Skip to main content

ZANZIBAR NA SURA YA UJUMUISHI BADO KAA LA MOTO

 


NA ZUHURA JABIRI, ZANZIBAR

ZANZIBAR, ni kisiwa kinachojivunia amani, mshikamano wa kijamii na historia ndefu ya kuishi pamoja.

Ingawa nyuma ya taswira hii ya utulivu, kuna sura nyingine isiyoonekana mara nyingi sura ya watu wenye ulemavu, wanaoendelea kusubiri usawa wa kweli.

Kwa mujibu wa takwimu rasmi, Zanzibar ina watu 167,308 wenye ulemavu, sawa na asilimia 11.4 ya wananchi wake milioni 1.89.

 Hata hivyo, katika meza ya maamuzi, katika ajira rasmi, na hata katika huduma za msingi, kundi hilo, bado lipo pembeni.

Ijapokuwa sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya nambari 8 ya mwaka 2022, inahakikisha haki sawa katika elimu, ajira, afya na ushiriki wa kisiasa.

Lakini kati ya maandishi ya sheria na maisha ya kila siku, kuna pengo kubwa pengo linalowaacha watu wenye ulemavu wakionekana, lakini hawasikiki.

“Nimejitolea maisha yangu kupambana na ubaguzi dhidi ya watu wenye ulemavu na kuhakikisha hatusahauliki,” anasema Salma Saadat, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA).

Kwa miaka mingi, Salma amekuwa mstari wa mbele katika harakati za kuunganisha sera na uhalisia.

Kupitia JUWAUZA, amefundisha wanawake wenye ulemavu, ujasiriamali na uongozi, akiwapa zana za kuvunja mitazamo potofu inayowafanya waonekane dhaifu au wasio na mchango.



“Sisi tuna uwezo, na tunastahili kuwa katika kila nafasi ambako maamuzi yanafanyika,” anasisitiza.

Kauli yake inaakisi kilio cha wengi kwamba tatizo si ukosefu wa vipaji, bali ni mifumo isiyo rafiki kwa kundi la watu wenye ulemavu.

Muhtasari wa takwimu za Zanzibar wa mwaka 2024 zinathibitisha hali hiyo, maana zaidi ya watoto 60,000 wenye ulemavu wako nje ya mfumo wa elimu.

Watu wazima wenye ulemavu wanawakilishwa kwa kiwango kidogo sana katika ajira rasmi, chini ya asilimia 2 katika sekta za umma na binafsi.

Wanawake wenye ulemavu wanakumbwa na ubaguzi maradufu kwa misingi ya jinsia kwa ulemavu wao.

Kwa wazazi kama Salma Hamadi Mwarabu, changamoto hizi si takwimu tu bali ni maisha halisi.

Kijana wake wa kiume mwenye umri wa miaka 24 amekuwa na ulemavu wa miguu na kifafa tangu utotoni, jambo ambalo kwa baadhi ya wakati huwa ni changamoto ya kukosa haki na fursa.

 “Kila mwaka natafuta programu au fursa kwa ajili yake, lakini msaada hautoshi,’’anaeleza.  

Hata huduma za kawaida za tiba na urekebishaji ni vigumu kuzipata kama huna fedha.

Hadithi ya Salma inaonyesha ukweli mpana wa mfumo unaowaacha watu wenye ulemavu na familia zao wakihangaika.

Ajira ni kikwazo kikubwa zaidi, akisema maana waliowengi hulazimika kujiajiri si kwa sababu wamechagua, bali kwa sababu hawana chaguo jingine.



Nassor Juma Nassor, mwenye ualbino, anakumbuka upweke aliokumbana nao akiwa mtoto huko Maungani, Wilaya ya Magharibi.

 Sasa akiwa na umri wa zaidi ya miaka 50, anasema uzoefu wake shuleni ulimvunja moyo.

 “Sikutendewa kama wingine, maana waalimu hawakujua jinsi ya kunisaidia, wanafunzi hawakunielewa,’’anakumbuka.

“Watu wenye ulemavu wana vipaji, ingawa hufifilizwa na jamii na wasisimamizi wa sera, kwa kule kutowapa haki na fursa zao,” anasisitiza.

Na ndio maana tasisi kama Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA-Zazibar inaendelea kuwatafuta wafadhili, ili kuwajengea uwezo waandishi wa habari, kuibua changamoto za watu wenye ulemavu.



Akifungua moja ya mafunzo hayo, Mkurugenzi wa TAMWA-Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali, anasema waligundua watu wenye ulemavu, mafanikio na juhusi zao zao hazitangaazwi na vyombo vya habari.

''Ukisikia taarifa ya watu wenye ulemavu, aidha amebakwa, amedhalilishwa ama amefukuzwa kazi, laki kazi zao na mafanikio husikii sana,''anasema.

