Skip to main content

UKOSEFU WA RUZUKU KWA BAADHI YA WAGOMBEA ULIVYOSABABISHA KAMPENI YA NYUMBA KWA NYUMBA

 

 

NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ 


WAGOMBEA kisiwani Pemba wamesema, changamoto yao kubwa inayowakumba katika kipindi hiki cha kutangaza sera zao ni ukosefu wa ruzuku ambayo inasababisha kutokufanya mikutano ya kampeni ambayo wamepangiwa kuifanya.


Walisema, mikutano ya kampeni ndio inayowatangaza kuwa wao ni wagombea, kwani hunadi sera zao ambazo ndizo zinazowafanya wananchi kuwachagua, hivyo kukosa ruzuku imesababisha wafanye kampeni nyumba kwa nyumba, jambo ambalo ni vigumu kuzimaliza nyumba zote kwenye Jimbo.


Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, wagombea hao wanasema, ruzuku ni muhimu kwao katika kuendesha mikutano yao ya kampeni ambayo wanajitangaza kwa lengo la kupata nafasi ya kuwa kunadi.


Mgombea uwakilishi Jimbo la Wawi kupitia chama cha Wakulima AFP, Farida Juma Khamis alisema, ukosefu ruzuku ni changamoto kubwa iliyomkabili, ambayo inaweza kurudisha nyuma lengo lake.


"Kwa vile nilikuwa na nia niliongozana na mgombea urais kila anapokwenda, hivyo ilikuwa nanadi sera zangu na nashkuru nimekosa mkutano mmoja tu kati ya niliyopangiwa kuifanya," alieleza mgombea huyo.


Kwa upande wake mgombea uwakilishi Jimbo la Kojani kupitia chama cha ADA TADEA Maryam Msanif Ali alisema, amelazimika kufanya kampeni ya nyumba kwa nyumba ili kuomba kura kwa wananchi.


"Nilisema hata ikiwa sina pesa basi, nipite kwa wananchi wa Jimbo langu, iliningharimu lakini nilisema kwa vile natafuta basi ni mwiko kukata tamaa," alifafanua Maryam.


Nae mgombea ubunge Jimbo la Pandani kupitia chama cha Chauma, Mkasi Ali Hamad alisema ametumia nguvu zake mwenyewe kuhakikisha anafanikiwa kuingia bungeni kwa ajili ya kutatua changamoto za Jimbo lake.


"Ingawa ni shida kumaliza nyumba zote lakini kwa jitihada zangu nimezimaliza na nina matumaini nitashinda nafasi ya ubunge, nawaomba wananchi wazidishe imani kwangu," alisema.


Mwenyekiti wa ADA TADEA Wilaya ya Wete Mohamed Khamis Hamad alisema, ukosefu wa ruzuku unawakazwa sana wagombea, jambo ambalo linaweza kuwafelisha.


"Hii hali inaumiza sana wagombea, kwa sababu tumefanya mkutano mmoja tu wa kuwanadi wagombea ubunge, uwakilishi na udiwani, hivyo wamelazimika kufanya kampeni ya nyumba kwa nyumba na sihaba tumefanikiwa kumaliza nyumba zote," alifahamisha.


Salma Khamis Tumu mgombea uwakilishi Jimbo la Tumbe kupitia chama cha Mapinduzi CCM amekishikuru sana chama chake kwa kumpatia fedha ambazo zimemsaidia kufanya mikutano yake ya kampeni na shughuli nyengine zinazohusiana na uchaguzi.


"Ingawa tulichelewa kupata fedha lakini hapo tulipoingiziwa tuliendelea kufanya kampeni vizuri na nashkuru zimeniwezesha sana, hivyo nawaomba wananchi wanichague ili niwaletee maendeleo katika Jimbo letu," alisema mgombea huyo.


Mkurugenzi wa chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Zanzibar, Dk. Mzuri Issa alieleza kuwa, wanawake ni kundi maalumu ambalo kwa miaka mingi limeachwa nyuma, ambapo walivishauri vyama vyote viwe na sera ya kijinsia ambayo wataitekeleza ipasavyo na sio kuwepo tu.


"Moja kati ya jambo muhimu ni kuwatambua wanawake ambao wanahitaji uongozi na kuwapa hizo nafasi na jengine ni kuwapa mashirikiano ya hali na mali, ili kuweza kutekeleza mambo ya ya uongozi vizuri," anafafanua.


Dk. Mzuri alisema, ikiwa wagombea hao hawakupata ruzuku hiyo ni bahati mbaya sana na ni mapungufu makubwa kwa vyama vya siasa, kwani walivishauri mwanzo kwa vile vyama vinavyopata ruzuku viweke fungu maalumu na ambavyo havipati vijue kwamba hilo jambo lipo na vianze kutafuta fedha mapema kuhakikisha wanawake hawapati shida kutokana na fedha.


Msajili Msaidizi vyama vya siasa Sisty Nyahoza alisema, chama chenye usajili kamili kina haki ya kupata ruzuku endapo kina mbunge au diwani wa kuchaguliwa na kimetimiza masharti ya kupata ruzuku, yaliyopo katika sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2024.


"Mfano kuwa na akaunti ya benki (kifungu cha 15(2), hesabu zake kukaguliwa na CAG (kifungu cha 14 (1) (b) (i) ) na kutumia fedha za ruzuku kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa inavyoelekeza (kifungu cha 18)," anaeleza.


                                                MWISHO.


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...