Skip to main content

WIZARA KUZIDI KUSHIRIKIANA NA POLISI: PEMBE

 



Na Muandishi wetu Zanzibar@@@@

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (WMJJWW) Mhe Riziki Pembe Juma amesema Wizara hiyo inaendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi ili kuona upelelezi wa kesi ya Mtuhumiwa Ramadhani Hamza Hussein (28) Mkaazi wa Tomomdo, Unguja anayetuhumiwa kwa kosa la kumdhalilisha mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 13 inafikishwa Mahakamani ili haki itendeke.

Kauli hiyo ameitoa jana wakati akimkagua mtoto huyo aliyelazwa katika Hospitali ya Mkoa, Lumumba Zanzibar, baada ya kufanyiwa  vitendo vya udhalilishaji huko Jang'ombe Mjini Unguja na Mtuhuhumiwa Ramadhani Hamza Hussein.

Waziri Riziki amesema tukio hilo limetokea tarehe mosi, Machi, mwaka huu,  na kuripotiwa  tarehe 31/03/2025 katika kituo cha Mkono kwa Mkono pamoja na kufanyiwa uchunguzi wa kitaalamu na hatimae kupewa PF3.

Ametoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano wa kutosha katika kupiga vita vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia kwani hatua hiyo itasaidia kupunguza vitendo hivyo katika jamii kwani vinaathiri kimwili na kisaikolojia.



Mhe Riziki amesema  endapo mtu ataona kuwepo kwa viashiria vya aina yoyote ambavyo vitasababisha kutokea vitendo hivyo, ni vyema kuripoti sehemu husika ikiwemo kwa sheha wa shehia husika au kituo cha Polisi kilichopo karibu naye ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa haraka.

"Ukweli suala la udhalilishaji linatuumiza sana wazazi, maana hata mshtakiwa afungwe miaka 100 au kifungo cha maisha, lakini hakiwezi kurudisha thamani na utu wa mtoto wetu, nawaomba wanaume jamani tafuteni watu wazima wenzenu na tuachieni watoto wetu" amesisitiza Waziri huyo.

Mwisho ametoa wito kwa jamii kuendelea kuwalinda na kuwajali watoto wao, pamoja na kuwafuatilia miendendo yao ili kuwakinga na vitendo vya udhalilishaji kwani kinga ni bora kuliko tiba.

Kwa upande wa Daktari aliepewa dhamana ya kumshughulikia mtoto huyo Dk. Hasnat Mbarouk Salum amesema mpaka sasa hali ya mtoto huyo inaendelea vizuri ambapo ametoa wito kwa jamii kuacha vitendo hivyo na kusaidia watoto kukua  katika mikono salama ya wazazi na walezi pia.

                     MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo n...

HABARI ZA HIVI PUNDE

 TAARIFA za hivi punde, zilizofikia ofisi ya Pemba Today, zinaeleza kuwa, Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia askari mwenzao, kwa tuhuma za ubakaji ndani ya moja ya kituo cha Polisi kisiwani Pemba Muume wa mwanamke aliyedai kubakwa na Mwanamke mwenyewe, wamedai kutokea kwa tendo hilo, na huku Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, akithibitisha kupokea kwa lalamiko hilo.... Kwa taarifa zaidi ya tukio hili endelea kufuatilia mtandao huu, ambao kukuhabarisha ni fahari yetu...