Skip to main content

FARIDA: MGOMBEA UWAKILISHI JIMBO LA WAWI ANAEPANIA KUWAINUA VIJANA, WANAWAKE

 




NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

 

Farida Juma Khamis mwenye umri wa miaka 59 mkaazi wa Kichangani shehia ya Mgogoni Wilaya ya Chake Chake, ni miongoni mwa wanawake wanaosaka uongozi kwenye majimbo yao.

 

Farida ni mgombea uwakilishi Jimbo la Wawi kupitia tiketi ya chama cha Wakulima (AFP) ambae ana lengo la kushirikiana na wananchi katika kuibua changamoto ndani ya vijiji na kuzichukuwa kwa ajili ya kwenda kutatuliwa.

 

Mgombea huyo uwakilishi anasema, atakapopata nafasi ya kuliongoza Jimbo atahakikisha kila mwananchi anapata fursa ya kushiriki katika vikao vya kuibua kero zinazowakabili, ambazo atazichukuwa na kuzitetea kwenye chombo cha maamuzi.

 

Anasema, uongozi ni dhamana, hivyo akifanikiwa kuwa mwakilishi atarudi kwa wananchi ili kuwaletea maendeleo endelevu katika Jimbo.

 

Farida hakushawishiwa na yeyote kugombea nafasi hiyo, bali alipoona kwenye Jimbo kuna changamoto mbali mbali ambazo hazijafanyiwa kazi, aliona ni vyema agombee ili apate nafasi ya kuzitatua.

 

"Hao viongozi waliopita kwenye jimbo hili hawakutuletea maendeleo, hivyo kwa vile mimi ni mwanamke na ni mama, kuliona Jimbo hivi siridhiki," anasema.

 

Amepania kuliweka Jimbo hilo katika hali nzuri, kwa kuondoa matatizo yote yaliyopo na kuhakikisha analeta maendeleo.

 

Mgombea huyo anasema, hatokuwa tayari kuona elimu ya vijana wa Jimbo hilo inatumiwa kwa uhalifu, bali atawakomboa kwa kuwapatia na shughuli mbali mbali za kufanya ili wajipatie kipato.

 

Anasema, vijana wengi wanamaliza masomo yao hawana kazi ya kujipatia riziki, hivyo atahakikisha anawatafutia miradi ambayo itawawezesha kuwainua kiuchumi.

 

"Vijana hawana kazi, hivyo muda wote unawakuta maskani, hali ambayo inasababisha kujiingiza kwenye makundi ya kihalifu ikiwemo, madawa ya kulevya, wizi na hata udhalilishaji," anasema.

 

Anasema kwa vile vijana ndio nguvu kazi ya Taifa, hana budi kuekeza katika kundi hilo ili kujenga jamii iliyobora ambayo itajitekemea kiuchumi na hayo ndio maendeleo wanayoyataka.

 

Kundi la pili atakaloliangalia mgombea huyo ni wanawake, ambapo anafahamisha kuwa atahakikisha wanapata elimu itakayowasaidia kuanzisha vikundi vya ushirika, ili kujipatia kipato kitakachowasaidia na familia zao.

 

"Kuna wanawake wajane na waliotelekezwa na waume zao na wana watoto wanataka huduma, hivyo nitawahamasisha kufanya miradi mbali mbali wapate kujikomboa kiuchumi," anafafanua.

 

Anasema, Serikali inatoa mikopo kwa wajasiriamali wote na pia kuna mikopo kwa ajili ya wanawake pekee, hivyo atahakikisha wanautumia mkopo uliopo kwa ajili ya kupata mtaji kwa kuendesha shughuli zao za ujasiriamali.

 

Farida alijiunga na chama hicho tangu mwaka 2006 na ilipofika mwaka 2017 aliteuliwa kuwa Mjumbe wa Bodi kwenye chama hicho, ambapo nafasi hiyo ameshaitumia kwa miaka tisa sasa.

 

"Mwaka huu wa 2025 nimeamua kuingia jimboni kugombea nafasi ya uwakilishi na nashkuru wajumbe wamenipitisha na kwa sasa nipo kwenye kinyang'anyiro cha kulitafuta jimbo," anasema.

 

Aliwaomba wananchi wamchague ili aweze kuwatatulia changamoto zilizomo kwenye Jimbo lao ambazo zimekuwa kero kubwa la kudumaza maendeleo yao.

 

Mgombea huyo, anasema hakuhamasishwa na mtu yeyote kugombea uongozi, lakini alipoona hali ya Jimbo kimaendeleo haiko vizuri, ndipo alipoona ili alikomboe ipo haja ya kuwa kiongozi.

 

"Zamani nilikuwa na hofu kugombea lakini kwa sasa jamii imekuwa na uwelewa wa kutosha juu ya umuhimu wa mwanamke kuongoza, hivyo nimeona nitimize lengo langu," anaeleza.

 

Farida anaeleza, tangu zamani alikuwa na ujasiri wa kuongoza ingawa alikosa kujiamini kwani alihisi kama jamii haitomkubali, ingawa alipoamua kugombea wananchi wamemuunga mkono kiasi ambacho kimempa hamasa zaidi.

 

Mgombea huyo anasema, atakapofanikiwa kuwa mwakilishi atahakikisha atakeleza vyema majukumu ya nyumbani na ya kazi kwa wakati wake bila kuathiri upande wowote.

 

"Pamoja na nafasi niliyonayo kwenye chama lakini pia ni Msaidizi mwalimu Mkuu na natekeleza vyema majukumu yangu ya uongozi na ya nyumbani, hivyo hata nikipata nafasi ya uwakilishi nawaahidi wananchi kuwa nitatekeleza vizuri," anafahamisha.

 

Anataja changamoto iliyomkwaza kuwa ni kukosa ruzuku ya kufanyia mikutano ya kampeni, hali ambayo ilikaribia kumkatisha tamaa.

 

"Kwa vile ilikuwa nimeshatia nia ya kugombea, nilisema nitahakikisha natumia nguvu yangu ya kifedha kufanya mikutano, ili kuwaomba wananchi kura za ndio," anafafanua.

 

Mume wa mgombea huyo ambae pia ni Mgombea Urais kupitia chama hicho, Said Soud Said anasema, mke wake wanampa ushirikiano katika familia yao na ndio maana amejiamini kuingia jimboni kugombea.

 

Anasema, pia wananchi wa Jimbo lao wanampa ushirikiano kwani wametambua kwamba mwanamke ni mlezi na ana imani, hivyo wamemuahidi kumchagua ili awatatulie matatizo yao.

 

"Naamini kwamba wananchi wa Jimbo hili watamchagua kwa sababu ni mwanamke jasiri, anaejiamini na ana uwezo wa kuongoza," anasema.

 

Alimshauri mgombea huyo, atakapopata ridhaa ya kuongoza Jimbo, ahakikishe anarudi kwa wananchi kusikiliza kero zao na kuzitatua kwa wakati, kwani wataendelea kujenga imani kwake na kuendelea kumchagua kwenye miaka mengine ijayo.

 

Mgombea huyo urais pia aliwaomba wananchi wamchague mgombea huyo uwakilishi, ili wapate maendeleo ya uhakika katika Jimbo lao.

 

Mama huyo ameolewa na ana watoto nane, ambapo ana elimu ya cheti katika fani ya uwalimu aliyoipata katika chuo cha Nkuruma mwaka 1987.

 

Amina Ahmed Mohamed ambae ni Kaimu Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake kwa upande wa Pemba, anasema TAMWA imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi ili waondokane na mawazo mgando kwamba mwanamke hawezi kuongoza na ndio maana mwaka huu wamegombea wengi.

 

"Jamii sasa imepata uwelewa na wamejua umuhimu wa mwanamke kuongoza kwa sababu waliokaa majimboni wote wamefanya vizuri na maendeleo yanaonekana," anaeleza.

 

Kaimu huyo anasema, pia wanawajengea uwezo wanawake wenye nia ya kugombea uongozi ili wajiamini, wawe na ujasiri pamoja na kutekeleza yale ambayo wanayaahidi kwa ajili ya kujenga Taifa lenye maendeleo.

 

Mgombea huyo ametekekeza haki yake ya kushiriki katika demokrasia na uongozi, kama Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1964 ilivyoeleza kwenye kifungu cha 21 (2) na kifungu cha 67 (1) cha Katiba hiyo kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2010.

 

                                              MWISHO.

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...