Skip to main content

MWENYEKITI KAMATI SIKU 16 KUPINGA UKATILI PEMBA AWAONESHA NJIA WAJUMBE KUFANIKISHA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA::::

WAJUMBE wa kamati maalum ya kuelekea siku 16 za kupinga ukatili wa wanawake na watoto, kisiwani Pemba, wametakiwa kutoa michango yao ya hali na mali, ili kufanikisha shughuli hiyo.

 

Kauli hiyo imetolewa leo Novemba 17, 2022 na Mwenyekiti wa kamati hiyo Nassor Bilali Ali, wakati akizungumza kwenye kikao kazi cha kamati hiyo, kilichofanyika Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ chenye lengo la kupanga mikakati ya kufanikisha shughuli husika.

 

Alisema, kwa wakati na siku zilizobakia, ni lazima kwa kila taasisi ambayo inaunda kamati hiyo, kutoa fedha au kitu kinachotakiwa kufanikisha shughuli hiyo, ikiwa ni pamoja na maji, chakula na usafiri.

 

Alisema, kama jambo hilo walilianzisha kwa furaha na bashasha, sasa wakati wa kulimaliza umefika, kwa wajumbe wa kamati hiyo, kuanza wao kutoa michango yao, kabla ya kuzifuatilia tasisi zilizoombwa.

 

‘’Kwanza wajumbe waache dharura ambazo sio za msingi, pili ni wakati na wao kuwasilisha michango yao, ili kiwango cha zaidi ya shilingi milioni 6 zilizopangwa kufanikisha, shughuli hiyo zipatikane,’’alisema.

 

Mwenyekiti huyo, alisema zipo baadhi ya taasisi kama TAMWA, TUJIPE, KUKHAWA, PEGAO, ZLSC, PAFIC, ZAPDD pamoja na jumuia za wasaidizi wa sheria za wilaya, zimeshaonesha moyo wa kutoa michango hiyo.

 

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo wa kamati ya maandalizi ya kueleka siku 16 za kupinga ukatili na dhalilishaji Nassor Bilali Ali, alisema kuanzia wiki ijayo hakuna mapunziko kwa wajumbe wote, hadi pale watakapofanikisha.

 

Mjumbe wa kamati hiyo Tatu Abdalla Msellem, alisema Jumuiya ya TUJIPE, itahakikisha inafikisha mchango wake, kwenye kamati hiyo, ili kufanikisha azma hiyo.

 

‘’Tunaahidi kuchangia kiasi fulani cha fedha, ili kufanikisha shughuli hii, maana na sisi TUJIPE inatugusa hasa kwa vile wanaotetewa ni wanawake na watoto,’’alisema.

 

Mjumbe kutoka TAMWA Fat-hya Mussa Said, alisem TAMWA itahakikisha, inachangia kiasi kikubwa cha fedha, utaalamu na uchapishaji mabango ili kufikia lengo hilo.

 

‘’Hata maji, mabango na vipaza sauti naahidi kuwa TAMWA itachangia, ili kufanikisha shughuli hii, maana sisi anapotajwa mwanamke na mtoto huwa ni eneo letu pia,’’alifafanua.

 

Kwa upande wake mjumbe wa kamati hiyo Khalfan Amour Mohamed kutoka ZAPDD alisema, ili kufanikiha shughuli hiyo, atakaa na viongozi wenzake.

 

Hata hivyo Katibu wa kamati hiyo, Safia Saleh Sultan na mjumbe Hafidh Abdi, walisisitiza wajumbe kushiriki katika vikao mbali mbali, ili kufanikisha shughuli hiyo.

 

Kamati hiyo inatarajia kukutana na waandishi wa habari Novemba 24, mwaka huu katika ukumbi wa TAMWA Chake Chake Pemba, ili kutoa taarifa ya kuelekea uzinduzi a siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji.

 

Aidha kazi nyingine ambayo itafanywa na kamati hiyo ni matembezi, makongamano, mikutano ya elimu kwa wilaya nne za Pemba, kwa kukutana wazazi, waalimu na wanafunzi wa madrassa.

 

Pamoja na shughuli nyingine kama vile vipindi vya redio, kilele cha maadhimisho hayo kinatarajiwa kufanyika ukumbi wa Samail Gombani Chake chake Disemba 10, mwaka huu.

                                           Mwisho  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch