Skip to main content

DUNIA ILIANZIA HAPA NA SASA IKO HAPA KUPIGANIA HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU

 



IMEANDIKWA NA HAJI NASSOR, PEMBA

KWA miaka mingi, suala la haki za watu wenye ulemavu halikuwa likoenekana na umuhimu wake, kuanzia hapa Zanzibar na duniani kote.

Dunia wakati inasonga mbele, hadi kufikia miaka ya 80, ambapo Umoja wa Mataifa UN, jumuiya za watu wenye ulemavu zilianza kutetea upatikanaji wa haki za binadamu kwa watu wenye ulemavu.

Suala ka kutetea haki za watu wenye ulemavu, lilijotokeza hata kwenye vita vya kwanza vya duniani vya mwaka 1914 na vile vya pili vya mwaka 1918, baada ya kujitokeza kwa majeruhi kadhaa.

Mitandao ya kijamii inahabarisha kuwa, kwa wakati huo waliotetea na kupata haki zao za matibabu na huduma nyingine ni wale, waliopkumbwa na madhila kwenye vita hivyo pekee.

Katika eneo jengine mwaka 2006, Umoja wa Mataifa ulianzisha mkataba wa kimataifa kuhusu haki za watu wenye ulemavu (UN -Convention on the Rights of Persons with Disabilities- UNCRPD).

Shabaha kubwa ya mkataba huo ilikuwa ni kulinda na kuboresha hali ya watu wenye walemavu duniani kote, wapatao 650.

Na tayari hadi mwaka 2015, mataifa 159 yashautia saini mkataba huo na mataifa 154 kati ya hayo, yaliidhinisha hatua hiyo.

Mataifa yaliyokubali mkataba huo yamepokea wajibu wa kuhakikisha haki sawa za elimu, ajira, kumiliki mali na kuoa, kama walivyo watu wengine.

Mikataba hiyo pamoja na mambo kadhaa, ipo mikataba ukiwemo wa Umoja wa Mataifa ya Haki za Watu Wenye Ulemavu, ulioasisiwa mwaka 1945, mkataba wa Kimataifa wa Haki za Binaadamu.

Lakini kulikuwepo kwa viwango vya kanuni na sheria juu ya nafasi sawa kwa watu wenye ulemavu wa mwaka 1973, samba mba na Mkataba wa kimataifa juu ya Haki za Watu Wenye Ulemavu (UNCRPD) wa mwaka 2009.

ZANZIBAR

Kwa upande wa Zanzibar, masuala ya watu wenye ulemavu yalianzia katika ustawi wa jamii chini ya wizara ya Afya kwa wakati huo.

Kisha mwaka 2004, yakahamishiwa chini ya Ofisi ya Waziri Kiongozi ambapo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) iliunda Idara ya Watu Wenye Ulemavu.

Pamoja hatua hiyo, pia serikali ilianzisha Baraza la taifa la watu wenye ulemavu mwaka 2008, ambapo sasa masuala ya watu wenye ulemavu yanashughulikiwa kupitia Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais.

 

SERA, SHERIA NA MIONGOZO YA ZANZIBAR

Kuanzia hapo Zanzibar, ilianza kutambua na kusimamia haki za watu wenye ulemavu, kutokana na hamasa ya kimataifa na kikanda pia.

 

Ndio maana hivi karibuni, Makamu wa Kwanza wa rais Zanzibar Othman Massoud Othman, ambapo Idara ya watu wenye ulemavu iko chini yake, amesema lazima kila mmoja asimamie haki za watu hawa.

 


Anasema, suala la kusimamia haki za watu wenye ulemavu, uwepo wa mikataba, sheria na kanuni ni hatua moja, lakini pili ni ngazi ya jamii kuona wanapatiwa haki zao.

 

“Kila mmoja katika familia yake, wapo watu wenye ulemavu wa aina yoyote ile, sasa ni wajibu kabla hata ya uwepo wa sheria, kuona kundi hili ni sehemu ya jamii na wanastahiki haki zote,’’anasema.

 

Rais wa sasa wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, amekuwa akirejea mara kwa mara, kuitaka jamii kuwalinda kwa nguvu zote watu wenye ulemavu.

 

Anasema, watu wenye ulemavu wana haki sawa kama walivyo wengine, hivyo suala la kuwafanyia ukatili na udhalilishaji lisipewe nafasi.

 

KATIBA YA ZANZIBAR

Kwa upande wa Zanzibar, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambayo inayokatiba yake ya mwaka 1984, pamoja na marekebisho yake ya mwaka 2010, imetambua kuwa watu wote wako sawa mbele ya sheria.

Kwa mfano katika kuona kundi la watu wenye ulemavu halibaguliwi, kifungu cha 11 cha katiba hiyo kimetaja usawa wa binadamu, kifungu cha 14 cha haki na uhuru wa mtu binfsi.

 

SHERIA no 9/2006 HAKI NA FURSA

Sheria hii yenye vifungu 47 na sehemu sita, imetungwa mwaka 2006, ili kukidhi haja na kuonesha haki za watu wenye ulemavu Zanzibar.

