Skip to main content

WAJAWAZITO WAKUMBUSHWA JAMBO PEMBA

 




NA HAJI NASSOR, PEMBA

WANAWAKE wajawazito nchini, wametakiwa kuchukua tahadhari zaidi ya kujikinga na maradhi mbali mbali ya mripuko, ikiwa ni pamoja na matumbo ya kuharisha, kwani kinga za miili yao hupungua nguvu kwa kule kubeba ujauzito huo.

Ushauri huo umetolewa na daktari wa afya ya uzazi kituo cha Afya Wambaa Mkoani Mafunda Mohamed Khamis, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya tahadhari zaidi, kwa mama wajawazito kujikinga na magonjwa ya mripuko.

Alisema, kitaalamu mjamzito na hasa ikiwa afya yake sio ya kawaida anakuwa rahisi kukumbwa na magonjwa ya mripuko, ikiwemo kuharisha ikiwa hatochukua tahadhari zaidi.

Alieleza kuwa, mwanamke wa kawaida ambae hana ujauzito au mwengine yeyote, anaweza kuchelewa kidogo kuandamwa na magonjwa ya kuharisha, hata ikitokezea amekula tunda lisilooshwa na lina bektiria.

“Ni kweli mama mjamzito anatakiwa kuchukua kinga mara mbili ikiwemo kupenda kutembea na viatu, kulala kwenye chandarua, kunywa maji safi na salama kwa wingi na hata kupendelea kukosha matunda kabla ya kuyala,’’alieleza.

Aidha daktari huyo alisema, kila mtu anapaswa kuchukua tahadhari, ili kuikinga afya yake na magonjwa mbali mbali hasa ya mripuko, lakini mama mjamzito ni zaidi.

Alielezwa kuwa, magonjwa kama ya kuharisha, corona, macho tongo, homa ya mapafu, homa ya matumbo, kipindu pindu, kuharisha damu na hata maradhi ya vikope, ni magonjwa yanaweza kumpata mtu yeyote.

“Mama mjamzito huwa tunawasisitiza zaidi kuchukua tahadhari na magonjwa ya mripuko, maana akiathirika yeye, na kilichomo tumboni kuna uwezekano mkubwa pia,’’alieleza.

Mwanaisha Makame ambae ni mjamzito alisema, tokea wiki mbili za mwanzo baada ya kujigundua ana ujauzito, amekuwa akinywa maji yaliomchemsha, ikiwa ni njia moja yapo ya kujikinga na magonjwa yatokanayo na maji machafu.

“Niliambiwa wakati nilipohudhuria kliniki kuwa, maji yana asilimia kubwa ya kufuatana na magonjwa kama ya mripuko kam vile homa ya mapafu, kuharisha damu na kipindu pindu, sasa lazima nijikinge,’’alieleza.

Nae Husna Haji Kassim wa Mtambile, alisema ijapokuwa magonjwa kama minyoo na malaria sio ya mripuko, lakini amekuwa akijinga, ili yasiwe sababu ya kujitokeza magonjwa mengine.

“Elimu ya kujikinga na magonjwa ya mripuko tumekuwa tukipewa sana kila tunapohudhuria kliniki, changamoto wakati mwengine na hali ya umaskini ndio kikwazo,’’alieleza.

Hivi karibuni, akizungumza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku na unawaji mikono duniani, mwakilishi wa Shirika la Afya Ulimwenguni ‘WHO’ Vendelin Tarmo Simano, alisema njia moja ya kukabiliana na maradhi ya mripuko, ni jamii kuwa rafiki wa maji.

“Maji ndio yanayoweza kusababisha magonjwa yote tusipofyanya rafiki, lakini pia ndio kinga ya magonjwa kama vile kuharisha, homa ya mapafu, kipindu pindu na macho tongo kama hatukuwa makini,’’alieleza.

Hivyo, ameitaka jamii kujenga utamaduni wa kutumia maji safi na salama iwe kwa kunywa, kunawish mikono na sabuni za maji ili kujikinga na maradhi mbali mbali ya mripuko.

Kwa upande wake Afisa Mdhamini Waziri wa Afya  Pemba Dk. Shoka Mohamed Yakoub, alisema wizara imekuwa ikitumia vituo vya afya na kliniki, ili kuwapa uwelewa mama wajawazito.

Nae Mkuu wa kitengo cha Homa ya Ini, Kifua kikuu na Ukoma Pemba, Hasnuu Fakih Hassan, aliitaka jamii kuchukua tadhari ya magonjwa ya mripuko.

Hata hivyo Mkurugenzi Kitengo cha Elimu ya Afya Zanzibar Halima Ali Khamis alisema, miongoni mwa maradhi 10 yanayochukua nafasi ya juu Zanzibar, yale ya mripuko na yamo.

                            Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch