Skip to main content

ELIMU YA UONGOZI KWA WANAWAKE YALETA MATUNDA


      


NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ 

 

TUKUMBUKE kwamba, zamani nafasi ya mwanamke haikuikuwa ikionekana na kusababisha kuwekwa nyuma na kukosa fursa mbali mbali ambazo zingemsaidia kutatua yale ambayo yanawakwaza wanawake katika jamii.

 

Wakati dunia na mabadiliko, ilionekana mwanamke hukosa yale yote ambayo anastahiki kuyapata, kwa kukosa elimu, pamoja na tamaduni zilizokuwa zikiendelea siku hadi siku.

 

Na vilionekana vikwazo mbali mbali vilivyokuwa vikiwakuta wanawake na kukosa hata kushirikishwa katika ngazi mbali mbali za maamuzi.

 

Ingawa sasa yanaonekana mabadiliko makubwa katika jamii na kuamini kwamba mwanamke anaweza kushika nafasi mbali mbali za uongozi sawa na mwanamme.

 

Ali Hamad sheha mkaazi wa Micheweni anasema, ushirikishwaji wa wanawake upo kwa kiasi, kwani zinapotokea nafasi wanashirikishwa ingawa kwenye upigaji wa kura wanawake hawana ushirikiano, hali inayomfanya akose nafasi.

 

Anasema, wanawake wakishirikiana wanayo nafasi kubwa ya kumfanya mwanamke mwenzako afanikiwe, ingawa bado hawajawa tayari, jambo ambalo linawakatisha tamaa baadhi yao.

 

"Lakini mimi naona ni ubinafsi walionao wanawake kwa sababu bado hawajawa tayari kuwepo kwenye vyombo vya maamuzi," anasema.

 

Anasema, kwa vile elimu imeenea katika jamii na wamejitokeza wengi kugombea, iliyobaki ni nafasi ya wananchi sasa kuwachagua viongozi wanawake kwaji ya maendeleo endelevu.

 


Asha Makame Haji anaeleza, wanahitaji kupeana elimu ya kuwawezesha wanawake wenye nia ya kugombea uongozi na wawape ushirikiano ili wajivunie kuwa ile nafasi anayo mwanamke.

 

Anasema, ikiwa sehemu hakuna mwanamke basi kunakuwa na mapungufu makubwa, kwa sababu mwanamke anafanya kazi nyingi na ngumu kuliko mwanamme, hivyo kunakuwa na mafanikio ya haraka.

 

"Nimewahi kufanya utafiti kwenye nyumba nikaona kwamba majukumu ya mwanamke ni mengi zaidi ya kila siku na anaweza kufika saa nne usiku bado hajapumzika anaendelea na kazi zake, lakini mwanamme anaenda zake maskani kucheza bao na mambo mengine," anaeleza.

 

Anasema, kwa hiyo wanapaswa kuwashirikisha katika nafasi za uongozi, ili kuhakikisha wanamkomboa mwanamke na utegemezi, kwani wanapokuwa tegemezi mara nyingi hawana maamuzi wala hafikii mbali kwa sababu kila kitu anachokihitaji mpaka aombe kwa mume wake.

 

Fatma Hassan Ali mkaazi wa Wingwi anafafanua kuwa, mwanamke anatakiwa na yeye amiliki mali, awe na uhuru wa maamuzi.

Ingawa kuna mambo lazima itakuwa yapo chini ya mumewe na mengine anatakiwa sauti yake mwenyewe, vyenginevyo atakuwa ananyimwa fursa na kudumaza maendeleo yao.

 

"Lakini pia kwa nafasi za kugombea, wenyewe tunakandamizana hivyo nawanasihi waache tabia hiyo, kwani wanawake tuna uwezo wa kutetea, hivyo tuwaunge mkono ili wafanikiwe kuwa viongozi," anasisitiza.

 

Fatma anafafanua, suala la kukandamizana, kupigana na kuumiza vichwa kwamba mwanamke asipewe nafasi ni choyo cha kibinadamu na ni tabia mbaya, inayosababisha wasifike mbali.

 

Khamis Hamad mkaazi wa Ole anasema, ni vyema mwanamke ashirikishwe kwa sababu kuna baadhi ya sekta ni lazima awekwe mwanamke, ikiwa ni pamoja na hospitalini kwani wakati mwengine wanashindwa kuelezea vizuri yanayomsibu anapomkuta mwanamme.

 

Anasema, bado kuna watu wana itikadi za zamani kwamba mwanamke ana wajibu wa kulea watoto tu, ingawa hayo ni mawazo finyu kwani kwa mtu mwenye uelewa wa kina basi anaamini kwamba mwanamke anaweza kushiriki na kushirikishwa katika mambo ya kimaendeleo.

 

"Tukizingatia kwamba mwanamke au mtoto wa kike anahitaji kuandaliwa mapema kushika nafasi ya uongozi tangu ngazi ya chini, lakini miaka ya sasa watu wengi wameshapata uelewa na ndio maana wameingia wingi majimboni," anaeleza

 


WAGOMBEA WANAWAKE 

 

Mgombea uwakilishi Jimbo la Tumbe kupitia chama cha Mapinduzi CCM Salma Khamis Tumu anasema, ameamua kugombea nafasi ya uwakilishi ili awafikishie wananchi huduma bora za kijamii na kiuchumi.

 

"Lengo langu ni kuwafikishia maendeleo wananchi wa Jimbo langu ili tuwe na maendeleo endelevu, hivyo nawaomba wananchi waniamini na wanichague, changamoto zote zitaondoka,’’ anaeleza.

 

Farida Juma Khamis mgombea uwakilishi Jimbo la Wawi kupitia chama cha Wakulima AFP anaeleza kuwa, wanawake wanaweza iwapo watapewa nafasi ya kuongoza, hivyo atahakikisha Jimbo lake linakuwa la mfano katika kulipatia maendeleo.

 

"Ikiwa nitafanikiwa kupata uwakilishi basi vijana watapata ajira na wanawake wataimarika kiuchumi, kwani nitawatafutia miradi mbali mbali kwa ajili ya kujipatia kipato," anafafanua.

 

 

Mgombea udiwani Wadi ya Ole kupitia chama cha Mapinduzi CCM Mtumwa Suleiman Salum anasema, sasa wananchi wamepata uelewa wa kutosha kwani, wanawaunga mkono wagombea wanawake na wanajua kuwa wanawake ni wenye kuleta mabadiliko kwenye majimbo.

 

‘’Mwaka huu ni tofauti na miaka iliyopita nyuma kwa sababu, wananchi wanatuunga mkono na ndio maana tumehamasika zaidi kugombea, tunaamini watatuchagua kwa kishindo,’’ anaeleza.

 

Khadija Anuwar ambae ni mgombea uwakilishi Jimbo la Wawi kupitia chama cha ACT Wazalendo anaeleza, zamani jamii ilikuwa ikiwakatisha tamaa wanawake wengi wanapohitaji uongozi, ingawa baada ya kupatiwa elimu wameelewa na kwa sasa wanawaunga mkono.

 

"Nguvu ya wananchi kuwakubali wanawake kuwa viongozi ndio iliyotufikisha hapa, kwa sababu wameelewa kuwa mwanamke anaweza kuleta maendeleo ya haraka, kwa kweli tunajivunia na tumezidi kujiamini," anasema.

 

Mgombea uwakilishi Jimbo la Kojani Mwanaidi Hamad Rashid anasema, kila anapopita wanajamii wanampa pongezi kwa hatua aliyoichukua ya kugombea, kwani wanaamini sasa wamepata mtetezi wa Jimbo lao.

 

‘’Kwa kweli wananchi hawaniangushi na nategemea kushinda, lengo langu ni kuhakikisha kero zote zilizopo nazitatua kwa kushirikiana na wananchi wangu,’’ anasema.

 

Mkasi Ali Hamad ambae ni mgombea ubunge Jimbo la Pandani anasema, hakushawishiwa na mtu kugombea nafasi hiyo bali alipoona jamii tayari inamkubali mwanamke, ndipo alipoamua kujitosa jimboni.

 

‘’Viongozi wa jimbo hili waliopita wote hawakufanya kitu na hii ilinishawishi nigombee ili niwatatulie wananchi kero zao, hivyo naomba wanichague ili niwaletee mabadiliko ya kimaendeleo,’’ anaeleza.

 

VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA

                                                

Katibu wa CCM Jimbo la Tumbe Mohamed Mwewe Omar anasema, wanawake wanaweza kuleta maendeleo ya haraka kwani ni waoga, hivyo wanatekeleza majukumu yao vizuri.

 

‘’Majimbo mengi yanayosimamiwa na wanawake yamepata maendeleo makubwa, kwani wanatatua kero kwa kushirikiana na wanajamii kuibua ili kuzifanyia kazi,’’ anasema.

 

Yussuf Maulid Issa ambae ni Katibu Habari, Mawasiliano na Uenezi ACT Wazalendo anasema, wanawake waliogombea wanapaswa kuungwa mkono ili watimize malengo yao ya kutaka kuingia kwenye vyombo vya maamuzi kwa ajili ya kutetea mambo yanayowahusu pamoja na kuwafikishia wananchi maendeleo kwenye majimbo yao.

 

Mgombea urais chama cha Wakulima AFP Said Soud Said anasema, wanawapa ushirikiano wanawake wanaogombea, ili kusudi watimize ndoto zao za kuwa viongozi kwenye majimbo.

 

Anawataka wagombea hao, watakapopata ridhaa ya kuongoza kwenye majimbo yao wahakikishe wanarudi kwa wananchi kusikiliza kero na kuzitatua kwa wakati, kwani wataaminika zaidi katika jamii.

 

Mwenyekiti wa ADA TADEA Wilaya ya Wete, anawataka wagombea hao iwapo watabahatika kuchaguliwa na kuingia kwenye vyombo vya maamuzi, wajitahidi kutekeleza ahadi walizozitoa kwa wananchi kipindi cha kampeni.

 

‘’Wanawake ni watendaji wazuri wa kazi, hivyo tunaamini watapita kwenye vijiji kuibu changamoto na kuzifikisha sehemu husika kwa ajili ya kutatuliwa,’’ anaeleza.

 

TAMWA

 

Amina Ahmed Mohamed ambae ni Kaimu Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake kwa upande wa Pemba, anasema TAMWA imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi ili waondokane na mawazo mgando kwamba mwanamke hawezi kuongoza na ndio maana mwaka huu wamegombea wengi.

 

"Jamii sasa imepata uwelewa na wamejua umuhimu wa mwanamke kuongoza kwa sababu waliokaa majimboni wote wamefanya vizuri na maendeleo yanaonekana," anaeleza.

 

Kaimu huyo anasema, pia wanawajengea uwezo wanawake wenye nia ya kugombea uongozi ili wajiamini, wawe na ujasiri pamoja na kutekeleza yale ambayo wanayaahidi kwa ajili ya kujenga Taifa lenye maendeleo.

 

Wagombea hao ametekekeza haki yake ya kushiriki katika demokrasia na uongozi, kama Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1964 ilivyoeleza kwenye kifungu cha 21 (2) na kifungu cha 67 (1) cha Katiba hiyo kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2010.

 

                                                         MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...