Skip to main content

MJASIRIAMALI PEMBA AWATAKA VIJANA KUKIMBILIA KILIMO

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA

MJASIRIAMALI wa mboga na matunda ya biashara ikiwemo ndimu, Mkubwa Ali Mkubwa wa Vitongoji wilaya ya Chakechake Pemba, amesema anawashangaa vijana wanaopanga foleni kusubiri ajira ya serikali, na kukipa mgongo kilimo.
Alisema huu sio wakati kwa vijana kupanga foleni kwenye ngazi za maofisi ya serikali, kwa kusubiri ajira zisizotosha, na badala yake wakijpanga vyema kwenye kilimo, wanaweza kupata mafanikio ya haraka.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi shambani kwakwe Makaani Shehia ya Vitongoji wilaya ya Chakechake, alisema hakuna serikali inayowatosheleza wananchi wake kiajira, hivyo ni vyema kwa vijana wakajikusanya ili kuendesha kilimo.
Alisema kwenye kilimo sifa yake kubwa hakuna kusubiri mwisho wa mawezi matumizi yake, bali ni wakati wowote, baada mazao kupevuka, jambo ambalo ndio njia rahisi ya kupungaza ukali wa maisha.
“Mimi hata leo ukiniambia niache kilimo niendele serikali, wala sikukilizi, maana sasa ndimu, tungule, vitango, vitunguu maji, mchicha na migomba ndio utajiri wangu’’,alifafanua.
Mjasiriamali huyo anaemiliki shamba la mchanganyiko wa mboga mbali mbali , lenye ekari zaidi ya mbili na nusu, alieleza kuwa, kwa msimu mmoja wa uvunaji, hujipatia wastani kati ya shilingi milioni mbili (2,000,000), na kwa msimu wa mwaka huu malengo yake yamepata mtikisiko kutokana na soko kuanza kupwaya.
Alieleza kuwa, kwa sasa ndimu zenye thamani ya zaidi ya shilingi 600,000, vitango vyenye thamani ya shilingi 200,000, tungule zenye thamani ya shilingi 800,000 na gunia mbili na nusu za vitunguu maji anavyotarajia kuvuna, soko lake anamashaka nalo.
“Unajua kila msimu wa uvunaji kipindi kama hichi, huwa tayari wateja wameanza kujitokeza hadi kufuata bidhaa huku kwenye shamba, lakini kwa msimu huu, mambo sio mazuri na hasara iko njiani kunifika,’’alieleza.
Katika hatua nyengine, mjasiriamali huyo ameziomba taasisi zenye kutoa mikopo kwa wafanyabiashara, kuacha kuweka riba, kwani kufanya hivyo, huwakosesha wengine haki hiyo.
Hafife Juma Hamad aliejiriwa na mjasiriamali huyo alisema, maisha yake yamebadilika kiasi, hasa kwa vile hana wasiwasi wa kusaidia familia yake kifedha.
“Hukaa wee, lakini kisha hulipwa kati ya shilingi 150,000 hadi shilingi 200,000 ambapo malipo hayo hutegemea na mavuno yalivyo, ambpo kwangu mimi hii ni faraja,’’alifafanua.
Nae Saada Ali Mkubwa, alisema mjasiriamali huyo, kwake amekuwa mkombozi, kutokana na kumsaidia kupata ajira kwenye sekta ya kilimo.
“Mimi hapa nipo kiajira, lakini pia najifunza jinsi ya kilimo cha kisasa kupitia mjasiriamali huyu, lakini soko ndio tatizo, maana mboga zisiponunuliwa na sisi hata kipato chetu hushuka,’’alifafanua.
Aidha waajiriwa hao wamesema malengo yao ya baadae sio kubakia hapo, bali na wao ni kuanzisha mboga mboga kama hizo, kwa vile wamekuwa pia wakipata ujuzi wa namna bora ya kilimo.
Sheha wa shehia ya Vitongoji Ayoub Suleiman Salim, amemtaka mjasiriamali huyo, kujiunga na vikundi vya saccos, ambavyo hutoa fedha bila ya riba.
“Kama anaona mabenki na taasisi nyengine zinatoa mikopo yenye riba, basi ajiunge na vikundi vya kuweka hisa, wapo wengi waliochukua mikopo mpaka shilingi 800,000 hadi shilingi milioni moja na sasa wako vizuri,’’alifafanua.
Mjasiriamali huyo alieacha kazi ya ujenzi wa nyumba na kujiingiza kwenye kilimo cha mboga mboga, alianza na mtaji wa shilingi 500,000 na kwa sasa ameshachimba kisima na kwa mwaka wa kwanza alipata mvuno ya shilingi 600,000 mvuno wa pili shilingi milioni mbili, na mvuno wa tatu alipata shilingi 1,000,000 na kwa sasa anategemea kuvuna mazao yenye thanani ya shilingi 1,000,000 ingawa inategemeana na soko.
Tayari serikali ya awamu ya nane, imetenga shilingi bilioni 81 kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wajasiriamali kadhaa wa Zanzibar, ili kuinua mitaji na vipato vyao.


ba

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch