Skip to main content

KURA YA MAPEMA PEMBA YAFANYIKA KWA AMANI

 




 NA WAANDISHI WETU, PEMBA

ZOEZI la upigaji wa kura ya mapema, lililofanyika Zanzibar, kwa upande wa Pemba liliripotiwa kwenda kwa amani na utulivu, katika vituo kadhaa, vilivyopangwa kufanyikwa kwa zeozi hilo, leo.

Waandishi wa habari walishuhudia vikosi vya ulinzi na usalama, vikizunguruka katika miji, mitaa na vitongoji mbali mbali, kisiwani humo.

Wakati zoezi hilo likiendelea kwa watu maalum, wakiwemo walinzi wa amani na watendaji wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ‘ZEC’, wananchi katika miji ya Chake chake, Mkoani, Wete na Micheweni waliendelea na shuguli zao.

Ilibainika kuwa, maandalizi ya zoezi hilo lilofanyika leo Oktoba 28 yalifanyika kuanzia jana Oktoba 27, kwa watendaji, wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa upigaji kura, kufunga vifaa kwa wakati.

Akizungumza na waandishi wa habari Mratibu wa ‘ZEC’ Pemba Ali Said Ali, alisema hadi leo majira ya saa 6:55 mchana, hakujaripotiwa tukio lolote, lililozuia au kuashiria kuzuia zoezi hilo.

Alisema, watendaji walioteuliwa na ‘ZEC’, wanaendelea kutekeleza kazi hiyo kisheria, na kila aliyepaswa kupiga kura ya mapema, alifanikiwa.

‘’Kwa hakika lazima tuwapongeze wenzetu wa kamati za ulinzi, maana zoezi hadi nazungumza na wewe, linakwenda vyema katika vituo vilivyopangwa,’’alifafanua.

Hata hivyo, aliwasisitiza wananchi kisiwani humo, kuendelea kuheshimu na kutii sheria kama zilivyo, ili uchaguzi wa mwaka huu, uwe wa kihistoria kwa utunzaji wa amani.

Kamanda wa Polisi mkoa wa kusini Pemba, Abdalla Hussein Mussa, alisema zoezi hilo liliripotiwa kuendelea kwa amani mkoani humo.

Alisema, vikosi vya ulinzi na usalama, vinaendelea kuwalinda wananchi, na kuhakikisha hakuna mtu wala kikundi cha watu, kitakachoharibu amani.

Alieleza kuwa, kura ya mapema ambayo ipo kisheria, itaendelea na kumalizika kwa amani, kama ilivyopangwa.



‘’Niwashukuru wapiganaji kwa kuendelea kulinda amani, hasa kwenye siku hii ya kura ya mapema, utulivu umetawala na twashukuru mno,’’alifafanua.

Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, akitoa taarifa kwa waandishi wa habari ofisini kwake, majira ya saa 5:20 mchana alisema mkoa huo unaendelea kutumia neema ya amani.

Alisema hakuna vitisho wala viashiria vya uvunjifu wa amani ndani ya mkoa huo, wakati zoezi la upigaji wa kura ya awali, likiendelea.

‘’Niwambie waandishi wa habari kuwa, mkoa wa kaskazini Pemba, hali ya ulinzi na amani imeimarishwa, hivyo hadi nazungumza na nyinyi hivi sasa, mkoa uko salama na umejaa amani,’’alisema.

Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, akizungumza na mwandishi wa habari hizi, alisema hadi majira ya saa 5:15 wilaya hiyo ilikuwa shuwari.

‘’Kila dakika vyombo vya ulinzi vinanipa taarifa, kuendelea kwa amani, na hakuna hata sehemu ambayo wananchi waliandamana,’’alifafanua.

Nae Mkuu wa wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja, alikiri kuwa, bado wilaya yake ni shuwari, na hakuna taarifa zozote za uvunjifu wa amani.

‘’Ni kweli leo kuliwepo kwa baadhi ya vituo ambavyo, vilipigisha kura ya mapema, lakini hadi saa 7:30 hali imeripotiwa shuwari,’’alisema.

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Rashid Hadid Rashid alisema, hadi saa 5: 55 mchana wa leo, tayari alishavitembelea vituo saba, kikiwemo cha Gombani, Kwale, Kiwani, Ole, Pujini, Chambani, na hali inaendelea vyema.

‘’Hapa nilipo sasa naelekea kitu chingine, na hivyo ambavyo nimeshavitembelea, hali ni shuwari na hakuna vitisho, wala maandamano yoyote,’’alisema.

Aidha, aliwakumbusha wananchi kuendelea kuilinda amani na utulivu katika maeneo yao, ili  zoezi la uchaguzi, limalizike kwa amani.

Baadhi ya wananchi waliviomba vyombo vya ulinzi na usalama, kuendelea kulinda amani, hata katika uchaguzi wa wote, unaotarajiwa kufanyika kesho.

Makame Iddi Makame wa Machomane, alisema kama leo wakati wa zoezi la upigaji kura ya mapema, umefanyika kwa amani, hakuna budi kuendelea.

Msimu Haji Issa wa Madungu ambae ni mfanyabishara, alisema aliendelea na bishara zake, kama vile hakuna jambo la kitaifa, kisiwani Pemba.

                      Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...