Kwa mujibu wa Hija Shamte, Afisa Mawasiliano wa Shirikisho la Watu Wenye Ulemavu Zanzibar (SHIJUWAZA), anasema tatizo hili ni la kimuundo.

“Sera zipo ndiyo, lakini utekelezaji ni wa kusuasua na huwapa mazingira magumu mara mbili kundi la watu wenye ulemavu,” anasema.

Anasema majengo mingi ya umma na sehemu za kazi, bado hayana miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu, ingawa sera na sheria zinalazimisha hilo.

 Anaona taratibu za kuajiri mara chache huzingatia kundi hilo, kama vile wanalazimishwa tu na sio kwa utekelezaji wa sheria.

Anafafanua kuwa, pengo la ajira na uongozi bado ni kubwa, akitolea mfano kuwa, katika majimbo yote ya uchaguzi ni jimbo moja la Ziwani Pemba, linanaoongozwa na mtu mwenye ulemavu.

Ukosefu huu wa uwakilishi unaendeleza mzunguko wa kutengwa kuanzia maamuzi hadi ugawaji wa rasilimali.



Katika ngazi ya jamii, athari zake zinaonekana wazi, kama anavyosema Naila Mohamed, Mwalimu kutoka Jendele, Wilaya ya Kati.

Anasema licha ya kauli mbiu za ujumuishi, uhalisia ni tofauti, maana watunga sera na watoa maamuzi bado wamezingiriwa na ubinafsi.

Mratibu wa Baraza la taifa la watu wenye ulemavu ofisi ya Pemba, Mashavu Juma Mabrouk, anasema mashirika ya kijamii, vikundi vya watu wenye ulemavu, na wanaharakati wanaendelea kuziba mapengo yaliyoachwa na mfumo.

Lakini juhudi hizi haziwezi kuchukua nafasi ya dhamira ya serikali na jamii kwa ujumla, kama mifumo hiyo haikukaziwa Kamba na serikali kuu.

“Matumaini yangu ni kuona watu wenye ulemavu wakijumuishwa, kikamilifu katika kila nyanja ya maisha,” anasema.

Zanzibar ina kila sababu ya kuwa mfano wa ujumuishi katika ukanda huu, ingawa hadi pale ambapo mtoto mwenye ulemavu, atapata elimu bila vikwazo na kuingiwa kwenye mifumo ya ajira.

Katika kisiwa kinachojivunia amani na mshikamano, swali linabaki, ikiwa je, amani hiyo itakuwa kamili bila ya kuwepo kwa mifumo jumishi.

Mashavu anaendelea kuhoji, kwamba watu wenye ulemavu wapo, wana sauti, na wana mchango mkubwa wa kutoa, ingawa mifumo thabiti na isiyo na kikwazo kama inawezekana.

Kilichobaki ni jamii na mifumo kuamua je, wako tayari kuwasikiliza na kuwapa nafasi wanayostahili.

Changamoto nyingine kubwa inayowakabili watu wenye ulemavu Zanzibar ni mtazamo wa kijamii, kwa kule kuwaona hawana mchango wowote.

Katika jamii nyingi, ulemavu bado hutazamwa kama mkosi, laana, au jambo la kufichwa na wakati mwingine hata kukosa haki za msingi ikiwemo aelimu.

Mtazamo huu huanza nyumbani, huendelea shuleni, na hatimaye hujikita katika taasisi za umma na hasa mifumo ya kiajira na fursa za uongozi.

Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Mgeni Khatib Yahya anasema, mtoto mwenye ulemavu anapokosa kupelekwa shule si kwa sababu hana uwezo wa kujifunza, bali kwa sababu wazazi au walezi huamini.

Anasema hii ni aina ya unyanyasaji wa kimnya kimnya unaonyima kizazi kizima haki ya kuota ndoto.

Akifafanua kuwa, suala ujumuishi kwa kundi la watu wenye ulemavu, sio jukumu la serikali tu, bali inapendezea ikianzia ngazi ya familia.

Anasisitiza kuwa, ni wajibu wa jamii nzima kuanzia familia, taasisi za elimu, waajiri, viongozi wa dini hadi vyombo vya habari, katika kulifanikisha hili.

Mtoto Daudi Hija Hassan mkaazi wa Mwembeladu Unguja, mwenye ulemavu wa uoni, anasema kama ujumuishi haukuanzia ngazi ya familia, kusitarajiwe mabadiliko serikali kuu.

Sheikh Hassan Omar Kassim wa Chake chake anasema Imani na mitazamo ya dini, ikiwa imejaa kiroho, yengetosha kuhakikisha kila mtu anapata haki yake.

Eneo la Mkataba wa Kimataifa wa watu wenye ulemavu wa mwaka 2016, kwenye ibara zake za 34 inazitaka nchi wanachama, kuanzisha kamati za kutetea haki za watu wenye ulemavu.

Ibara ya 27, yenye ikasisitiza suala la kuwaajiri watu wenye ulemavu, wakiwa ni sehemu ya jamii.

      Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...