Skip to main content

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA PANDANI AAHIDI KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO

 


NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

WAKATI nchi ikielekea kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka huu, wanawake wengi wamejitupa majimboni kwenye kinyang'anyiro cha kugombea uongozi.

Mwaka huu wa 2025 wanaonekana wanawake wengi wakinadi sera zao kwenye mikutano ya kampeni na wengine wakipita nyumba kwa nyumba kutafuta kura ambazo zitamuwezesha kuibuka mshindi kwenye Jimbo lake.

Kuna wanaogombea ubunge, uwakilishi na udiwani, hivyo kila Jimbo unalopita kuna wagombea wanawake wanaosaka kura kwa kishindo.

Hii ni kutokana na kwamba elimu inayotolewa sasa imezaa matunda, kwani wanasimama imara tena bila woga kuomba kura ili kuhakikisha wanaingia kwenye vyombo vya maamuzi kwa ajili ya kuleta maendeleo kwenye majimbo yao.

Mkasi Ali Hamad mwenye umri wa miaka 35 ni mmoja kati ya wanawake waliojitupa majimboni kuwania nafasi za uongozi, ambapo yeye anatafuta nafasi ya ubunge Jimbo la Pandani kupitia ticket ya chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA).

Mkasi ni mwanamke mpambanaji mwenye lengo la kutatua shida za wananchi kwenye Jimbo lake ili kupata maendeleo endelevu.

Anasema, ni miaka mingi sasa imepita ingawa wabunge waliokuwepo hawakufanya chochote kwenye Jimbo lao, hali ambayo ilimfanya achukue fomu haraka ili awatatulie wananchi kero zilizopo.

Mgombea huyo anasema, iwapo atafanikiwa kupata nafasi hiyo ya ubunge atawasaidia wananchi mmoja mmoja, familia na kutatua changamoto zilizomo kwenye vijiji vya Jimbo lao.

"Zinapotokea shughuli za kijamii kama vile msiba na harusi basi nitoa mchango kwani familia zetu nyingi ni masikini, hivyo nitawasaidia ili ziwawezeshe," anaeleza mgombea huyo.

Mkasi anasema, atawaweka watu maalumu ambao wataibua changamoto zote za Jimbo ambao watashirikiana bega kwa bega na wananchi, hiyo itasaidia kupata changamoto zote na kuweza kuzifanyia kazi.

"Hata wakati nitakapokuwepo bungeni basi shughuli za kuibua kero zitaendelea na watanifikishia ili nipate kuzitetea na nikija mwenyewe tutashirikiana kuziibua, lengo ni kupata maendeleo ya haraka," anaeleza.

Anaeleza kuwa, wananchi watarajie mazuri kwani atahakikisha anafikisha maendeleo kila sekta, ili wananchi wajisikie kwamba wamepata mtetezi wa Jimbo lao.

Anawaomba wananchi wa Jimbo la Pandani wamuunge mkono na wamchague, kwani amepania kuwatatulia changamoto zilizomo kwenye Jimbo na kuwafikishia maendeleo.

"Tumeona hapa miaka mingi imepita lakini tukiwa na tatizo hata tuwaite mwakilishi na mbunge basi wanatupuuza na hawatekelezi, wala hawapokei hata simu zetu, hivyo nichagueni mimi mupate maendeleo," anasema.

Mgombea huyo anasema, kwa upande wa wananchi hajapata changamoto yeyote, ambapo wanamuunga mkono na kumtaka asimame imara kulitetea Jimbo.

Anafafanua kuwa, changamoto iliyomkwaza ni kukosa ruzuku, hali iliyomsababisha afanye kampeni ya nyumba kwa nyumba.

"Nimefanya kampeni ya nyumba kwa nyumba, ingawa ni ngumu sana lakini kwa vile nimedhamiria nikasema ni mwiko kukata tamaa," anaeleza dada huyo.

Mgombea huyo hakushawishiwa kugombea nafasi ya ubunge, ingawa alipoona viongozi wa Jimbo waliokuwepo hawakufanya kitu, ndipo alipoamua kuingia ulingoni kwenye kinyang'anyiro cha kugombea.

Safari yake ya uongozi mgombea huyo ilianza pale tu alipojiunga na chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mwaka 2010 na kubahatika kuwa Mwenyekiti wa akinamama Jimbo la Pandani na baadae kuwa Mwenyekiti wa akinamama Wilaya ya Wete, nafasi ambazo aligombea na kuibuka mshindi.

Anasema, baada ya kuona Chadema hakikushiriki kwenye uchaguzi ndipo alipoona aingie kwenye chama cha CHAUMA, ili aweze kutelekeza lengo lake alilojiwekea.

"Nimeshazoea harakati za huku na kule, hivyo sikuweza kustahamili, nikaona nijiunge na CHAUMA nipate kuwaletea maendeleo wananchi wa Jimbo langu," anasema.

Anahadithia, baada ya kujiunga na CHAUMA, alipata nafasi ya Mwenyekiti wa Jimbo la Pandani, ambapo anaendelea na nafasi hiyo.

Mume wa mgombea huyo, Omar Khamis Mohamed anasema, katika familia wanamuunga mkono mgombea huyo ili atekeleze majukumu yake vizuri.

Anasema, anaamini kuwa Jimbo hilo atalitumikia vizuri iwapo wananchi watamchagua, kwani ameshaona kasoro za viongozi wa Jimbo waliopita kwamba, hawakutekeleza ahadi zao walizoziweka.

"Tunamuumga mkono na tunaamini kwamba yeye atakuwa tofauti na waliopita na hasa kwa vile ameshaona ile kasoro yao, mgombea huyu ni mkakamavu na anaweza kuleta maendeleo ya haraka," anasema.

Alimtaka atekeleze ahadi ipasavyo iwapo atabahatika kuibuka mshindi wa nafasi hiyo, kwani atakapogeuka itakuwa amefanya vibaya na hatokuwa mfano mzuri kwa jamii.

Naibu Katibu Mkuu wa CHAUMA Zanzibar Mohamed Massoud Rashid anasema, mara hii wamewaingiza wanawake wengi kwenye mchakato wa kugombea uongozi Zanzibar na Tanzania Bara, kwani wanaamini watafanya vizuri kwenye majimbo yao na kutekeleza vyema ilani ya chama chao.

Anasema, atakapopata nafasi kuingia kwenye uongozi akasimamie maamuzi ya viongozi wao pamoja na kutekeleza masuala mbali mbali ya kimaendeleo kwenye sekta zote.

"Watakapofanikiwa kuwa viongozi, tunawataka warudi majimboni kwa wananchi waliowachagua na kuchukua kero zao kwa ajili ya kuzifikisha kwenye vyombo vya maamuzi," anaeleza.

Mgombea huyo ameolewa na ana watoto sita, ambapo ana elimu ya kidato cha tatu aliyoipata katika skuli ya Pandani Wilaya ya Wete.

                             MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...