Skip to main content

WANAWAKE ‘WALIOTEMWA’ NA WAJUMBE 2025 WAJISUKA UPYA 2030, TAMWA YATOA RAI

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

‘’NA mwaka 2030, najitupa tena jimboni, na napandisha ngazi, nitaomba Ubunge jimbo la Kojani,’’ndivyo alivyoanza Katija Mbarouk Ali.

 

Akiwa pembezoni mwa nyumba yao, eneo la Kiuyu Minungwini, akijivalia kanga za chama cha Mapinduzi, huku akichezea simu yake.

 

Katija, ni mcheshi, mweye sura ya bashasha pamoja na kwamba, anawania kuwa kiongozi, kwa sasa ni mjasiriamali.

 

Akizungumza nami huku, akiangaza macho yake usoni kwangu, na kwa upole, analiambia safari ndio kwanza, inaanza.

 

Kumbe kwa uchaguzi wa 2025, Katija pamoja na ulemavu wake wa viungo, aligombea nafasi ya Uwakilishi jimbo la Kojani, na kisha wajumbe kumkataa.

 


‘’Si wajumbe mara hii bado wameniona ni mchanga, mwaka 2030, roho zikifika najitupa tena jimboni humo, kwa nafasi ya ubunge,’’anasisitiza.

Nilipomuuliza, kama ameyapata machungu kwa uchaguzi wa mwaka 2025, anasema, ameyaona kama mbolea na kumuongezea mwendo.

 

‘’Hakuna kukata tamaa, maana sheria, katiba na mikataba yote ya kikanda na kimataifa, haijamzuia mwanamke kugombea,’’anasisitiza.

 

Sio Katija pekee, ambao kwa uchaguzi wa 2025, wajumbe na wapiga kura wamewakataa, lakini kwa Pemba wapo wanawake 25, kwa nafasi mbali mbali.

 

Mwingine aliyegombea nafasi ya Uwakilishi Jimbo la Mtambile Asha Said Suleiman, kwa tiketi ya ADA-TADEA, anasema neno kuvunjika moyo kwenye maisha yake, halijazaliwa.

 


….aaaa…..kumbe Asha, anataka kuishi kwenye msemo wa wahenga, kuwa mgaa gaa na upwa, abadani hali ugali mkavu.

 

Anaamini kugaa gaa, ni kule kuendelea kuchukua tena fomu, mwaka 2030, na anaamini kula ugali na samaki, ni kushika madaraka ya uongozi.

 

Anasema, moja ya changamoto alizoziona ni, wagombea wanaume, kujiona kama vile nafasi za uongozi, zimeumbiwa wao.

 

‘’Nilikwenda kijiji kimoja ndani ya Jimbo la Mtambile, wakati wa kampeni zangu za nyumba kwa nyumba, niliulizwa kama nastahiki kuwa Mwakilishi,’’anakumbusha.

 

Anaona, kuanzia wapiga kura na jamii kwa ujumla, haimini kuwa mwanamke, anahaki ya kuwa kiongozi na kuleta mabadiliko.

 

Lakini kumbe hata Khadija Anuwari, aliyegombea nafasi kama hiyo jimbo la Wawi, kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, bado anasema vipo vyombo vyenye mamlaka, sio rafiki kwao.

 


‘’Bado inaonekana mwanamke kama vile hawezi kushika nafasi, tena hata ya usheha, achia mbali ubunge, na uwakilishi,’’analalamika.

 

Anasema, wakati kampeni zake na hasa za mtaa kwa mtaa, wapo waliomkebehi kwa kumwambia, wanawake ni wa jikoni tu.

 

‘’Wingine wananiambia kwamba, ningejaribu nafasi za wanawake viti maalum, lakini sio jimbo,’’anafafanua.

 

Anachoomba ni uhai kutoka kwa Muumba, maana mapema 2030, amefika tume ya Uchaguzi, kuomba tena kuchukua fomu.

 

Tatu Abdalla Msellem wa Ole Chake chake, mwaka 2015 nae alijitupa jimboni kusaka nafasi ya uwakilishi, anasema hatosahau, dharau alizofanyiwa.

 

‘’Moja ni kufananishwa na malaya, muhuni na mtu niliyekosa kazi, lakini baya zaidi ni kwa wapiga kura, kuniomba rushwa ya ngono,’’anasema.

 

WANAWAKE WALIOWAHI KUFANIKIWA

Bahati Khamis Kombo, anaewania kwa awamu ya tatu, nafasi ya Uwakilishi Jimbo la Chambani, kwa tiketi ya CCM, anasema wanawake hakuna kurudi nyuma.

 

Anaeleza, kuwania jimbo ambalo wanaume wanadhani ni mali yao, sio kazi nyepesi, lakini umakini na ustahamilivu ndio ngao.

 

Bahati kuanzia mwaka 2015 na mwaka 2020, alifanikiwa kupenya na kuwatumikia wananchi wa Jimbo hilo, kwa heshima.

 


Na sasa anasubiri huruma za wapiga kura, kama wakiridhia wanaweza kumrejesha tena jimboni humo, kuendelea kuwa mtumishi wao.

 

Sheha wa Chumbageni Mgeni Othman Shaame na Katibu wa sheha Wawi Sham Haroub Said, wanasema hakuna kuwa laini, kwenye kuwatumia wananchi.

 

Wananchi hawaamini kuwa wanawake, wanaweza kuwa viongozi, sasa nafasi zinapopatikana, lazima umakini na uchapa kazi uwepo.

 

Mkuu wa Mkoa wa kaskazini Pemba, Salama Mbarouk, akaendelea kuwasisitiza wanawake wenye nafasi, kufanyakazi kwa bidii.

 

‘’Wanawake ambao wamo kwenye nafasi za uongozi, wafanye kazi vizuri na kwa bidi, ili jamii ione na ifahamu nguvu ya mwanamke,’’anasema.

 

WANAHARAKATI WA HAKI ZA WANAWAKE

Aliyekuwa Mratibu wa TAMWA-Pemba Fat-hya Mussa Said, anasema hoja ya mwanamke kuwa kiongozi, isiwe ajenda, maana katiba haijabagua.

 

Anawakumbusha wanaume, kuacha kuwatisha na kuwapandikiza chuki wanawake, aidha walioviongozi ama wanaogombea nafasi mbali mbali.

 

Katibu Mkuu wa Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Sifuni Ali Haji, anasema changamoto za wanawake kuziogopa nafasi za kugombea, ni mifumo dume iliyotawala.

 

‘’Inatokezea mwanamke anagombea na mwanamme, basi wanawake wenzake wanatumika vibaya, ili aachie nafasi hiyo,’’anaeleza.

 

Msaidizi wa sheria, shehia ya Wawi Fatma Hilali Salum, anasema mikataba na sheria, imeweka njia huru kwa kila mmoja kugombea, ingawa hoja ya kutojiamini na kujengwa uwelewa kwa wanawake, hutanda.

 

Mkurugenzi wa Jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Abdalla, anasema jamii isipowawapa nafasi wanawake, zipo huduma zitaendelea kudumaa.

 

WANANCHI WA KAWAIDA

Zamzam Khamis Sabour wa Kengeja, anasema mitazamo ya jamii, juu ya wanawake na uongozi, huwaweka njia panda, kuomba nafasi za uongozi.

 

‘’Sisi wanaume, inaonekana bado tumelewa na madaraka, na kumuona mwanamke kama sio sehemu ya jamii, kuleta mabadiliko,’’anasema Juma Haji Hakim wa Mtambile.

 

Aisha Hassan Juma wa Mbuyuni na mwanafunzi wa kidato cha sita skuli ya Madungu Fatma Juma Nassor, wanawake wanaweza kuleta mabadiliko, wakipewa nafasi.

 

MIKATABA/SHERIA

Sheria ya watu wenye Ulemavu nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (1) (e) chenyewe kimetamka haki ya kushiriki, katika shughuli za kijamii, ikiwemo siasa.

 

Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu mwaka 2006, Ibara ya 29 (b) (i), kwamba watu wenye ulemavu, wana haki ya kujumuishwa kisiasa.

 

Mkataba wa kimataifa wa kutokomeza aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake ‘CEDW’ wa mwaka 1979, Ibara ya 7, ukasisitiza kwamba, lazima hatua zichukuliwe, kuhakikisha wanawake wanakuwa na ushiriki sawa kwenye ulingo wa siasa.

 

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kifungu cha 21(1), kinafafanua, watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki bila ya ubaguzi, kupata haki mbele ya sheria.

 

NINI ATHARI YAKE

Haji Mohamed Omar wa Kojani, anasema kwanza ni kuporomosha huduma za wanawake na watoto katika jamii.

 

Wakili wa serikali Safia Saleh Sultan, anasema ni kudumaza demokrasia, sheria na mikataba inayozungumzia, haki za jamii.

 

NINI KIFANYIKE

Mwakilishi wa Chambani Bahati Khamis Kombo, anashauri wanawake, wapewe darsa la kuwajengea uthubutu.

 

Asha Haji Said wa Mtambile, anasema sheria zizidi kutangaazwa, juu ya uhuru na haki za wanawake, ikiwemo kugombea nafasi mbali mbali.

 


Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, anasema ni kuendelea kuwakosesha haki zao za kidemkrasia.

 

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...