Skip to main content

IDARA YA KATIBA, MSAADA WA KISHERIA YAPEWA MBINU KUWAFIKIA WATU WENYE ULEMAVU

  

NA HAJI NASSOR, PEMBA

IDARA ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, imeshauriwa kuandaa mazingira rafiki, ili kuwafikia watu wenye ulemavu kuwapa elimu, ushauri na msaada wa kisheria.

Ushauri huo umetolewa na msaidizi wa sheria kutoka wilaya ya Micheweni Saleh Hamad Juma, alipokuwa akichangia taarifa ya maadhimisho ya tatu ya wiki ya msaada wa kisheria kwenye mkutano uliofanyika Gombani.

Alisema, kundi la watu wenye ulemavu na hasa kwa mazingira yao, wamekuwa wakisahauliwa mno na hawafikiwi ipasavyo na msaada, ushauri wa sheria.

Alisema, suala la kuitisha mkutano pekee kwenye maeneo husika bila ya kuzingatia mazingira rafiki ya watu wenye ulemavu, wataendelea kukosa msaada wa kisheria, ambao ni haki yao.

Kwa upande wa Mjumbe wa Baraza la taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar Ayuoub Juma Shaame, aliishauri Idara hiyo kuweka wakalimani maalum, kwenye wiki ya msaada wa kisheria, ili kuwasaidia viziwi.



“Pamoja na kuimarisha mazingira kwa ajili ya watu wenye ulemavu, lakini msisahau kuweka wakalimani kwenye shughuli za utoaji wa msaada wa kisheria, ili wenzetu viziwi wapate taarifa,’’alishauri.

Mapema akifungua mkutano huo wa robo mwaka wa kuratibu masuala ya msaada wa kisheria, Afisa Mdhamini wizara ya Katiba na sheria Pemba Halima Ali Khamis, alisema Idara hiyo, imekuwa mstari wa mbele kuwafikia wananchi.

Alisema Idara hiyo kupitia Mkurugenzi wake Hanifa Ramadhan Said, imekuwa ikiyafikia makundi kadhaa ndani ya jamii, kuwapa ushauri na msaada wa kisheria bila ya malipo.

“Lazima nimpongeze Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na msaada wa kisheria, amekuwa halali ili kuhakikisha jamii inapata haki zao za kisheria,’’alieleza.



Mapema Mkurugenzi wa Idara hiyo Zanzibar Hanifa Ramadhan Said, alisema awali mkutano kama huo, ulikuwa ukifanyika Unguja pekee, ingawa kwa mwaka huu unafanyika na Pemba.

Alisema, Idara imekuwa ikifanyakazi kwa karibu mno na wasaidizi wa sheria waliopo kila jambo la uchaguzi, ili kuhakikisha jamii hailalamikii kwa kukosa uwelewa wa msauala ya kisheria.

Akiwasilisha taarifa ya maadhimisho ya tatu ya wiki ya msaada wa kisheria, Afisa sheria kutoka Idara ya Katiba na msaada wa sheria Pemba Bakar Omar Ali, alisema kwa upande wa Pemba wiki hiyo ilifanyika Micheweni.

Alisema wananchi 3,160 walifikiwa na elimu ya msaada wa sheria, wakiwemo wanawake 1, 483 na wanaume 1, 677 ambapo hilo ni baada ya Idara, kushirikiana na wanasheria wengine katika kambi hiyo.

Akiwasilisha muhutasari wa rasimu ya ripoti ya mwaka msaada wa kisheria ya mwaka 2020/2021, Afisa Sheria wa Idara hiyo Zanzibar Ali Haji Hassan, alisema wananchi 4,339 walifikiwa kupata msaada na ushauri wa kisheria Zanzibar.

Alisema kwa mwaka 2019/2020 waliofikiwa ni wananchi 1,346 ambapo inaonesha utendaji kazi wa kukua hasa kutokana na ushairikiano uliopo, wa watoa msaada wa sheria na wasaidizi wa sheria.



Wakichangia katika mkutano huo, washiriki ambao ni watoa msaada wa kisheria na wasaidizi wa sheria, walisema bado elimu zaidi inahitajika kwa jamii.

Kwa upande wake Kaimu Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzbar ‘ZLSC’ tawi la Pemba Safia Saleh Sultan, alisema kazi inayofanywa na Idara hiyo ni kubwa, na inafaa kuungwa mkono.

Nae Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema wakati umefika kwa wiki ya msaada wa kisheria, kufikia kila wilaya.

“Hata kama ile siku ya wiki ya msaada wa kisheria itakuwa ni siku tatu, tuangalie uwezekano kila wilaya, wananchi wafaidike nayo kuliko kwenda wilaya moja pekee,’’alishauri.

Mkutano huo ulifungwa na Mkurugenzi wa Idara ya Katiba na msaasa wa kisheria Zanzibar Hanifa Ramadhan, aliyesisitiza ushirikiano baina ya watoa msaada wa sheria, wasaidizi wa sheria na viongozi wengine. 

                         Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch