Skip to main content

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA PANDANI AAHIDI KUBADILISHA PANDANI KUWA YA KISASA.

 


NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA

KATIKA miaka ya hivi karibuni, wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika nyanja nyingi za uongozi, kuanzia siasa hadi biashara.

Hata hivyo, safari yao haijakosa changamoto,Ingawa dunia imepiga hatua katika masuala ya usawa wa kijinsia, bado wanawake wengi wanakosa nafasi sawa za kushiriki katika maamuzi

Dunia ya sasa imekua kiteknolojia hususa ni ushiriki wa wanawake katika kutoa mamuzi na hata kusimamia uwongozi wa nyanja mbali mbali nchi.

Tanzanzia ni moja ya nchi ambayo kila ifikapo October  hufanya uchaguzi kila baada ya miaka 5 kuwapa nafasi wananchi ya kuchagua kiongozi wanaye mtaka.

 Takwimu za Zanzibar  zinaonyesha kuwa katika uchaguzi wa mwaka 2020, waombaji wanawake walikuwa 135 kati ya jumla ya 601 waliojitokeza kuchukua fomu sawa na asilimia 22.4% na mwaka 2025 zaidi ya asilimia 75 ya wagombea wanawake wamejitokeza kugombania.

Hii ni kutokana na elimu iliyotolewa na wadau mbali mbali wakiwemo wa haki za binadamu ili kuona usawa wa kijinsia umefikiwa.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Pandani  Salama Massoud amesema kuwa ,lengo la  chama chao ni kumuwezesha mwananchi kujikwamua kiuchumi na kufikia uchumi wa soko la kati kimataifa ili nchi kuendana na ukuwaji wa kiteknolojia uliopo.

 


Salama ni mwenye umri wa miaka 47  mkazi wa mzambarauni  mwenye elimu ya kidato cha nne mwenye taluma ya uwalimu ngazi ya cheti ambaye pia amebahatika kua na nafasi ya ofisi ya bunge  EALA ambaye anahudumua kama katibu muktasi binafsi wa Mbunge wa CUF

Amesema kilicho msukuma kuamua kugombea nafasi hiyo ni kuhakikisha analeta mabadiliko jimbo la Pandani katika nyanja mbali mbali.

Alifahamisha kuwa, ataweka miundombinu rafiki itakayowawezesha wajasirimali na wananchi wa kipato cha nchi kuweza kujikwamua kimaisha kwa kuanzisha miradi itakayowaletea kipato.

"Malengo yangu ni kuhakikisha nakipatia ushindi chama cha wananchi CUF na kuijenga Zanzibat inayoendana na mtazamo mpya unaoendana na dunia ya mahitaji ya dunia ya sasa inayomilikiwa na teknolojia,"alieleza.

Amesema atahakikisha wananchi wanamiliki mlo wa mara 3 kwa siku ili kukuza ustawi mzuri wa mwili na akili sambamba na kukuza sekta ya uchumi husasa ni kwa wajasirimali pamoja na kukuza pato la zanzibar katika mazao yaliyopo ikiwemo karafuu.


Ukosefu wa ruzuku haukusita katika kufanya kampeni zake kwa kuimarisha uzalengo wa chama chake kwa wananchi wake ili kuhakikisha malengo yake matimia na hata ya jimbo lake.

Asha Makame Juma mkazi wa Pandani ambaye pia ni mwanachama wa chama cha CUF asema amefurahishwa na sera za mgombea ubunge huyo na atashirikiana nae ili kuona wanaleta mabadiliko katika jimbo lao.

"Tunatakiwa kwenda kwenye mikutano kuskiliza sera za wagombea mbali ili sasa ifikapo uchaguzi kila mmoja achaguwe kiongozi anaye mfaa bila ya virugu ya aina yoyote na kwa amani kabisa,"alieleza.

Juma Khamis faki amesema kuchagua kiongozi ni haki ya kila raiya hiyp hawana budi kuona na wao wanapata haki hiyo kwa kujitokeza kwa wingi na kuona wanatimiza haki yao ya msingi ili kuoa na taifa imara.



Salma khamis Mjasirimali mdogo mdogo alieleza, jinsi alivofurahishwa na sera ya kuwawezesha wajasirimali kwani bado kuna uhitaji katika kuhakikisha wajasirimali wanafikia malengo yao hivo ni kuona badailiko katika hatua hiyo.

"Sisi kama wanawake tunashirikina kwa pamoja ili kuona wanawake wenzetu wanashika nafasi mbali mbali katika ngazi za mamuzi hususa ni serekali.

Chama cha wandishi wa habari Tanzanzia TAMWA kwa kushirikiana na wadau mbali wa haki za binadamu wamesema kuwa wanawake wanayo haki sawa ya kushiriki na kuongoza kama walivyo wanaume.

Aliyasema hayo Kaimu Mratibu wa Chama cha Wandishi wa Habari wanawake Tamwa TAMWA Zanzibar ofisi ya Pemba Amina Ahmed Muhammed.

Katiba ya Zanzibar ya 1984, kwenye kifungu cha 11 na cha 14, vimeweka wazi kuwa kila mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi, juu ya mambo yanayomuhusu..

Serikali ya Zanzibar imejidhatiti kuweka rasilimali maalum (mfano: bajeti, kamati kitaifa) kama sehemu ya kuhakikisha utekelezaji wa usalama wa wanawake.

 Dira ya Zanzibar 2050 inaweka msingi mzuri wa sera na mwelekeo kwa masuala ya usawa wa jinsia, kuondoa unyanyasaji wa kijinsia, na uwezeshaji wa wanawake. Hata hivyo, ama utekelezaji wa vitendo, ushiriki wa wanawake kwa ukamilifu katika ngazi zote, na ufuatiliaji wa kina ni maeneo ambayo yatahitaji nguvu zaidi ili dhamira hiyo iwe matokeo.

Mwenyekiti wa chama hicho Profesa Lipumba amesema wanawake walio wengine wamepata elimu na uwelewa wa kushiriki katika nafasi mbali mbali za kugombani uwongozi ili kuona nchi sasa inaenda na uswa wa kijinsia katika kushiriki na kushirikishwa kwa wanawake.

Mgombea huyo hakusita kuwasisitiza wananchi endapo watamchagua wataona mabadiliko makubwa husasa katika nyaja muhimu ili kuona mabadilo ya jimbo la Pandani na kuwa mfano kwa majimbo mengine.

Ushiriki wa wanawake katika nyanja mbali mbali utasaidia kujenga taifa imara na lenye usawa wa kijinsia.

      Mwisho.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...