa hilo limeshaandoka na tunaendelea na kazi,’’alisema.

Makamu huyo wa Pili na ujumbe wake ulitembelea ujenzi wa hospitali za wilaya za Micheweni na Kinyasni kwa Wete, ujenzi wa skuli za wilaya zilizopo Makangale na Maziwani mkoa wa kaskazini Pemba.

                           Mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch