Skip to main content

SAUMU HUSSEIN, ANAEWANIA URAIS TANZANIA, AAHIDI KUIFUNGUA NCHI KIUCHUMI

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KIPYENGA cha kampeni za uchaguzi mkuu, kwa upande wa Zanzibar, kilipulizwa Septemba 12.

Hapo, ilikuwa ni nfasi kwa wagombea, kujitupa viwanjani na kwenye kumbi mbali mbali, kutangaaza sera na ilani zao.

Kwa Tanzania, kwa mujibu wa sheria ya Vyama vya Siasa, uchaguzi hufanyika kila baada ya miaka mitano.

Maana uchaguzi wa kwanza, wa vyama vingi nchini ulifanyika pale mwaka 1992, na sasa taifa hili linaelekea kufanya uchaguzi wake wa saba, Oktoba 29, mwaka huu, yaani kesho.

IIishazoeleka, kila unaposikia neno uchaguzi, huihusisha jinsia ya wanaume pekee, jambo ambalo ni kukiuka mikataba, sheria na katiba.


 Ijapokua, kwa sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022, Tanzania ilionesha wanawake ni wengi zaidi kwa asilimia 51.6 na wanaume 48.4, lakini takwimi hizi hazinauhusiano na uwingi wao, kwenye safu ya uongozi.

Kwa upande wa Zanzibar, sensa ikamulika kuwa, wananchi wote ni milioni 1.8, kati yao wanawake wakiwa laki 974,281 na wanaume ni 915,492.

Eneo jingine, Zanzibar inayo mikoa mitano, ingawa wakuu wake wa mikoa wanawake ni wawili tu, huku takwimu zikiumiza tena kichwa kwenye wilaya 11, wanawake wakiwa wawili.

Hayo yanaendelea kuwaumizwa vichwa wanaharakati kuona nini kinakwamisha wanawake kutokuwa wingi kwenye uchaguzi, kwengineko ni majimbo 18 wawakilishi wakiwa wanne pekee wanawake ksiwani Pemba.

Lakini, chenyewe chama cha UDP, kimemuamini mwanake, kupeperusha bendera ya chama chao, katika nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  

Ushupavu wa mgombea huyo Saumu Hussein Rashid, amesema lengo la chama hicho ni kufungua fursa za kiuchumi kwa kila mtanzania, ili aweze kujitosheleza kupitia biashara yake.

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wajasiriamali wa soko la Tibirinzi Chake chake Pemba, wakati akitoa sera ya chama hicho na kuomba kura kwa wafanyabiashara hao.

Anasema kuwa atahakikisha anakuza kipato cha watanzania, ili kuifungua kiuchumi kwa kila mjasiriamali, aweze kujitosheleza katika mahitaji yake.



Alifafafanua kuwa atahakikisha anaweka miundombinu mizuri, itakayowawezesha wajasiriamali wadogo, ili waweze kuwa wafanyabiashara wakubwa, kwa kuongeza pato lao.

‘’Niwambie wajasiriamali nina nia njema na ilani ya chama change, ni kuwanyanyua kiuchumi, ili muwe wafanyabiashara wakubwa, muweze kujitosheleza katika mahitaji yenu,’’ alifafanua.

Alieleza kuwa chama hicho kimejidhatiti, katika suala la upendo daima, pamoja na kuendeleza kudumisha amani, umoja na utulivu.

KILICHOMSUKUMA KUOMBA NAFASI HIYO

Anasema, ni kuona wanawake na watu wenye ulemavu, wakilalamikia kudororo kwa uchumi, jambo linamlokasirisha.

Njia pekee ni kugombea nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na pindi akipewa ridhaa atalitekeleza hilo kwa vitendo.


‘’Nina hamu sana kuwataka watanzania, wahakikishe wananipa kura za ndio, ili nije niwatumikie kwa dhati,’’anasema.

Eneo jingine, anasema ni kuona wananchi, wananufaika na rasilimali zao, ikiwemo mazao ya biashara na taifa.

Lakini, akwaahidi wanawake, kuwa hawatodhalilishwa tena, na kisha kesi zao kubakia kwenye mafaili ya mahakamani, kama ilivyo sasa.

‘’Niwahakikishie kuwa, nikiingia madarakani, jambo la mwanzo sheria zitarekebishwa, maana nimegundua wanawake wanadhalilisha na hawapati haki zao,’’anasisitiza.

HAWAOGOPI WANAUME KWENYE KINYANG’ANYIRO HICHO

Anasema, hana hofu, wasiwasi na wagombea wanaume, maana anasema hawaendi kwenye jukwa kwa mapambano ya mwili, bali wanashindana kwa sera.

Mgombea huyo, anasema ilikuwa kazi rahisi mno, ndani ya chama chake, baada ya kutangaaza nia kukubaliwa, kutokana na ujasiri wake.

‘’Mara tu wajumbe waliponikubali kuwa nipeperushe bendera, ndipo nilipoanza, kujiamini na sikuwa na hofu hata mgombea mwingine,’’anasema.

Akawataka wanawake, waendelee kutetea haki zao za kudai uongozi, iwe ngazi ya familia, taasisi, udiwani, ubunge n ahata urais kama mimi,’’anashauri.

 

WAFANABIASHARA WANAMATUAMINI GANI?

Mfanyabiashara wa soko la Chake chake kwa niaba ya wenzake Mohamed Juma, wamemuomba mgombea huyo, kuwaimarishia soko hilo, ili liwe katika mjumuiko na muanganiko wa biashara zote.


Anasema kuwa kwa sasa soko hilo, limewatenganisha wafanyabiashara hao kupitia bidhaa zao, na limepoteza haiba yake kibiashara.

‘’Sisi wafanyabiashara tumejitenga kupitia biashara zetu mbali mbali, tunakuomba utuimarishie soko letu, liwe la kisasa na lenye muonekano mzuri,’’ alifafanua.

Nae Omar Haji Omar, amesema anayomatumaini ya karibu, pindi mgombea huyo akipata ridhaa, kwa kuimrisha biashara zao, kutokana na kuwa na sera za kijamii.

Khadija Yussuf Mgeni, anasema kwa sasa wajasiriamali wadogo, wanaendelea kudidimia, kutokana na kodi na matozo yasiozingatia mwenendo wa soko.



‘’Mimi kura yangu utaipta kesho Oktoba 29, maana sera za ahadi zako, kwangu zinanipeleka kwenye ndoto za kuwa mjasiriamali mkubwa,’’anafafanua.

WANAWAKEW WANASEMAJE

Aisha Haji Hassan wa Chake chake, anasema mgombea huyo ana dira la kuwainua kiuchumi, na sio kuwakandamiza.

Khadija Ali Hija wa Madungu, anasema amekuwa akimfuatilia mgombea huyo, na amekuwa na sera kama mbobevu wa uchumi.

‘’Wanawake kama hawa wanafaa mno kuwaunga mkono, maana sera zake hazionekani kama za kubabaisha,’’anasema.

WANAHARAKATI

Amina Ahmed Mohamed, ambae ni Kaimu Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, anasema wanayo haki sawa ya kuongoza, kama walivyo wanaume.

Anasema, wakati umefika sasa kwa wapiga kura, kuwaamini wagombea wanawake, kuanzia ngazi ya udiwani hadi urais.



Mashavu Juma Mabrouk, ambae ni Mratibu wa Baraza la taifa la watu wenye ulemavu, anasema kadiri siku zinavyokwenda, na wanawake wanaanza kuonekana.

‘’Lakini juhudi inahitajika mno, maana wanawake wamekuwa wakiburuzwa kwa uhaba wao, katika vyombo vya maamuzi,’’anasema.



Mohamed Hassan Ali, anasema sheria kwa vile zinawaruhusu kuomba nafasi za uongozi, jamii iendelee kuwaamini.

KATIBA/SERA/MATAMKO

 Katiba ya Zanzibar ya 1984, kwenye kifungu cha 11 na cha 14, vimeweka wazi kuwa kila mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi, juu ya mambo yanayomuhusu.

 

Dira ya Zanzibar ya 2050 imeelezea jinsi gani masuala ya usawa wa jinsia, juu ya kuondoa unyanyasaji na kuimarisha mifumo ya uwezeshaji wanawake.

 


Sera ya jinsia inaeleza ushiriki wa wanawake katika vyombo vya utoaji maamuzi, katika ngazi zote ni mdogo na kwa hivyo serikali, itafanya juhudi kuona makundi yote na yaliyopembezoni.

 

Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ambayo mkataba wake ulitiwa saini mwaka 2008 inaeleza, kutaka kuondoa utafauti na kuwatenga wanawake katika nyanja mbalimbali za maendeleo.

 

Na kusaidia kuwepo usawa wa kijinsia katika nchi wanachama na kufikia asilimia 50/50 kwenye  ngazi zote za maamuzi.

 

Makubaliano yanayojulikana kama ‘Itifaki ya Maputo’ ambayo yalifanyika Msumbiji mwaka 2003, inacho kipengele kinachoonyesha haki ya wanawake, kushiriki katika siasa na mchakato wa vyombo vya kutoa maamuzi.

 

Mkataba wa kimataifa wa kutokomeza aina zote za ubaguzi, (CEDAW) wa mwaka 1979, ambao unapinga aina zote za udhalilishaji na kusisitiza, ushiriki wa wanawake katika siasa na uongozi.

 

Ibara12, inasisitiza ushiriki sawa wanawake na wanaume kufikia asilimia 50 kwa 50, kwenye nyanja za maamuzi, serikalini na taasisi binafsi.

 

Aidha jukwaa la Mpango wa Utekelezaji wa Beijing mwaka 1995, ibara ya 7 kinataka ushiriki katika vyombo vya maamuzi kwa kuzingatia uwiano wa kijinsia kwenye ngazi zote.

                                    Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...