Kwa mfano kifungu cha 15 cha sheria hiyo, kimeanisha taarifa ya mawasiliano, (1) kimetamka kuwa vituo vyote vya televisheni, vilivyosajiliwa Zanzibar vinatumia lugha ya alama.

“Au televisheni hizo, zinatumia maandishi katika taarifa zao ili, viziwi watumie maandishi katika taarifa zote za habari, vipindi vya elimu na vile vya matukio ya kitaifa,’’kinafafanua kifungu hicho.

 

SERA YA WATU WENYE ULEMAVU

Sera hii imeweka ajenda za Kitaifa ili kuhakikisha ujumuishaji wa watu wenye ulemavu kwa kuzingatia mchakato wa kimaendeleo.

Serikali, imeandaa sera hii ili kuifanya kuwa ni chombo muhimu cha kutoa maelekezo ya masuala ya watu wenye ulemavu.

Aidha ni kusaidia mchakato wa fursa sawa, kupunguza umaskini na kukuza ujumuishaji wao katika ngazi ya jamii na serikali kuu.

Sera imebainisha  baadhi ya changamoto na vikwazo vinavyowakabili watu wenye ulemavu Zanzibar, ikiwemo ufikiaji wa miundombinu, upatikanaji wa huduma za umma.

 

Huduma za afya kwa kundi hilo, ikitajwa kuwa bado hakuna dirisha wala eneo maalum, ambalo linaweza kutumiwa na watu wenye ulemavu.

 

Suala la upatikanaji wa taarifa, haki katika masuala la kisheria, jambo linalotajwa kuwakwaza na kuwarejesha nyuma watu wenye ulemavu

 

Khamis Abdalla Sururu ambae ni Mkurugenzi wa Jumuia kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa akili Zanzibar ‘ZAPDD’ anasema suala la vikwazo kwa watu wenye ulemvu linatengenezwa na jamii.

 



“Watu hawaoni umuhimu wa kuweka miundombinu ambayo yatakuwa wezeshaji kwa watu wote, hadi pale anapopata tatizo na kupelekea ulemavu,’’anasema.

 

Sururu anasema watu wenye ulemavu, wameshajielewa nafasi yao, na kazi sasa iko kwa wale ambao wanaona hawa ulemavu, na sasa ni kuandaa mazingira rafiki sasa.

 

Anasema kama kuna ujenzi wa majengo ya umma, kama skuli, hospitali, barabara na hata kufikia huduma za kibenki ni wakati sasa kuweka mazingira rafiki.

 

Bimkubwa Mohamed Ali ambae ni mjumbe kwenye Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu JUWAUZA, anasema bado watu wenye ulemavu wanakabiliwa na chungu ya changamoto.

 

“Mfano hata unapokwenda benki kutoa fedha kwenye mashine ‘’ATM’ hakuna nambari za nukta nundu, jambo linalowatesa watu wasioona,’’anasema.

 

INETERNEWS

Ni moja ya shirika la kimataifa linalowajengea uwezo waandishi wa habari katika kuwapa mbinu za uandishi bora wa habari za watu wenye ulemavu.

 

Katika mafunzo yaliofanyika hivi karibuni Zanzibar baina ya Machi 7 hadi 8, na kushiriki kwa waandishi wa habari wa Unguja na Pemba, walielezwa hata majina sahihi ya kutumia.

 

Mkuu wa program kutoka Internews Tanzania Shaban Maganga, aliwaeleza waandishi hao kuwa moja ya jina sahihi ni kusema mtu mwenye ulemavu na sio mwenye ulemavu.

 

“Wapo waandishi wamekuwa wakieleza ulemavu wa mtu kwanza na kusahau ubinadamu wake, jambo ambalo ni kinyume na haki za binadamu,’’anasema.

 


Mhariri mtendaji wa shirika  la Magazeti ya serikali Zanzibar Ali Haji Mwadini, alisema waandishi wa habari wasipokuwa makini wanaweza kuwaumiza watu wenye ulemavu.

 

“Unapoandika neno ‘kiwete’ badala ya mtu mwenye ulemavu’ au mfano neno jengine lisilokubalika ni kusema ‘kipofu’ badala ya mtu asieoona na kumwita ‘asiyesikia’ badala ya kiziwi unaweza kuwadhalilisha,’’anasema.

 

WANANCHI

Hilali Omar Mjaka wa Chake chake, anasema kinachoonekana bado jamii haijakuwa tayari kuzitekeleza haki za watu wenye ulemavu.

 

Aisha Hussein Sadala wa Mchanga mdogo, anasema kama sheria na kanuni hazitumika kuwaabidhi wanaozipinda haki na fursa za watu wenye ulemavu, kundi hilo litaendelea kupata shida.

WAANDISHI W AHABARI

Fatma Hamad Faki mwandishi wa blog ya pembayaleo, anasema kunahitaji uthubutu na ujasiri ili kuyafikia makundi ya watu wenye ulemavu.

 

Mwandishi wa mitandao ya kijamii Zanzibar Yassir Mkubwa, amesema mafunzo ya siku mbili yalioandaliwa na Internews yamempa mwanga.

 

“Sasa nimeona maeneo ‘angle’ ambazo naweza kuziandikia habari na kutengeneza vipindi vya kuwasaidia watu wenye ulemavu,’’anasema.

 

 

 

                                 Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch