Skip to main content

POLISI KUSINI PEMBA, LAWAHAKIKISHIA ULINZI, USALAMA WAPIGA KURA

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

JESHI la Polisi mkoa wa kusini Pemba, limewataka wananchi wote wenye sifa ya kupiga kura, kujitokeza kwa wingi Oktoba 29, mwaka huu, kutumia haki yao ya kidemokrasia, huku ulinzi ukiimarishwa.

Kauli hiyo imetolewa jana na Kamanda wa Polisi mkoani humo, Abdalla Hussein Mussa, ofisini kwake Madungu Chake chake, wakati akizungumza na waandishi wa habari,  juu ya namna jeshi hilo, lililivyojipanda na ulinzi.

Alisema, Jeshi hilo lipo kwa mujibu wa kanuni na sheria za nchi, na likiendelea kuwalinda raia na mali zao, hivyo kwa wananachi wasiwe na hofu, kwa siku kupiga kura.

Alieleza kuwa, tayari limeshajipanga kila eneo la mkoa huo na mipaka yake, ili kuwapa nafasi wenye sifa za kupiga kura kufanya hivyo, bila ya vitisho vyovyote.

Kamanda huyo alieleza kuwa, haiwezekani hata kidogo kujitokeza kwa kundi la wananchi, kutaka kuwazuia wenzao wasitekeleza haki hiyo, ndani ya mkoa huo.

‘’Niwaombe wananchi wote wa mkoa wa kusini Pemba, kwanza kuondoa hofu na usalama wao, na jingine kila mwenye sifa ya kupiga kura, aende kwenye kituo chake, bila ya wasiwasi,’’alifafanua.

Aidha Kamanda huyo wa Polisi mkoa wa kusini Pemba, Abdalla Hussein Mussa, alieleza kuwa, jeshi hilo halipo kwa ajili ya kumuonea mtu yeyote, bali linafanyakazi kwa mujibu wa sheria na kanuni.

‘’Kwa mwananchi ambae ana sifa kama atatoka kwenda kituoni kupiga kura kwa amani, na kukaa kwenye foleni kwa usalama, hatoulizwa na Jeshi la Polisi,’’alisema.

Katika hatua nyingine, Kamanda huyo wa Polisi, aliwaasa wananchi au vikundi vya watu, waliojipanga kutaka kufanya vurugu, wahakikishe watakumbana na mkono wa sheria.

‘’Ikiwa mwananchi anajiamini na anauwezo wa kupambana na vyombo vya ulinzi na usalama, ajaribu kutaka kulichafua zoezi la upigaji kura, anaweza kujutia,’’alifafanua.

Hata hivyo, aliwakumbusha wananchi, mara wamalizapo zoezi la kupiga kura, kurudi kwenye makaazi yao, na wenye mamlaka wataendelea zoezi la kura.



Mapema Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Rashid Hadid Rashid, aliendelea kuwasisitiza wananchi, juu ya kuilinda amani iliyopo, kabla, wakati na baada ya uchaguzi.

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, aliwakumbusha vijana, kutokubali kutumiwa vibaya, na baadhi ya watu, wasiowatakia mema.

Akizungumza kwenye kongamano la amani, lililofanyika umoja ni nguvu Mkoani, alisema wapo baadhi ya watu, wanakusudia kuwatumia vibaya vijana kwa lengo la kuharibu amani.

Sheikh Said Ahmad, kutoka ofisi ya Mufti Pemba akizungumza kwenye kongamano, lililofanyika ukumbi wa Kiwanda cha Makonyo Wawi, aliwatadharisha wanasiasa, kutotumia lugha za kebehi.

Wananchi wa Mkoani, akiwemo Omar Haji Mbwana na Hamada Ussi Makame wa Mwambe, waliliomba Jeshi la Polisi, kuimarisha amani karibu na vituo vya kupigia kura.

Hidaya Mjaka Ali mwenye ulemavu wa viungo, alisema athari ya vurugu zinapotokezea, waathrika wakubwa ni wao na watoto, kisha ndio jamii.

Zoezi la upiga kura kwa wagombea urais, ubunge, uwakilishi na udiwani kwa nchi nzima, linatarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.

                  Mwisho   

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...