Skip to main content

KAMATI MTEGA WAWI YATOA ONYO LA MWISHO WACHIMBA MCHANGA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA

KAMATI ya Maendeleo ya kijiji cha Mtega shehia ya Wawi wilaya ya Chake Chake, imeahidi kuwachukulia hatua za kisheria, wananchi wote wenye tabia ya kuchimba mchanga kwenye barabara yao, iliyoingia kijijini kwao.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Khamis Haji, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya tabia iliyojitokeza ya uchimbaji mchanga na kusababisha mashimo kwenye barabara hiyo.

Alisema, waligundua hilo baada ya kuitembelea barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 2.5, ambapo alisema waligundua mashimo yenye kina kirefu, ambayo yanaweza kuhatarisha uimara na uendelevu wa barabara hiyo.

Mwenyekiti huyo alisema, lazima wawachukuliwe hatua za sheria, ambao watawakamata wakiichimba barabara hiyo kwa kuchukua mchanga, kwa ajili ya ujenzi.

“Baada ya hivi karibuni kuitembelea barabara hii nikiwa na wajumbe wa kamati hii, tulikuta vishungu vya mchanga pembezoni mwa barabara yetu, na kwamba wapo wanaoichimba kwa maslahi yao,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti huyo alisema, ni vyema kila mmoja anayetumia barabara hiyo, kuwa mlinzi kwa wananchi wanaoichimba barabara hiyo, kwani inapoharibika athari yake huwa kwa wote.

Nae Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Omar Mohamed, aliwataka wale ambao hawajamaliza michango yao, kuharikisha kufanya hivyo, ili zipatikane fedha kwa ajili ya ununuzi wa kifusi.

Alisema, waliamua kupanga mikakati ya kuchangisha fedha kwa kila nyumba shilingi 50,000 ili zipatikane kwa ununuzi wa kifusi ikiwa hatua kuikoa barabara hiyo.

“Kwa wale ambao bado wanasua sua kwenye michango, lazima wajikaze, maana msaada wa kwanza kwa ujenzi wa barabara hii ni wananchi wenyewe, na kisha ndio tutafute wafadhali wengine,,’alieleza.



Nao mjumbe wa kamati hiyo ya maendeleo, Rashid Khamis Mussa na Khalfan Khamis, waliwaomba wabunge na wawakilisha kuwasaidia kifusi au fedha taslimu kwa ajili ya kuiokoa barabara hiyo.

Walisema, kama wapo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi, basi ni vyema wakajitokeza na kuwasaidia kifusi au rasilimali fedha, ili waondokane na ubovu wa barabara yao.

Baddhi ya wananchi wanaotumia barabara hiyo, wameahidi kuwaelimisha wenzao, juu ya kuacha kuchimba mchanga kwenye barabara hiyo, na watakapowakamata watawafikishwa mbele ya kamati.

Khadija Omar Said na Ismail Haji waliiomba kamati hiyo, kufanya ziara ya mara kwa mara kwenye barabara hiyo, ili kusaidiana nao, kwa vile baadhi ya wachimbaji mchanga wameshakuwa wasugu.

Nae Afua Ali Bakari, alisema wapo baadhi yao wamekuwa wakitumia hata gari za Ng’ombe nyakati za usiku wakati wanapochimba mchanga kwenye barabara hiyo.

Mhandisi ujenzi wa barabara kutoka wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji kisiwani Pemba Khamis Massoud, aliutaka uongozi wa Kamati hiyo, kujitolea usafiri wao na kuchukua kifusi kwenye kware zao.

Alisema, kwa sasa gari zao za kusambaazi kifusi zinaendelea kutumika kwenye ujenzi wa barabara mbali mbali, hivyo itakuwa vigumu kutumika sehemu nyingine na ambayo haina dharura.

“Sisi baada ya kupokea maombi yao kutaka kifusi, tumeshawaruhusu wakachukue kifusi, kama ni Vitongoji au Pujini, lakini lazima wawe na gari zao maana za kwetu, zina kazi maalum,’’alisema.

Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 2.5 ambayo imeanzia kambi ya mwanzo wa Jeshi la wananchi wa Tanzania Wawi na kuishia tawi la zamani la CUF, imeasisiwa na wananchi wa kijiji cha Mtega shehia ya Wawi miaka 15 iliyopita.

Ambapo uongozi wa kijiji hicho, tokea mwaka 2018, ulitangaaza kupokea michango ya wastani wa shilingi 50, 000 kwa kila nyumba, kati ya nyumba 80, ili wajipatia shilingi milioni 4 ingawa hadi sasa wameshakusanya shilingi 1,000,000.

                            Mwisho

    

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch