Skip to main content

MADC: WANAWAKE PEMBA, WAWAONESHA NJIA WANAWAKE NAMNA YA KUONGOZA

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

‘’HESHIMA, bidii ya kazi, upole, ustahamilivu na kufanya uamuzi sahihi, ndio njia moja wapo za kuwatumikia watu,’’anasema Mkuu wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki.

Anasema inawezekana waliowengi, wandhani ili uwe kiongozi mzuri, lazima uchupe mipaka, kimavazi, heshima, uondoe upole, ukiuke sheria, jambo ambalo ni tofauti.

Anahadithia wakati wakiwa mtendaji wa Tume ya Uchaguzi, miaka 15 iliyopita, alichunga sana nidhamu na heshima yake, huku akihakikisha halazi kazi.

Alizingatia mno kivazi cha heshima, kujenga mapenzi ya kazi kwa kila mmoja, na kuhakikisha kitengo chake hakifeli kwa jukumu, walilopewa.

''Kuna wakai tunasafirisha vifaa tena siku ya mvua, ilipofika majira ya saa 5:50 usiku, wapo walionitaka nirudi nyumbani kumpunzika na wao wataendelea na kazi, niligoma,''anakumbushia.

Aliwaambia kama ni wakati wa kazi wanafanya kwa pamoja na wakati wa kumpunzika, wanapumzika kwa pamoja, maana kazi ndio kazi.

‘’Siku hiyo kila mmoja aliniona kama sio mwanamke wa kawaida, maana nilichapa kazi, hadi tunamaliza zoezi la usambaazaji vifaa ni saa 12: 00 alfajiri, nimeroa chapa,’’anasema.

Mkuu huyo wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, anasema utii wa kazi kwa mwanamke, ni njia sahihi na kulinda heshima na nidhamu yake na kwa wingine.

Anakiri kuwa, hakuna uhusiano wowote wa mwanamke kuwa kiongozi na kuvunja mipaka, maadili na heshima yake, na ikiwa wako wanaofanya hivyo, ni mwenendo na malezi yao ya asili.

Akawataka wanawake wanaosaka uongozi, kwanza kuondoa hofu kwamba kwa sababu ya jinsia yao, ikiwa wanaweza kutekeleza majukumu ya umma.


'’Utumishi wa umma, tayari miongozo, sheria na kanuni zimeshawekwa, unapofika kwenye nafasi ya uongozi, iwe usheha, ukuu wa wikaya, Katibu mkuu na hata Waziri, ni kuifuata tu,’’anasema.

Kumbe anaona  hakuna tofauti ya kutisha kati ya mwanamke na mwanamme, kwenye utekelezaji wa majukumu, na hasa ikiwa mwanamke huyo, anataka kweli kuwatumikia watu.

Anakumbuka akiwa Katibu Tawala wilaya ya Mkoani, aliwasaidia sana wakuu wake wa wilaya, akiamini wakiharibu wao, ndio ameharibu yeye.

Siri nyingine ambayo anasema waliowingi hawaifahamu, wanadhani anapoharibu mkuu wake wa kazi, kama vile muhudumu ama dereva hahusiki, jambo ambalo sio sahihi.

‘’Niwatake wanawake ambao wanahudumu kwenye nafasi mbali mbali au wanaowania nafasi, kufanyakazi kwa bidii na wawe na bango, hakuna kushindwa,’’anasema.

Mkuu wa wilaya ya Chake chake Mgeni Khatib Yahya, ambae alihamishiwa wilaya hiyo akitokea wilaya ya Micheweni, anasema hakuna kazi kwenye kuongoza.

Akawaelekeza wanawake wenzake, kuzingatia mambo makubwa matano, ambayo hayo akifanikiwa anaweza kuongoza hata taifa, sembuse shehia ama mkoa.

Moja, ni huruma kwa unaowaongoza, ili kuhakikisha majukumu ya kazi yanakamilika, ni kuweka kando uongozi wa maguvu na vitisho.

Jingine ni kufuata maadili na kujenga heshima kwa kila mtumishi, jambo ambalo litakupa marafiki kuanzia muhudumu, mtunza fedha hadi dereva.

‘’Jingine Mkuu huyo wa wilaya, analoliona linafaa kwa wanawake kulifuata ni kujua walau kidogo kanuni, sheria na miongozo ya utumishi, ili uwe mtatuzi mzuri wa migogoro,’’anasema.

Akawakumbusha wanawake wanaowani uongozi kuwa, jambo jingine na muhimu la kuzingatia, ni kuwajua watu tabia zao, kuanzia mkuu wako wa kazi hadi unaowaongoza.

Kujiamini kunakofuatana na kupenda ushauri, ni eneo jingine ambalo kiongozi mwanamke, anatakiwa kuwa nalo hilo na kujiondoa kwenye safu kuwa anajua kila kitu.

‘’Tena hili, wapo wengi wanaolipuuza na wakati mwingine hata kupekelekea kuzikosa nafasi, iwe za uteuzi ama za kupigiwa kura,’’anawakumbusha.

Dc Mgeni, anawakumbusha wanawake, kuwa wasiwe na woga wa kuzitafuta nafasi, maana hakuna katiba, sheria, miongozo wala kanuni, iliyomzuia mwanamke.

‘’Mimi mwenyewe nilianzia ngazi ya shehia, jimbo na kisha nikabahatika kuwaongoza wananchi kuanzia wilaya za Wete, Micheweni na sasa nipo Chake chake,’’anasema.

Nilipomuliza anaona wanawake waliowengi wanakwama wapi, kwenye safu ya uongozi, anasema kwanza shida inanzia kwa jamii, bado haijawaamini sana wanawake.

Anasema, wanahofu kuwa, kila kiongozi mwanamke kama vile ni mvunja maadili au anaeipa kisogo familia yake, jambo ambalo sio sahihi.


‘’Na kwanza Tanzania kumpata Rais mama Samia, kwangu amekuwa ni muongozo wa utendaji kazi, pamoja na namna anavyoshughulikia shida za wananchi, bila ya ubaguzi,’’anasema.

Ndio maana akawataka wanawake wenzake, kuiba nyenendo, tabia, hulka, misimamo na kuchangamana na watumishi, kama anavyofanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Saluhu Hassan.

KIPI WANAWAKE WANAOTAKA UONGOZI WAKIEPUKE?

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki na mwenzake wa Chake chake Mgeni Khatib Yahya, wanasema ni matumizi mabaya ya ofisi.

Wakifafanua kuwa, wapo baadhi wanapopata nafasi, mfano usheha huanza kunuka na kutoa harufu za tabia mbaya, kwa matumizi mabaya ya cheo.

Jingine wanawashauri wanawake, wasiache kuzishughulikia familia, maana wajibu huo, hauondoki maana ni kutoka kwa Muumba.

Eneo jingine, ni kutoacha kuzibebe shida za wananchi kama zao binafsi, na kuhakikishi hawalali, hawali, hawanywi ikiwa ufumbuzi haujapatika.

WANAHARAKATI WANASEMAJE?

Dk. Mzuri Issa Ali, ni Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, anasema ujasiri wa mwanamke kiongozi, huanzia kwenye utekelezaji wa majukumu yake.

‘’Tunapotaka wanawake waingie kwenye safu ya uongozi, ni kuwataka kuwatumikia wananchi na sio jambo jingine lolote,’’anasema.



Katibu Mkuu wa Mwenvuli wa asasi za Kiaria Pemba ‘PACSO’ Sifuni Ali Haji, anasema vikwazo vilivyopo kwa wanawake wanaowania uongozi, wa kuviondoa ni wanawake wenyewe.

‘’Njia moja ni kuvunja ukimya, wanapoona nafasi zao zinachukuliwa ni kusema, kugombea, kurekebisha ama kukataa,’’anaeleza.



Mohamed Hassan Abdalla Msaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake, anasema miongozo ya kisheria, ipo wazi juu ya kila mmoja kuomba nafasi.

Anasema, wanawake waendelee kujengewe uwezo, maana kwa karne moja iliyopita, waliachwa nyuma na kuonenakana kama bihdaa ya kukaa ndani, jambo ambalo sio sahihi.



MIONGOZO INASEMAJE

Katiba ya Zanzibar ya 1984, kwenye kifungu cha 11 na cha 14, vimeweka wazi kuwa kila mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomuhusu.

 

Dira ya Zanzibar ya 2050 imeelezea jinsi gani masuala ya usawa wa jinsia, juu ya kuondoa unyanyasaji na kuimarisha mifumo ya uwezeshaji wanawake.

 

Sera ya jinsia inaeleza ushiriki wa wanawake katika vyombo vya utoaji maamuzi, katika ngazi zote ni mdogo na kwa hivyo serikali, kwa kushirikiana na wadau wingine, itafanya juhudi kuona makundi yote na yaliyopembezoni.

 

Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), ambayo mkataba wake ulitiwa saini mwaka 2008 inaeleza, kutaka kuondoa utafauti na kuwatenga wanawake katika nyanja mbalimbali za maendeleo.

 

Makubaliano yanayojulikana kama ‘Itifaki ya Maputo’ ambayo yalifanyika Msumbiji mwaka 2003, inacho kipengele kinachoonyesha haki ya wanawake, ikiwemo kushiriki katika siasa na vyombo vya kutoa maamuzi.

 

Mkataba wa kimataifa wa kutokomeza aina zote za ubaguzi, (CEDAW) wa mwaka 1979 ambao unapinga aina zote za udhalilishaji na kusisitiza, ushiriki wa wanawake katika uongozi.

 

Mpango wa Utekelezaji wa Beijing mwaka 1995, ibara ya 7 inataka ushiriki katika vyombo vya maamuzi kwa kuzingatia uwiano wa kijinsia kwenye ngazi zote za uongozi.

 

NINI ATHARI YAKE

Hidaya Mjaka Ali mwenye ulemavu wa viungo, anasema ni kuendelea kukukosa huduma stahiki, kama za afya ya uzazi, kwa kule kukosa mtetezi wa moja kwa moja.

Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, anasema ni kuendelea kudhalilishwa kidemokrasia na kiuongozi,’’anasema.

NINI KIFANYIKE

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, anasema kwa nafasi ambazo ni za uteuzi wanawake, waendelee kuaminiwa na za kura wapigiwe.

Haji Kassim Haji wa Mchanga mdogo, anasema wakati umefika kwa wanaume, kuwakatia minyororo ya utumwa wanawake, na sasa kuwapa haki zao, ikiwemo ya uongozi.

Mwanafunzi wa kidato cha sita skuli ya Madungu Hafsa Issa Khamis, anasema elimu ya uongozi, ianzie ngazi ya elimu ya maandalizi, ili kuwajengea uthubutu mapema.

Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, kwenye sherehe za kutimiza miaka mwili ya uongozi wake, zilizofanyika Wete, aliahidi kuwapa nafasi zaidi wake.

         mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...