Skip to main content

ZLSC YAIKUMBUSHA JAMBO JAMII SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA::::

MKURUGENZI wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Harusi Miraji Mpatani, amewakumbusha wananchi kuwa, njia pekee ya kumaliza matendo ya ukatili na udhalilishaji, dhidi ya wanawake na watoto, ni wahanga kutokubalia kurubuniwa kwa fedha au ahadi ya ndoa.

 

Alisema, mfumo uliopo sasa kwa wadhalilishaji wakiona wazazi wa muhanga anamsimamo wa kufikisha na kuisimamia kesi ya mtoto wake, watuhumiwa huanza kutoa ahadi za ndoa na fedha, ili kuzilainisha kesi hizo.

 

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu leo Novemba 18, 2022  kuelekea siku 16 za kupunga ukatili n audhalilishaji, Mkurugenzi huyo alisema, tayari zipo kesi kadhaa ambazo zimeshafikisha mahakamani, na hukosa hatia kutokana na wazazi kukubali kurubuniwa.

 

Alileza kuwa, wakati huu wa kuelekea siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto, ni vyema jamii, ikamka na kutetea haki za watoto waliodhalilishwa.

 

Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa, ikiwa tayari mtoto ameshadhalilishwa, kwa mzazi au mlezi kuchukua fedha au kitu chengine cha thamani ili kuiua kesi hiyo, ni kumuongezea maumivu mtoto wake.

 

‘’Wanaharakati tukiwemo sisi Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ kwa sasa tumo kwenye kampeni na ukumbusho maalum, ndani ya siku 16 za kupinga ukatili, kwa jamii kuwa makini na mbinu chafu za wadhalilishaji,’’alieleza.

 




Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo wa ZLSC, aliisisitiza jamii kuendelea kuwatumia wasaidizi wa sheria, waliomo kwenye maeneo yao, ili kujua haki na wajibu wao.

 

‘’Naamini kama jamii ikiendelea kupata elimu, ushauri na msaada wa kisheria, wanaweza kuona athari ya kuzifanyia sulhu kesi za udhalilishaji,’’alieleza.

 

Hata hivyo Mkurugenzi huyo, amewakumbusha wasimamizi wa haki wakiwemo majaji, mahakimu, waendesha mashtaka, Polisi na wengine kuendelea kutumia weledi wao katika uendeshaji a usimamizi wa utoaji wa haki wa kesi mbali mbali.

 

Akizungumzia kuhusu siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji, Mkurugenzi Harusi, amesema ni wakati kwa jamii kuendelea kufuatilia vyombo vya habari, ili kuongeza elimu ya maarifa.

 

‘’Kipindi hichi ni kizuri kwa jamii, kusikiliza vyombo vya habari, ili kuongeza ujuzi wa namna bora ya kupambana na matendo ya ukatili na udhalilishaji,’’alifafanua.

 

Hivi karibuni Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema kila mmoja akitimiza wajibu wake, matendo hayo yataondoka.

 

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, amewakumbusha masheha, wasijiingize kwenye kusimamia sulhu ya mtendo hayo.

 

‘’Sheha ambae atajiingiza kwenye matendo hayo, na kuyafanyia suluhu, basi mwenyewe andike barua ya kuacha kazi, kabla sijagundua,’’alisisitiza.

 

Mzazi ambae mtoto wake wa miaka 11 alibakwa na Khamis Chuma ‘soda’ miaka 76 mjini Chake chake, alisema matendo hayo kama sheria ya adhabu ya kifungo cha maisha haikutekelezwa, yanaweza kuendelea.

 

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ambacho kimeanzishwa mwaka 1992, malengo yake makuu ni pamoja na kutoa msaada wa kisheria, kwa wazanzibar bila malipo, ushauri, na elimu ya kisheria kwa watu hasa maskini.

                                         Mwisho    

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch