Skip to main content

HAYA HAPA MATUNDA MRADI WA ‘SWIL’, WANAWAKE WAONEKANA SAFU YA UONGOZI, WENYEWE WASEMA BADO KIDOGO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

SIKU hizi imekua tofauti na zamani, wanawake kuwa viongozi sio jambo geni kujitokeza kugombea nafasi hizo na kushinda.


Nchi kadhaa, hivi sasa zimeendelea kutokana na wanawake kupewa nafasi za uongozi na kufanikiwa kuleta mabadiliko ya kiutendaji.
 
Mataifa kama ya Ethiopia, Liberia pamoja na Tanzania, ambazo uchumi wake umepanda na kupata mabadiliko makubwa katika sekta tofauti.



Ellen Johnson-Sirleaf ni Rais wa kwanza mwanamke barani Afrika, hata hivyo yeye sio mwanamke wa kwanza kuongoza nchi barani Afrika.

Maana yupo Malikia Zauditu wa Ethiopia alieongoza nchi yake kwa miaka 13 toka mwaka 1917 hadi 1930. 

Katika miaka michache iliopita, Tanzania imepata mafanikio  makubwa, ikiwa pamoja na utulivu wa kisiasa na maendeleo katika sekta mbali mbali kufuatia uongozi wa nchi kushikwa na Rais wa kwanza mwanamke, Dk. Samia Suluhu Hassan.
 
Mama Samia hivi sasa anahesabika kuwa ni mfano mzuri wa kuigwa na wanawake wa hapa nyumbani na nchi nyingine.



Mifano mingine ya wanawake wanaofanya vizuri kweye nafasi za uongozi ni balozi Amina Salum Ali ambae ni Waziri wa Fedha, Anna Makinda aliyekuwa Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kawaida familia nyingi humlea mtoto wa kike kwenye utamaduni na mifumo isiyowaweka tayari kuingia katika uongozi na humuwekea mazingira ya mtumishi wa kazi za ndani kitu kinachojenga taswira mbaya katika makuzi ya watoto.

Licha ya vikwazo na changamoto mbali mbali wanazopitia watoto na vijana wakike, bado uwezo wao wa kuongoza ni mkubwa, na hili linadhirika mara tu anapopewa nafasi.

 
Tukumbuke kuwa Idadi ya vijana wenye umri wa miaka 15 hadi 35 imefikia, 699,845, wanawake 368,066 na wanaume 331,779, ni wazi kuwa vijana wakike ni wengi kuliko wakiume.

Aidha idadi ya vijana kuanzia umri wa miaka 15 hadi 24, imefikia 384,647 wanawake ni 202,067 huku wanaume ni 182, 580.

Sham Haroub Said, Katibu wa sheha Wawi, anasema anasema wanawake wana mchango mkubwa katika jamii na familia zao licha ya changamoto za kifamilia kuwarudisha nyuma.

Kawaida familia nyingi humlea mtoto wa kike kwenye utamaduni na mifumo isiyowaweka tayari kuingia katika uongozi, badala yake humfanya kama mtumishi wa kazi za ndani na mtoto wa kiume kama muangalizi wa familia.


Takwimu za Sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022, wanawake ni wengi zaidi kwa asilimia 51.6 dhidi ya wanaume ambao ni asilimia 48.4 huku Zanzibar ina idadi ya watu 1889, 773 kati yao wanawake 974,281 na wanaume ni 915,492.

Mwakilishi wa Jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo, anatarajia kuwaona wanawake, sasa wakiwa mbele katika nafasi ya uongozi, hasa baada ya mazingira kuwa rafiki.



Anasema hata serikali ya awamu ya nane, imekuja kuwapa heshima yao wanawake katika safu ya uongozi, kwa kuwepo wakuu wa mikoa wawili wanawake, kati ya watano.

Mkuu wa Mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbaruk Khatib, anasema uwezo wa wanawake katika uongozi, sasa unaonekana maana Dk. Mwinyi amewaanini mno kwa utendaji wao wa kazi.

‘’Kwa mfano nafasi ya Katibu Mkuu Kiongozi na katibu wa Baraza ka Mapinduzi Mhandisi Zena Ahmed Said, amekuwa wa kwanza tokea Zanzibar ijitawale mwaka 1964,’’anasema.

Eneo jingine anasema, ni kuwapo wa wakuu wa wilaya wawili kati ya wilaya nne za Pemba, jambo ambalo halijwahi kutokezea kwa historia ya mwanamke na uongozi.

JAMII

Ali Salim Hamad wa Mchanga mdogo, anasema, ile dhana ya 50 kwa 50 kwa wanawake katika ngazi ya maamuzi, imeanza kunukia mno, maana wapo hata masheha wanawake. 

Omar Haji Hasnuu wa Wawi, anasema Katibu wa sheha ni mwanamke anaefanyakazi kwa bidii na kumsaidia kwa kiasi kikubwa sheha wao. 

Maryam Hassan Kombo wa Mizingani Mkoani, anasema kasi ya Dk. Mwinyi inayochagizwa na wanaharakati kama TAMWA, imeonesha uhodari wa utendaji kazi wa wanawake.

 

‘’Kwa mfano Mkuu wetu wa wilaya ya Mkoani ni mwanamke, lakini tunaoona anavyoendesha wilaya, kw ahakika kweli wanawake wanaweza,’’anasifia.

 


Hidaya Mjaka Ali mwenye ulemavu wa viungo anaeishi Vitongoji wilaya ya Chake chake, anakiri kuwa sasa juhudi za wanawake katika safu ya uongozi inaonekana kwa ufanisi.

 

‘’Ukitaja Tanzania rais wetu ni mwanamke, ukienda wilaya ya Chake chake, mkoa wa kaskazini Pemba na hata Katibu mkuu kiongozi na Katibu wa baraza la Mapinduzi, nae ni mwanamke,’’anasema.

 

YALIKUJAJE HAYA
 Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wa habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, anasema zipo juhudi kadhaa wao walizozifanyia kuanzia zaidi ya miaka 25 iliyopita.

 


Anasema, katika siku za hivi karibuni, walikuwa wanaendesha mradi wa  kuinua wanawake na uongozi na demokrasia SWIL, ambao unalenga kuwaonesha haki za uongozi na nafasi yao katika jamii.

Dk. Mzuri anakiri kuwa, kwa muda mrefu, wanawake wamekua na nafasi ndogo katika nafasi za uongozi na ngazi za maamuzi, na ndio maana waliamua kuwajengea uwezo na kuwashajiisha watumie fursa ziliopo za kugombea.
 
Anasema, tathmini inaonesha idadi ya wanawake nchini, inaendelea kuongezeka za uongozi kutokana na elimu inayotolewa katika jamii na utayari wa mtoto wa kike mwenyewe, kujitokeza mbele na kuongoza.
 
Akizungumza katika moja ya mafunzo ya kuwajengea uwezo vijana wa kike kwa lengo la kuisaidia jamii, aliwahi kusema kuwa, wameamua kuwakutanisha vijana wakike wenye vipaji tofauti na uthubutu, ili kusaidia wanawake na jamii kiujumla.

 

Alisema dunia imeamini kuwa wanawake wana uwezo katika nafasi za uongozi kama anavyoweza kulea familia, vijana wa kike wakikaa pamoja na kupeana mawazo na kufanya maamuzi ya kusaidia jamii kufika sehemu nzuri.

Alitumia nafasi hiyo kuwataka vijana wakike kuitumia vizuri nafasi hiyo, kwa kuendeleza vipaji na kuiga mfano kutoka kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan.

Akitolea mfano alipokua kijana, Dk. Mzuri alisema alipata nafasi ya kuajiriwa serikalini lakini hakuona kama nafasi nzuri kwake ya kuitetea jamii hasa wanawake, hivyo aliamua kujiunga na taasisi binafsi kwa lengo la kuisaidia wanawake kwenye nafasi za siasa, uchumi wa masoko na uongozi.

"Mfano sheria iliyotumika ya 1985, zilimkandamiza mtoto wa kike  na kulazimika, wanaopata ujauzito kufungwa, kupitia nafasi hiyo walifanikiawa kufanya utetezi kwa sheria zenye madhara na mifumo dume zilizowakandamiza wanawake zifutaw,"alisema.

Kwa mwaka 2020, wanaume waliojitokeza kugombea uwakilishi Zanzibar 190, walioshinda 42 na wanawake 61 na waliobahatika kushinda ni wanane (8) tu.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa kutambua umuhimu wa wanawake na kuwaaamini kwenye uongozi, amewapa nafasi mbalimbali ikiwemo nafasi za mawaziri, makatibu wakuu.

Dira ya mpango wa Maendeleo ya Zanzibar yamwaka 2020 hadi 2050 imeelezea kuboresha mfumo wa kisisa, kupitia taasisi mbalimbali katika masuala ya uongozi.

Kwa mijibu wa makubaliano ya Maputo Protocol yaliyofanyika Julai 11, 2003 nchini Msumbiji, kipengele namba 9 imeonesha haki ya wanawake kushiriki katika siasa na mchakato wakushiriki katika vyombo vya kutoa maamuzi.

SWIL

Utekelezaji wa mradi huo ambao ulitarajiwa kuwafikia na kuwawezesha wanawake 6,000 kwa Unguja na Pemba, katika kudai haki zao ili nao waweze kuwawezesha wengine, tayari umeonyesha njia katika kufikia hatua ya kudai haki zao za uongozi.

 Mradi huo wa SWIL ambao unafadhiliwa na ubalozi wa Norway umetekelezwa maeneo mbalimbali ambapo kwa upande wa  Pemba tayari   umeshawafikia wastani wa wanawake zaidi ya 4,000.

 Kamati hizo zinajulikana kwa jina la kiutaalamu 'citizen brigged' asilimia 60 ni wanawake na 40 ni wanaume ambao ndio walengwa wakuu wa kutowa ushirikiano kufikia malengo ya mradi huo.

Mkurugenzi Mtendaji wa mradi wa ‘SWIL’ kutoka PEGAO Hafidh Abdi Said, anasema kwa wilaya za Pemba, mradi umevuuka lengo kwani wameshajengewa uwezo zaidi ya watu waliokusudiwa.

 Anasema uhamasishaji huo haukulenga kuwajengea uwezo wanawake hao kuwa viongozi serikalini, wala vyama vya siasa pekee bali hadi ndani ya sekta iliyomo ndani ya jamii.

Aliyekuwa Mratibu wa mradi huo kutoka TAMWA Pemba, Fat-hiya Mussa Said, anasema tayari mradi umefikia hatuwa ya lengo lililokusudiwa, ambapo ndio tarajio lake kwani mradi huu unawawezesha  wanawake na jamii.

 Anaeleza kuwa utekelezaji wao mkubwa ndani ya mradi huo, kuwawezsha  waandishi wa habari,  ili wapate uweledi wa masuala ya wanawake na uongozi.

 “Tunaamini kama tukiwawezesha vizuri waandishi  wa habari watakuwa na maono mapana na kuondokana na dhana zilizo ndani ya jamii, juu ya wanawake na uongozi.

  WAHAMASISHAJI JAMII KUPITIA MRADI

 Nachia Khamis Mohamed wilaya ya Mkoani anasema katika kutembelea vijijini, wamebaini changamoto mbalimbali zinazosababisha wanawake wasifikie malengo ya kuwa viongozi, ikiwemo uwelewa hafifu.

Anasema wamebaini wanawake wengi wanakuwa na lengo la kugombea nafasi za uongozi, ingawa wanakwazwa ikiwemo ndoa kwani hupambana na wivu kwa wanaume zao.

Ali Abdalla Juma  wa Chake chake anasema kutokujiamini, jamii kuwa na uwelewa mdogo, unaohusiana na wanawake na uongozi ni eneo jingine la changamoto.

 WANAHARAKATI

 Khadij Henock Maziku, anasema hata nafasi za usheha, udiwani na nyingine katika jumuiya mbalimbali, zinaonekana kukamatwa na wanawake, jambo ambalo hapo zamani halikuwepo.

 Uthibitisho wa hilo ni pale tunapoona kuongezeka idadi ya masheha katika wilaya zilizopo kisiwa cha Pemba, kwa upande wa wilaya ya wete inayo masheha wanawake 14 kati ya shehia 36 jambo ambalo hapo nyuma hawakuwepo.

Sifuni Ali Haji anasema, lazima wenye mamlaka waone aibu pale wanapowaacha wanawake katika nafasi za uongozi, kwa vile wanapopewa nafasi hizo, hufanya vizuri.

  VIONGOZI WA DINI

Sheikh Said Ahmad Mohamed kutoka ofisi ya Mufti, anasema mwanamke hajakatazwa kuwa kiongozi na hasa, akiwa atazingatia maadili, mila na desturi za dini na jamii yake.

Father Zeno Marandu wa Kanisa Katoliki Chake chake, anasema hajakatazwa mwanamke kuongoza, kwani anasema hakuna kondoo mwanamke kuchungwa na mwanamme, hivyo lazima na wanawake nao wafike kwenye zizi, ili kuwaangalia .

                                  MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...